Posts

Showing posts from February, 2021
Image
MTU mmoja ameuawa na Jogoo wake aliyekuwa amefungwa kisu mguuni kwa ajili ya mchezo uliopigwa marufuku wa kupambanisha jogoo Kusini mwa India.     Mmiliki wa jogoo alichomwa kisu usawa wa kati ya tumbo na nyonga wakati kuku huyo akijaribu kutoroka. Mwanaume huyo alipoteza maisha akiwa njiani kuelekea hospitali kwasababu ya kupoteza damu nyingi.     Polisi hivi sasa wanawatafuta watu wengine 15 waliohusika kwenye tukio hilo, ambalo lilifanyika kwenye kijiji cha Lothunur jimbo la Telangana wiki hii, Kuku huyo alishikiliwa katika kituo cha polisi kabla ya kupelekwa shambani.     Polisi wamesema mnyama huyo alikuwa akitayarishwa kwa ajili ya kushiriki mpambano alipojaribu kutoroka. Mmiliki alijaribu kumkamata lakini alichomwa na kisu hicho chenye urefu wa sentimita 7 kilichokuwa kimefungwa kwenye mguu wa kuku huyo wakati wa purukushani hizo.   Wale waliohusika katika tukio hilo wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya kutokusudia, kujihusisha na mchezo haramu wa k

Wanaswa na vipande 13 vya meno ya tembo wakisaka wateja

Image
Kikosi maalum ya kupambana na ujangili katika eneo la ikolojia ya Tarangire – Manyara, kimewakamata watu wawili katika  kijiji cha Moyaka wilaya ya Babati mkoani Manyara wakiuza vipande 13 vya meno ya tembo. Mkuu wa kikosi cha kuzuiwa ujangili (KDU) Kanda ya Kaskazini, Peter Mbanjoko leo Februari 28 amethiitisha kukamatwa watuhumiwa hao, Benard Masalu na  Yembeson Masumbuko na kupongeza kazi nzuri ambayo imefanywa na askari wa hifadhi ya Taifa ya Tarangire, Burunge WMA na Chemchem ambao wamewekeza katika eneo hilo. “Nimepata taarifa za tukio hili na tayari watuhumiwa hao wanashikiliwa na jeshi la polisi na taratibu za kuwafikisha Mahakamani zinaendelea,” amesema. Mtendaji mkuu wa Taasisi Chemchem Assosiation, Walter Pallangayo amesema kukamatwa kwa watuhumiwa hao kulitokana na taarifa za siri ambazo walizipata na wakaandaa mtego uliofanikisha kukamatwa kwao. Taasisi ya Chemchem ambayo imewekeza hoteli za kitalii na kufanya utalii wa picha katika eneo la Burunge WMA

Dismas Ten Hakuna kama Haji Manara

Image
Afisa Habari wa zamani wa Yanga Dismas Ten amesema Afisa Habari bora kwenye vilabu vya soka Tanzania ni Hassan Bumbuli wa Yanga na Idrissa Bandari wa Ndanda FC. Dismas Ten ambaye pia amewahi kuwa Afisa Habari wa Mbeya City amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo pia ameweka wazi kuwa kwa upande wa wasemaji hakuna kama Haji Mana wa Simba SC. ''Msemaji bora hakuna kama Haji Manara wa Simba SC haswa linapokuja suala la kuzungumza na kuhamasisha''. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3b38G4n via IFTTT

Auawa na jogoo wake katika mchezo wa kupambanisha kuku

Image
Mtu mmoja ameuawa na Jogoo wake aliyekuwa amefungwa kisu mguuni kwa ajili ya mchezo uliopigwa marufuku wa kupambanisha jogoo Kusini mwa India. Mmiliki wa jogoo alichomwa kisu usawa wa kati ya tumbo na nyonga wakati kuku huyo akijaribu kutoroka. Mwanaume huyo alipoteza maisha akiwa njiani kuelekea hospitali kwasababu ya kupoteza damu nyingi. Polisi hivi sasa wanawatafuta watu wengine 15 waliohusika kwenye tukio hilo, ambalo lilifanyika kwenye kijiji cha Lothunur jimbo la Telangana wiki hii, Kuku huyo alishikiliwa katika kituo cha polisi kabla ya kupelekwa shambani. Polisi wamesema mnyama huyo alikuwa akitayarishwa kwa ajili ya kushiriki mpambano alipojaribu kutoroka. Mmiliki alijaribu kumkamata lakini alichomwa na kisu hicho chenye urefu wa sentimita 7 kilichokuwa kimefungwa kwenye mguu wa kuku huyo wakati wa purukushani hizo. Wale waliohusika katika tukio hilo wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya kutokusudia, kujihusisha na mchezo haramu wa kamari na kuhodhi mchezo w

Kocha Simba Aiwekea Mtego Yanga

Image
WAKATI mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara zikiwa bado mbili, Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes, amesema licha ya kushiriki mashindano mengi tofauti, lakini hawajasahau michezo yao mitatu ya viporo kwenye ligi hiyo ambayo wanataka kushinda ili kuishusha Yanga kileleni.   Hivi sasa Simba inakamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa imekusanya pointi 42 baada ya kucheza mechi 18, ikizidiwa pointi saba na vinara wa ligi hiyo, Yanga wenye pointi 49 zilizotokana na kucheza mechi 21 ambazo ni tatu zaidi ya Simba. Kesho Jumatatu, Simba inatarajiwa kushuka uwanjani kuvaana na JKT Tanzania katika mchezo wa kiporo wa ligi kuu, utakaopigwa Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.   Endapo Simba ikifanikiwa kushinda mechi zate tatu za viporo, basi itaishusha Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo na kukaa mabingwa hao watetezi kwa tofauti ya pointi mbili.   Akizungumza na Spoti Xtra,Gomes alisema: “Hivi karibuni ratiba yetu imetubana kidogo kwani tumekuwa na mich

