Waziri Mhagama: Waajiri Msiogope Uwepo Wa Vyama Vya Wafanyakazi Kwenye Maeneo Ya Kazi
Na: Mwandishi Wetu, Morogoro Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewataka waajiri nchini kutoogopa uwepo wa Vyama vya Wafanyakazi katika sehemu za kazi kwa kuwa ndio fursa ya pekee ya kutatua changamoto zinazojitokeza katika sehemu za kazi. Ametoa kauli hiyo jana Disemba 29, 2020 alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa sita (6) wa Taifa wa Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano uliyopo katika Hoteli ya Edema, Mkoani Morogoro. Waziri Mhagama alieleza kuwa Vyama vya wafanyakazi vimekuwa tegemeo kwa wafanyakazi hususan katika kulinda na kutetea maslahi na haki za wafanyakazi waliopo nchini, hivyo wajibu wa waajiri kutambua uwepo wa vyama vya wafanyakazi ili kuleta tija katika sehemu za kazi. “Uwepo wa Vyama Vya Wafanyakazi imekuwa ni nyenzo muhimu ambayo imeongeza tija na kujenga hali ya msukumo ...