Majonzi:Mfanyabiashara maarufu Arusha, afariki

Image
Mfanyabiashara maarufu mkoani Arusha, Andrew Mollel ambaye alikuwa mwanzilishi na Mkurugenzi wa kampuni mbalimbali mkoani Arusha amefariki dunia na kuibua simanzi kwa wakazi wengi wa jiji hilo. Akizungumza na Mwananchi leo, Februari 28, Mbunge wa jimbo la Monduli , Fredrick Lowassa amesema kifo cha Mollel ni pigo kubwa katika jiji la Arusha kutokana na mchango wake. Lowassa amesema taratibu za mazishi wa Mollel zinaendelea kufanywa na wanafamilia lakini, kubwa ambalo Arusha watamkumbuka ni kuandaa michoro ya mradi mkubwa wa nyumba za PPF zilizopo eneo la Kijenge jijini hapa ambalo lilikuwa ni eneo lake. Mollel alikuwa pia ni mkurugenzi wa kampuni ya Happy Sausages ,Kijenge Animal Products Limited, Georges Center Ltd na AGM Holding na pia mjumbe wa bodi mbali mbali hapa nchini. Mollel pia alikuwa ni rafiki wa karibu wa Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa. Kifo cha mfanyabiashara huyu ni mfululizo wa vifo vya wafanyabiahara kadhaa katika jiji la Arusha katika siku z

Uso kwa Uso ROSA REE na wasanii wachanga wenye unyama wa hatari Aliowachagua Kufanya Collabo Nao

Image
Uso kwa Uso ROSA REE na wasanii wachanga wenye unyama wa hatari, Wafunguka baada ya kufanya NGOMA VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3sBKlJ6 via IFTTT

Baba Mzazi wa Young Killer afunguka mazito

Image
  EATV & EA Radio Digital imepiga stori na baba mzazi wa msanii wa HipHop Young Killer, anayefahamika kwa jina la Mzee Msodoki ambaye amesema chanzo cha kutokuwa sawa na mwanaye huyo ni mama yake kumwambia kwamba baba yake amefariki tangu utotoni.   Mzee Msodoki amesema mama Young Killer aliamua kumwambia hivyo mtoto wao kwa sababu aliumizwa na kitendo cha Mzee Msodoki kuukimbia ujauzito wa msanii huyo kabla hajazaliwa na kwenda kuishi nchini Congo DR. "Mama Young Killer nilikuwa nakaa naye jirani kule Mwanza, wakati huo nilikuwa nafanya kazi Saloon, tukawa kwenye mahusiano ambayo yalidumu kama miezi 6 na baadaye akaniambia nina ujauzito, sasa kwa wakati huo mimi nilikuwa sijajiandaa kulea na majukumu hivyo nikapata safari ya kwenda Congo nilivyorudi sikumkuta" ameeleza Mzee Msodoki  "Nimekuja kugundua kama mtoto yupo na ameshakuwa mkubwa ila mama yake alishamwambia kwamba baba yake ameshakufa wakati mimi nipo, ndiyo maana hata yeye haamini kama mimi ndiyo

Kisa Simba, Senzo Avamia Kambi

Image
  KATIKA kuongeza morali na mzuka wa ushindi, Mshauri wa Yanga, Senzo Mazingisa, raia wa Afrika Kusini, juzi jioni alivamia kwenye kambi ya timu hiyo na kufanya kikao na wachezaji, benchi la ufundi. Hiyo ni katika kuelekea mchezo wao wa leo Jumamosi wa Kombe la FA dhidi ya Kengold FC ya mkoani Mbeya utakaopigwa saa kumi kamili kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Yanga yenye pointi 49, ikiongoza kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara, imepanga kubeba mataji yote katika msimu huu ikiwemo huo wa ligi na Kombe la FA ambayo yote yanawaniwa na wapinzani wao Simba wenye muendelezo mzuri wa Ligi ya Mabingwa Afrika. Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumamosi, Senzo alifanya ziara hiyo ya kushtukiza katika kambi ya timu hiyo iliyopo Kijiji cha Avic Town, Kigamboni na kufanya kikao cha pamoja na wachezaji, benchi la ufundi kabla ya kuanza mazoezi.Mtoa taarifa huyo alisema kikao hicho kilitumia dakika 15 ambacho kilifanyika katikati ya uwanja na kikubwa mshauri aliwasisiti

Saudia yakanusha Bin Salman kuhusika na kifo cha Khashoggi

Image
  Saudi Arabia imekanusha vikali ripoti ya kijasusi iliyotolewa na Marekani ikifichua kuwa mrithi wa kiti cha ufalme wa nchi hiyo Mohammed bin Salman aliidhinisha mauaji ya mwandishi habari Jamal Khashoggi mwaka 2018. Taarifa iliyotolewa na wizara ya mambo ya kigeni ya Saudi Arabia imesema serikali mjini Riyadh inaipinga vikali ripoti hiyo ikisema imejaa taarifa za uzushi na tathmini isiyokubalika kuhusu utawala wa falme hiyo ya eneo la Ghuba. Tathmini hiyo ya Marekani iliyotolewa na utawala wa rais Joe Biden kutoka ripoti pana ya kijasusi imehitimisha kuwa Bin Salman aliidhinisha operesheni ya kumkamata au kumuua Khashoggi mjini Istanbul, nchini Uturuki. Hapo kabla Saudi Arabia ilisema mauaji ya Khashoggi kwenye ubalozi mdogo wa Saudi Arabia nchini Uturuki yalifanywa katika operesheni ya kihalifu na kukanusha kuhusika kwa mwanamfalme Salman. "Kwa bahati mbaya kuwa ni kweli kwamba ripoti hii, ikiwa na hitimisho lisilo sahihi, imetolewa wakati falme hii imekwisha kosoa u

Mbwa watumika kukagua wagonjwa wa Covid-19 Finland

Image
Mbwa waliofunzwa nchini Finland wana uwezo wa kugundua wagonjwa walio na maambukizi ya virusi vya corona (Covid-19). Mbwa hao waliopewa mafunzo maalum wamekuwa wakitumika katika viwanja vya ndege nchini humo tangu Septemba, kudhibiti abiria kwa sababu ya Covid-19.  Kulingana na matokeo ya awali, kiwango cha usahihi ni kati ya asilimia 95 na asilimia 100. Baada ya ukaguzi wa Covid-19 ambao unafanyika ndani ya dakika moja, abiria huruhusiwa kuendelea na safari zao kwa kutegemea na matokeo. Katika mchakato wa ukaguzi, abiria hufuta shingo zao kwa vitambaa vya kufyonza, kisha vitambaa hivyo huwekwa kwenye makopo ambapo baadaye mbwa huja kufanya ukaguzi kwa kunusa upande wa pili wa kuta za makopo hayo. Ikiwa matokeo yanaonyesha kuwa na maambukizi, abiria hupelekwa kwenye kitengo cha huduma za afya katika uwanja wa ndege. Wakati wataalam wanadai kuwa matokeo ya mbwa ni ya kuaminika zaidi kuliko vipimo vya PCR,  Dr. Anna Hielm-Björkman kutoka kitengo cha matibabu ya wanyama cha c

Jamaa Yake Amemwekea Tego, Msichana Yupo Tayari Tuwe Wapenzi ila Anaogopa Tutanasiana au Ntapata Tatizo

Image
Nimempata dada mmoja mitaa fulani, ni mzuri sana na she is sexy. Kiukweli tumependana nami nilivyomuona tu siku ya kwanza pale ofisini nilimpenda nikaomba tuwe na ukaribu. Tukaanza ukaribu basi juzi juzi hapa nikamwambia mi natamani mambo flani. Yule dada alinikubalia lakini akasema shida kubwa ni kuwa jamaa yake mshirikina alimwekea dawa hivyo tukikutana naweza pata matatizo, anasema watu wa Morogoro/waruguru ndo zao hizo. Sasa hajui atafanyaje maana anasema aliwahi achana na jamaa akawa na mtu mwingine yule jamaa aliyetembea naye alipata matatizo makubwa sana hadi ikabidi yule dada arudi akamwambie Mluguru amwachie jamaa awe salama. Toka kipindi hicho dada amekuwa hana amani anashindwa sasa afanyeje. Aliniambia maneno haya kwa uchungu sana nami nikimwona kiukweli anataka sana nimkandamize yaani hata tukiongea hivi namwona tu jinsi macho yanavyochoka nami mzuka unapanda natamani nimnaniii hivyo hivyo lakini ananikataza anasema coz she loves me hapendi nipate shida. Sasa hapa wada

Fei Toto: Tutashinda leo mechi yetu na Kengold ya Mbeya

Image
FEISAL Salum, kiungo wa Klabu ya Yanga amesema kuwa wana amini kwamba watapata ushindi kwenye mchezo wa leo wa Kombe la Shirikisho hatua ya 32 bora dhidi ya Kengold ya Mbeya. Uwanja wa Uhuru saa 10:00 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa ambapo timu ambayo itashindwa kupata matokeo itatolewa jumlajumla. Feisal amesema kwa namna ambavyo wamejiandaa inawapa nafasi kupata ushindi ndani ya uwanja kwenye mchezo huo muhimu. "Tupo sawa na tunaamini kwamba kila mchezaji anahitaji kuona timu ikishinda hivyo tutapambana kupata matokeo ndani ya uwanja. "Inawezekana kupata ushindi na nafasi yetu ipo pia tunawaheshimu wapinzani wetu hilo lipo wazi kwa kuwa nao pia wanahitaji ushindi," . from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3dSCl2g via IFTTT

Hizi Ni Baadhi Ya Mbinu Unazoshauriwa Kutumia Pale Unapokutana Na Mwanamke Usiyemfahamu ili Uweze Kumteka Kimapenzi

Image
Unaambiwa Hizi Ni Baadhi Ya Mbinu Unazoshauriwa Kutumia Pale Unapokutana Na Mwanamke Usiyemfahamu Lakini Ukavutiwa Kumpenda Na Kumhitaji 1: Unapoomba namba ya simu hakikisha huombi kwa papara, yaani usioneshe kama una shida sana na usioneshe kama unataka kumtongoza, bali onesha kama unataka tu ulafiki wa kawaida,yaani lafiki wa kuchati nae tu kawaida. 2: Akikupa namba leo kausha usimtafute leo leo, mtafute baada hata ya wiki,msalimie tu na umpigie, hapa uangalie na muda ambao unadhani mtu anakuwa free, sio kupiga simu asubuhi sana au mchana au usiku sana, piga mida ya saa mbili usiku,na usiongee nae zaidi ya dakika 5. 3: Hakikisha kila siku unamtumia msg mara 3 na kumpigia simu mara moja, yaani asbh mtakie asbh njema, mchana, jioni na usiku piga kumpa pole na heka heka za mchana, ongea nae si zaidi ya dakika 5 ili usimchoshe. 4: Hakikisha hutumii maneno ya mtaani sana mfabo oya,inakuwaje,michongo vipi, barida, mzuka, poa n.k. Tumia maneno mazuri ya busara mfano sawa, haya, ume

Jela miaka 30 kwa kumlawiti mtoto wa miaka 15

Image
  Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Serengeti imemhukumu Mageta Masaro (29) mkazi wa Nyakitono kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka 15. Hakimu mkazi mfawidhi wa Wilaya Serengeti,  Ismael Ngaile katika kesi ya jinai namba  117/2020 leo Ijumaa Februari 26, 2021 amesema ushahidi wa watu sita uliowasilishwa na Serikali haukuacha shaka. Amesema kutokana na kukithiri kwa matukio ya ubakaji mahakama inalazimika kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine. Mwendesha mashtaka wa Serikali, Renatus Zakeo amesema Aprili 24, 2020 mshtakiwa alimtumia binti aliyekuwa akiishi nyumbani kwao kumuita mtoto huyo mwanafunzi wa shule ya msingi Nyakitono na alipofika alimkamata na kumlawiti. Amesema mtoto huyo alipiga kelele na wananchi wakajitokeza na kumkamata mshtakiwa, na mtoto huyo alipopimwa iligundulika kuwa amelawitiwa. Alibainisha kuwa hawana rekodi ya matukio ya mshtakiwa lakini ameiomba mahakama itoe adhabu kulingana na kosa alilokuwa nalo.

Marekani inasema Mwanamfalme wa Saudia aliidhinisha mauaji ya Khashoggi

Image
 Ripoti ya kijasusi ya Marekani imebaini kuwa Mwnamfalme wa Saudia Arabia Mohammed bin Salman aliidhinisha mauaji ya mwandishi wa habari wa nchi hiyo aliyekuwa ukimbizini Jamal mwaka 2018. Ripoti iliyotolewa na utawala wa Bw Biden inasema mwanamfalme aliidhinisha mpango wa "kumkamata au kumuua" Khashoggi. Marekani ilitangaza vikwazo kwa makumi kadhaa ya Wasaudia lakini sio dhidi ya mwanamfalme mwenyewe. Saudi Arabia ilipinga ripoti hiyo ikiitaja kuwa "hasi, uongo na isiyokubalika ". Mwanamfalme Mohammed, ambaye anatambuliwa kama mtawala wa ufalme, amekanusha kuhusika kwa namna yoyote ile katika mauaji hayo. Khashoggi aliuawa alipokuwa akiutembelea ubalozi mdogo mjini Instanbul , Uturuki , na mwili wake ulikatwa katwa. Mwandishi huyo wa habari aliyekuwa na umri wa miaka 59 wakati mmoja aliwahi kuwa mshauri wa serikali ya Saudi Arabia na alikuwa karibu sana na utawala wa Ufalme , lakini alikosana nao na kwenda nchini Marekani mwaka 2017.

Amber Lulu Adai Kutishwa na P-Funk na Mkewe Kuhusu Ujauzito wake, P Afunguka Instagram

Image
  Amber Lulu adai kutishwa na P-Funk na mkewe kuhusu ujauzito wake, P afunguka Instagram VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3bLuMaU via IFTTT

VIDEO ya ALIKIBA akicheza ngoma ya DIAMOND, Awapa shavu WCB wote(Zuchu,Ray Vanny,Mbosso) NANDY pia

Image
VIDEO ya ALIKIBA akicheza ngoma ya DIAMOND, Awapa shavu WCB wote(Zuchu,Ray Vanny,Mbosso) NANDY pia VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/37RTOEe via IFTTT

Kauli ya Dkt. Bashiru baada ya kuapishwa Ikulu

Image
  Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Bashiru Ally, amemshukuru Rais Dkt. John Magufuli, kwa kundelea kumuamini huku akiwaomba Watanzania waendelee kumuombea ili aweze kukidhi matarajio ya Rais Dkt. Magufuli.   Kauli hiyo ameitoa hii leo Februari 27, 2021, mara baada ya kula kiapo cha kuwa Balozi na Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu Jijini Dar es Salaam, nafasi ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Balozi John Kijazi, aliyetangulia mbele za haki Februari 17 mwaka huu. "Leo siwezi kusema mengi kwa sababu mbili, ya kwanza ni kwa mazingira ambayo nimepata uteuzi huu, ulinipa kazi ambazo zingeweza kuchukua mwezi mzima na niongeondoka kesho au keshokutwa jana jioni napata taarifa kwenye mitandao kwamba umeniteua," amesema Balozi Dkt. Bashiru Ally Aidha, ameongeza kuwa "Bado natafakari sana nitafanya nini na vipi ili kukidhi matarajio yako kwa imani uliyonipa kwa mfulululizo, niwaombe Watanzania wote mniombee ili niweze kukidhi matarajio ya Mh. Rais". Kabla ya uteuzi huo hiyo,

Mobeto Aungana na Sarah Kumkabili Kajala

Image
  MWANAMITINDO wa kimataifa na msanii wa Bongo Fleva, Hamisa Mobeto, anadaiwa kuungana na aliyekuwa mke wa msanii mwenzake, Rajab Abdul ‘Harmonize’, Sarah Michelotti, IJUMAA WIKIENDA limedokezwa. Kwa mujibu wa watu wa karibu wa Mobeto, kwa sasa kuna muunganiko mzuri kati ya Mobeto na Sarah ambaye alimwagana na Harmonize mwishoni mwa mwaka jana, kabla ya jamaa huyo kuibuka kwa staa wa Bongo Movies, Kajala Masanja ambao kwa sasa ndiyo kapo inayotetemesha zaidi kwenye mitandao ya kijamii Sasa, ubuyu wa moto unaeleza kwamba, baada ya Mobeto kutibuana na Kajala kiasi cha kumuweka ndani kwa sababu ya lile sakata la mwanaye Paula kurekodiwa video chafu akiwa na msanii Rayvanny kisha kusambaa mitandaoni, basi bifu limekuwa zito kiasi cha kuomba msaada wa hali na mali kutoka kwa Sarah ambaye naye ana bifu na Harmonize kwa kuwa hawakuachana vizuri. Gazeti la IJUMAA WIKIENDA limefuatilia nyendo za Mobeto na Sarah na kung’amua kwamba, kwa sasa ni mashosti walioshibana. Ukaribu wao unadhiris

Je, Mvi ni Dalili ya Uzee au ni Kitu Gani...?

Image
Kama mvi ni kipimo cha busara.......... Kwa nini zifichwe? Kwa zamani ingekuwa ni muhali mkubwa mtu kuuliza swali la aina hii, kwa sababu mvi zinahesabiwa kama dalili ya busara, bila shaka zikihusianishwa na kuona mengi ambayo ni wenye umri mkubwa tu waliokuwa na nafasi hiyo. Lakini leo, mvi ni kisirani na karibu kila mtu anajaribu kuzikimbia, kwani kuendalea kuwa kijana ni sifa kubwa. Kwa sasa uzee unanuka na kila mmoja anajaribu kuukimbia kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kukana umri na kujirudisha nyuma kimatendo. Kwa kifupi hii ndiyo historia ya mvi, usiziogope bure! Karibu rangi zote asilia za nywele zinatoka kwenye kitu kiitwacho melanin, ambacho huzalishwa na mwili kutokana na seli zinazofahamika kama melenocytes. Nywele zinapobadilika na kuwa nyeupe ina maana kwamba, melenocytes haizalishi tena melanin. Mabadiliko haya ya nywele kutoka rangi nyeusi na kukosa rangi (mvi) siyo hatua ya siku moja bali mwaka na miaka, kwani nywele moja hubadilika baada ya muda mrefu na nyingine

Kimenuka, Sibomana Naye Aipeleka Yanga Fifa

Image
MSHAMBULIAJI wa zamani wa Yanga, Patrick Sibomana ameibuka na kudai yupo kwenye mpango wa kuifungulia mashitaka Klabu ya Yanga kwenye Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), kwa kile alichokieleza kuwa, ukiukwaji wa makubaliano ya malipo ya stahiki zake.   Hii inakuja ikiwa ni siku chache baada ya Fifa kuitaka Yanga kumlipa aliyekuwa mshambuliaji wa timu hiyo, Amissi Tambwe.   Sibomana aliichezea Yanga kwa msimu mmoja uliopita kabla ya kuachwa mwishoni mwa msimu huo.Akizungumza na Championi Jumamosi, Sibomana alisema: “Tulikubaliana kwamba Yanga wanilipe fedha zangu za usajili ambazo zilibaki kiasi cha dola 10,000 (Sh mil 23).   “Kwa kuwa niliishi nao vizuri na nilijua timu ilikuwa haina fedha, tulipanga wanilipe kwanza fedha ya miezi mitatu pamoja na fedha ya usajili ambayo jumla yake ni dola 16,000 (Sh mil 36.9) ambayo nilikatwa kodi hadi kufikia dola 14,500 (Sh mil 33.4). “Tukakubaliana kwamba wangenilipa Oktoba 30, mwaka jana ambapo walinipatia dola 3,000 (Sh m

Gomes Ampa Mapumziko Maalum Luis Simba

Image
KOCHA Mkuu wa Simba, Mfaransa Didier Gomes ametoa mapumziko ya siku nne kwa baadhi ya nyota wake akiwemo Luis Miquissone.   Hiyo ni baada ya kumalizika kwa mchezo wa pili wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly ya nchini Misri uliochezwa Jumanne iliyopita kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.   Mchezo huo ulimalizika kwa Simba kushinda bao 1-0 lililofungwa na Miquissone baada ya kugongeana vizuri na Mzambia Clatous Chama. Akizungumza na Championi Jumamosi, Gomes alisema mapumziko hayo waliyaanza Jumatano yatamalizika Jumamosi na kuanza mazoezi pamoja na wenzao.   Gomes alisema kuwa wachezaji wake hao walitumia nguvu nyingi katika mchezo huo dhidi ya Ahly zilizowawezesha kupata ushindi huo na kukaa kileleni katika msimamo wa Ligi ya Mabingwa Afrika wakiwa na pointi 6.   Aliongeza kuwa katika mchezo wao wa jana wa Kombe la FA alitarajia kuwatumia wachezaji ambao hawakucheza mechi ya Al Ahly ili kutoa nafasi ya kupumzika.   “Nim

Huyu Hapa Muuguzi Aliyenusurika Ajali Tatu za Meli Ikiwemo Titanic

Image
  Violet Constance Jessop alikuwa Nesi akihudumu kwenye Meli na anajulikana zaidi kwa kunusurika ajali tatu zilizowahi kutokea ikiwemo meli ya #Titanic ambayo ilitokea April 1912, akiwa na miaka 24 Ajali yake ya kwanza kunusurika ilikuwa 1911 ambapo ndio alikuwa anaanza kazi kwenye Meli ya Olympic ambayo kimsingi haikusababisha vifo Ajali yake ya mwisho ilikuwa kipindi cha Vita ya Kwanza ya Dunia, Novemba 1916 akiwa ndani ya Meli ya #Britannic ambayo ilizama katika Bahari ya Aegean kutokana na mlipuko Violet Constance Jessop alizaliwa Oktoba 2, 1887 na alifariki Mei 5, 1971 Nchini Uingereza akiwa na miaka 83 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/39Lvk0R via IFTTT

Je Wajua Adolf Hitler Alikuwa na Korodani Moja?...Yafuatayo ni mambo usiyoyajua kuhusu Adolf Hitler

Image
Nani ambaye hamjui Dikteta Adolf Hitler? Adolf Hitler ni mtawala maarufu zaidi katika karne ya ishirini, kiongozi wa chama cha Kinazi aliyeitawala ujeruman kati ya mwaka 1934 mpaka 1945. Kama ulikuwa hujui, hitler ndiye mwanzilishi mkuu wa vita ya pili ya dunia. Yafuatayo ni mambo  usiyoyajua kuhusu Adolf Hitler. Alipendelea zaidi kuangalia Filamu za mauaji, wafuasi wake walipenda kurekodi video pale walipokuwa wanawauwa wafungwa na kumpelekea Hitler! Adolf Hitler Ndiye aliyeanzisha sheria ya kutovuta sigara hadharani. Alikuwa mvuta sigara enzi za ujana wake na alikuja kuacha baadae akidai ni utumiaji mbaya wa fedha. Licha ya kufurahia Kuua sana binadamu, adolf alipinga sana ukatili wa wanyama, na alikuwa hali nyama ya aina yeyote ile. Hitler aliokolewa kufa maji na mfanyakazi wa kanisa alipokuwa na umri wa miaka minne (4), na kwa kipindi hicho, hitler ilipenda saana awe mfanyakazi wa kanisa akiwa mkubwa. Mpenzi wa kwanza wa Hitler alikuwa myahudi na aliona aibu kumuelez

Top 10 ya Madictator Waliouwa Watu Wengi zaidi Duniani....

Image
10. Yakubu Gowon Nigeria : 1966 - 1975 Total kills : 1.1 Million 9.  Mengistu Haile Mariam Ethiopia : 1974 - 1991 Total kills : 1.5 million  8. Kim II Sung North Korea : 1948 - 1994 Total killing : 1.6 million  7. Pol Pot Cambodia : 1963 - 1981 Total kills : 1.7 million 6. Ismail Enver Pasha Turkey : 1913 - 1919 Total kills : 2.5 million  5. Hideki Tojo Japan : 1941 - 1944 Total klls : 5 million  4. Leopold II of Belgium Belgium : 1865 - 1909 Total kills : 15 million  3. Adolf Hitler German : 1934 - 1945 Total kills : 17 million  2. Jozef Stalin The Sovjet : 1922 - 1953 Total kills : 23 million 1. Mao Ze Dong China : 1943 - 1976 Total kills : 78 million from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2X7xeSG via IFTTT

Je? Umeachwa na Mke/Mume/Mchumba na bado unampenda? Mpigie Bi Mariam.

Image
BIBI MARIAM.Anawashukuru wale wanao piga simu za shukrani na kutoa shuuda jinsi Tiba zake zinavyo saidia watu Je? Umeachwa na mke/ mume/mchumba na bado unampenda ? Kuna mtu unamtaka unashindwa kumwambia? BIBI. Mariam humvuta mume, mke ,mchumba na mtu yoyote unaye muhitaji katika mahusiano na kumfanya atimize unachokiitaji kutoka kwakwe na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako hata kama yupo mbali ndani ya masaa .(2) tu na kukutafufuta yeye mwenyewe ,unamatatizo ya kushika mimba ? Na ukishishika zinaharibika?dawa zipo .  PIA.TUNAYO DAWA YA ASILI YA NGUVU ZA KIUME YENYE KUTIBU MATATIZO MATATU KWA WAKATI MMOJA  (1)nguvu za kiume , (2) kurefusha na kunenepesha uume saizi uyipendayo ,nchi (1-7)  (3)kuchelewa kufika kilelen, Yajue .matatizo yanayosababisha upungufu wa nguvu za kiume . (1)ngiri ya kupanda na kushuka  (2)korodani moja kuvimba  (3)tumbo kuunguruma,kujaa yes. (4)kisuk ari  (5)presha (6)kiuno kuuma  (7)kutopata choo  Tunatibu kisukari Suki (14)vidonda vya tum

Soma Funzo Hili Kutoka Kwa Michael Jackson Aliyetaka Kuishi Miaka 150 Kutokana na Utajiri Wake Lakini Hakuweza

Image
 Michael Jackson wanted to live for 150 years. He appointed 12 doctors at home who would daily examine him from hair to toenails. His food was always tested in laboratory before serving. Another 15 people were appointed to look after his daily exercise and workout. His bed had the technology to regulate the oxygen level. Organ donors were kept ready so that whenever needed they could immediately donate their organ . The maintenance of these donors were taken care of by him. He was proceeding with a dream of living for 150 years. Alas ! He failed. On 25th June 2009, at the age of 50, his heart stopped functioning. The constant effort of those 12 doctors didn't work. Even, the combined efforts of doctors from Los Angeles and California too couldn't save him. The person who would never put a step forward without the doctors suggestion for his last 25 years, couldn't fulfil his dream of living 150 years. Jackson's final journey was watched live by 2

Nandy Afanyiwa Hujuma Nzito

Image
  PISI kali kunako muziki wa Bongo Fleva, Faustina Charles Mfinanga ‘Nandy’, anadaiwa kufanyiwa hujuma nzito, IJUMAA WIKIENDA lina kisanga kamili.   Hujuma hiyo imeelekezwa kwenye wimbo wake mpya alioutoa na nguli wa muziki barani Afrika, Le Grand Mopao Koffi Olomide unaokwenda kwa jina la Leo Leo.   Inasemekana wimbo huo alioutoa kwa mfumo wa audi (sauti) umeshindwa kufikisha wasikilizaji milioni moja ndani ya wiki moja kwenye Mtandao wa YouTube kutokana na kiki zilizoingizwa mitandaoni kwa makusudi na kuufanya wimbo huo usiwe gumzo.   Watu wa karibu wa Nandy wanasema kuwa, Nandy ameshagundua njama hizo kuwa zilipangwa na watu ili kumuharibia kwa sababu wimbo wake huo ungekamata zaidi ya sasa pamoja na kwamba bado unasikilizwa mno na kutingisha mitandaoni.   Inaelezwa kwamba, washindani wake walipoona kuna kila dalili wimbo huo ukafunika nyimbo zote zilizotoka wiki iliyopita ndiyo maana ikatafutwa mbinu ya kuweza kuuzima moto wake.   “Unajua Nandy mwenyewe anajua wazi kwa

Polisi Mbeya watuhumiwa kuua

Image
  Kijana Ivan Kabambala, mwenye umri wa miaka (17) mkazi wa Kagera, Halmashauri ya Jiji la Mbeya, amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, baada ya kupigwa risasi mgongoni na  polisi mkoani humo.   Akizungumzia tukio hilo, Baba mzazi wa marehemu, Aggrey Kabambala, amesema kuwa tukio limetokea majira ya saa 2:00 usiku katika eneo ambalo marehemu alikuwa anafanyakazi ya kuosha magari. Mkuu wa wilaya ya Mbeya, William Ntinika, ametoa pole kwa familia ya marehemu Ivan na kuwaomba wananchi wa Mtaa wa Kagera kuwa watulivu wakati wakisubiri ukweli wa tukio hilo. Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, amesema marehemu Ivan ni miongoni mwa vijana 20 waliokuwa wakipanga njama za kufanya uhalifu na kwamba baada ya kupata taarifa Jeshi la Polisi ilifika eneo la tukio. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2MAGM6A via IFTTT

Joe Biden azungumza na Kenyatta

Image
Rais wa Marekani Joe Biden amefanya mazungumzo ya simu na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na kuelezea hamu ya Marekani kushirikiana na nchi ya Kenya. Kulingana na Ikulu ya White House, Biden amesisitiza umuhimu wa uhusiano thabiti kati ya Marekani na Kenya wakati wa mazungumzo hayo. Kwa mujibu wa habari, Marekani imesisitiza azma yake ya kufanya kazi kwa karibu na Kenya kukuza amani na usalama wa eneo. Taarifa hiyo ilisema, "Rais Biden amesifu uongozi wa Kenya, kujitolea kwake kupambana na ugaidi, ukuaji wa uchumi, mapambano dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa na maendeleo endelevu,"  Viongozi hao wawili pia walizungumzia mgogoro wa katika mkoa wa Tigray wa Ethiopia. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2ZVjbAl via IFTTT

Wanafunzi wa Kike 300 Watekwa

Image
  Wanafunzi 300 katika Jimbo la #Zamfara lililoko Kaskazini Magharibu mwa Nigeria wametekwa nyara Ijumaa asubuhi baada ya shambulio Msemaji wa Gavana wa Jimbo amethibitisha kutokea kwa shambulio hilo. Hili ni tukio la karibuni la utekaji unaowahusisha Watu wengi Watu wenye silaha huwateka Wasichana wa Shule kwa ajili ya kupata fedha. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3dOnrd7 via IFTTT

Wapiga Debe 30 Wakamatwa Stendi Mpya iliyoko Mbezi Luis

Image
Wapiga debe 30 wamekamatwa katika Kituo cha Mabasi cha Magufuli Bus Terminal kwa kusababisha usumbufu kwa Abiria Meneja wa Stendi, Maira Mkama amesema wapiga debe waliokuwa Ubungo, Riverside na Mbezi wamevamia stendi hapo Mkama ameliomba Jeshi la Polisi Kanda Maalum kuongeza Askari na gari kwaajili ya doria ili kuwakamata wapiga debe watakaoendelea na shughuli hiyo Stendi mpya ya Mabasi yaendayo Mikoani na Nchi jirani imeanza kutumika Februari 25 ambapo Stendi ya Ubungo imefikia ukomo wa matumizi from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3aUdE3u via IFTTT

PROFESSOR JAY awaonya wasanii wapenda KIKI, Wafunguka na STAMINA, Rais MAGUFULI kuipenda BABA

Image
PROFESSOR JAY awaonya wasanii wapenda KIKI, Wafunguka na STAMINA, Rais MAGUFULI kuipenda BABA VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3aTxyvt via IFTTT

Rais Magufuli ampa siku 7 Simbachawene

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli, amempa siku saba Waziri wa Mambo ya Ndani George Simbachawene, ahakikishe wastaafu wote wa jeshi la polisi wanaodai mafao yao  Rais Dkt. Magufuli ametoa maagizo hayo Februari 26, 2021, wakati akizungumza na Askari Polisi mara baada ya kuzindua Chuo cha Maafisa wa Polisi Kurasini Dar es Salaam, ambapo awali IGP Sirro alimuomba Rais Magufuli awasaidie wastaafu ambao hawajalipwa mafao yao waweze kulipwa kwa wakati. "Waziri Simbachawene nakuagiza nenda kashughulikie malipo ya wastaafu na ikiwezekana ndani ya wiki moja wawe wamelipwa, tuliwatumia vizuri wakati hawajastaafu ni lazima wafaidike na kustaafu kwao hakuna kinachoshindikana pesa ipo," amesema Rais Dkt. Magufuli. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3qYj1nT via IFTTT

Kim amrejesha Yondani taifa stars

Image
  Kocha wa timu ya taifa ya Tanznaia Taifa Stars Kim Poulsen amemrejesha kikosini mlizi kisiki na mkongwe Kelvin Yondani kwenye kikosi cha wachezaji 42 alichokiita leo, kitakachoingia kambini kujiandaa kwa michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Kenya na ya kufuzu AFCON. Taifa stars itacheza pia michezo miwili ya kufuzu AFCON mwishoni mwa mwezi Machi ikiwa ni michezo ya kundi J, ambapo kikosi Tanzania kitakuwa na mchezo dhidi ya Equatorial Guinea  Machi 22, 2021. mchezo huuutachezwa ugenini na Machi 30 itacheza dhidi ya Libya mchezo utakao chezwa Dar es salaam. Kwenye kundi hilo taifa Stars ipo nafasi ya 3 ikiwa na alama 4, wakati Tunisia ndio vinara wa kundi hilo na wameshafuzu wakiwa na alama 10 na nafasi ya pili wapo Equatorial Guinea wenye alama 4 na Libya ndio wanaburuza mkia wakiwa na 3. Kikosi kamili kilichoitwa na kocha Kim Poulsen from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3kpl3uA via IFTTT

Huyu Hapa Muuza Madawa ya Kulevya Aliyependwa na Wananchi Mpaka Kupewa Jina la Yesu na Mlinzi wa Amani

Image
TAJIRI WA UNGA AKAWA MWEMA MPAKA AKAITWA YESU Christopher Coke a.k.a Dudus, ni tajiri wa dawa za kulevya, akiongoza genge la Shower Posse. Genge hilo na mtandao mzima wa unga, Dudus au President alirithi kutoka kwa baba yake, Lester Coke a.k.a Jim Brown au Ba-Bye aliyeuawa gerezani mwaka 1992. Shower Posse makao makuu yake yapo Tivoli Gardens, Kingston, Jamaica. Dudu alikuwa mtu mwema. Alisaidia fedha familia maskini, alilipia ada wanafunzi ambao wazazi wao hawakuwa na uwezo, zaidi alitengeneza ajira nyingi kwa vijana. Hayo yalisababisha apendwe sana. Dudus aliitwa Rais wa Tivoli Gardens, alilindwa na kila mwananchi. Serikali ya Jamaica pia ilimlinda, maana alikuwa mfadhili wa viongozi. Marekani ilitaka Dudus akamatwe lakini Serikali ya Jamaica haikutekeleza. Dudus alipokamatwa na Marekani mwaka 2010, kwananchi wa Jamaica, hususan wakazi wa Tivoli Gardens, waliingia mitaani na kuandamana, wakitaka Dudus aachiwe huru. Wananchi walikuwa na mabango yaliyoandikwa kuwa Dud

Yafahamu Mafuta ya Kuvuta Pesa za Majini na Jini wa Mali - Shantaru

Image
MAFUTA YA KUVUTA PESA ZA MAJINI AU JINI WA UTAJIRI Pesa Kwa wanayoyafahamu wanajua faida zake. Haya ni mafuta yanayotumiwa sana katika kuvuta pesa za majini ama kuita Jini wa Utajiri. Ni mafuta yenye kazi nyingi za umuhimu na kimaendeleo, shida ni kwamba hayapatikani kiurahisi sana kwa ajili ya umuhimu wake na mafanikio yake. MATUMIZI YAKE : Tafuta kitambaa cheupe mita moja kitandike katikati ya sakafu ndani ya chumba, kisha nyunyuzia poda katika kitambaa chote. Chukua noti ya pesa ya nchi yoyote iweke katikati ya kitambaa hicho Dondosha tone moja la mafuta ya Shantar Washa mshumaa warangi ya njano mbele ya kitambaa hicho. Nuwia ukitakacho huku ukiwa umefumba macho takribani dakika 7 kisha fumbua macho yako utaona maajabu Kwa mahaitaji ya mafuta haya piga ☎️ +255 655 040 967 ---------- @ostadhi_juma_ramadhani-----**ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI(+255 655 040 967) NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYOSAIDIA...** Je una NUKSI zisizo kwisha.!? JE ume

Amber Lulu ajitokeza hadhani kuonesha ujauzito wake kwa mara ya kwanza

Image
Kwa mara ya kwanza msanii wa BongoFleva Amber Lulu amejitokeza hadharani kuonesha ujauzito wake kwenye 'Baby Shower' yake iliyofanyika maeneo ya Mikocheni ambayo ilihudhuriwa na mastaa mbalimbali wa kike. Wakati yupo kwenye 'red carpet' anafanya mahojiano na waandishi wa habari, Amber Lulu amesema anafuraha sana kuelekea kuwa mama mpya mjini ila cha ajabu hamfahamu ni mwanaume gani aliyempa ujauzito huo "Nijasikia vizuri kwa sababu naenda kuwa mama mpya mjini na kuna vitu vingi ambavyo vimebadilika na nahitaji kuvifanya, mimi mwenyewe baba wa mtoto simjui ila yupo na sio P Funk Majani, labda msubiri nikijifungua" amesema Amber Lulu from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2ZVOISE via IFTTT

Nzige wahamia Siha na Simanjiro, Waziri afika eneo la tukio

Image
Waziri wa Kilimo Prof Adolph Mkenda pamoja na Naibu waziri wa Kilimo wamefika Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro na Simanjiro Mkoani Manyara baada ya nzige wa Jangwani kuhaminia maeneo hayo. Prof Mkenda amesema nzige hao hawajaleta athari zozote nakuwataka wananchi kutokuwa na taharuki wakati wanalifanyia kazi suala hilo ikiwemo kutumia ndege kunyunyiza viatilifu. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/37S1i9Y via IFTTT

Hasira za Carlinhos Zamvuruga Kaze Yanga

Image
  UPO uwezekano mkubwa wa Kocha Mkuu wa Yanga Mrundi Cedric Kaze kukifumua kikosi chake cha kwanza na kumuingiza kiungo mshambuliaji Carlos Fernandez ‘Carlinhos’. Kiungo huyo katika mchezo uliopita wa Ligi Kuu Bara ndiye aliyewafungia bao la ushindi dhidi ya Mtibwa Sugar akitokea benchi katika ushindi wa bao 1-0 walioupata kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar, lakini alionekana kuwa ni mwenye hasira na hakutaka kushangilia bao hilo. Awali kiungo huyo alikuwa hapati nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo, licha ya kupona majeraha yake aliyokuwa akiyauguza na inadaiwa kuwa nicho ni chanzo cha kuwa na hasira ya kutopangwa wakati alikuwa fiti, ndiyo maana hata bao lake hakulishangilia. Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Ijumaa, kutoka ndani ya kambi ya timu hiyo iliyoweka Avic Town, Kigamboni nje ya Dar kiungo huyo ameingizwa kwenye program na wachezaji wa kikosi cha kwanza katika mazoezi ya siku tatu wanayoendelea kuyafanya. Mtoa taarifa huyo alisema upo

Amber Lulu Amejibu “Mtoto Hana Baba, Majani Simjui” – Video

Image
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Amber Lulu amegoma kumuweka wazi baba wa mtoto wake ajaye huku akisisitiza kuwa sio P-Funk Majani ambaye watu wengi wamekuwa wakidai kuwa ndio baba wa mtoto wake. Amber amesema hayo usiku wa kuamkia leo kwenye hafla ya Baby shower yake iliyofanyika pale Hekima Garden, maeneo ya Mikocheni jijini Dar es Salaam. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3bIG3sm via IFTTT

Gigy Money Amtetea Rayavnny – “Paula Kataka Mwenyewe” -Video

Image
  MSANII wa muziki Bongo Fleva, Gift Stanford maarufu ‘Gigy Money’ usiku wa kuamkia leo akifanya mahojiano na wanahabari amezungumzia lkuhusu sakata la mtoto wa Kajala Paula na Rayvanny. “Sioni tatizo kwa Rayvanny mwanangu mimi sio chizi, mtoto wa kike ana nguvu yake huwezi kumzuia kufanya, wangapi wana mahusiano na watu walio wazidi umri? Mimi kama mama ningewabariki tu. VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3aWYdYs via IFTTT

Abiria Kenya Airways Ruhusa Kulipia Viti vya Ziada Kujikinga na Corona

Image
ABIRIA wa ndege za shirika la Kenya Airways (KQ) sasa wanaweza kununua kiti cha ziada cha pembeni wakati wanasafiri iwapo wanataka kuwa mbali na abiria wengine. Huduma hiyo inayoitwa Economy Max itakuwepo kwa watu wanaotaka faragha na usalama hasa wakati huu wa kuenea kwa ugonjwa wa Covid-19. Wanaotaka kufanya hivyo watalazimika kununua mapema kiti kimoja au zaidi katika muda wa kati ya saa tatu na 48 kabla ya kusafiri. Abiria wa ndani watalipa Dola 15 kwa ajili ya kiti cha ziada na Dola 20 kwa viwili. Abiria kutoka au kwenda Nairobi kutoka Amerika watalipa Dola 120 kwa kiti cha ziada na Dola 230 kwa viti viwili. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2ZTqgBC via IFTTT