Posts

Showing posts from October, 2020

Kufungwa Kwa Bar ya Last Minute ..Irene Uwoya Adaiwa Kufulia, Vyuma Vimekaza

Image
VYUMA vimekaza! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mwanamama na staa wa fi lamu za Kibongo, Irene Uwoya, kufunga baa yake ya Last Minute iliyopo Sinza, Dar, huku sababu zikiwa hazijulikani. Baa hiyo ambayo mbali na kazi yake ya fi lamu, ndiyo ilikuwa ikimuingizia kipato na kumpa jeuri mjini hapa mwanamama huyo, ilifungwa huku taarifa nyingi zilikuwa zikisambaa zikianisha sababu za kufungwa kwa baa hiyo. VYANZO VINASEMAJE Taarifa kutoka katika vyanzo mbalimbali zimesema kuwa, msanii huyo alikosa mtaji wa kuendesha biashara yake na ndiyo sababu akaamua kuifunga. “Hana lolote zaidi ya kufulia na kukosa mtaji wa biashara japo anafi cha tu,’’ kilisema chanzo kimoja kilichoomba kuhifadhiwa jina lake. Haikuishia hapo mmoja wa watu wake wa karibu na Uwoya ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, aliliambia Gazeti la Amani kuwa, Uwoya kakosa kodi ya kulipia pango na hata kwenye mapato ya serikali na ndiyo maana akaamua kuifunga. “Sababu kubwa ya Uwoya kuifunga hiyo baa ni kutokana n

Ex wa Aunt Aibua Mambo Mtandaoni "Aunty Anapenda Sana Kutawala Wanaume"

Image
HAYA mambo yakuachana halafu mnaanza kuongeleana vibaya mtandaoni si ushamba huu? Haya buana mapema wiki hii aliyekuwa mpenzi (EX) wa msanii wa filamu nchini Aunt Ezekiel, Alfo Alfo ameonekana kumkandia bidada kuwa hafai. Alfo aliulizwa na shabiki mmoja huko mtandaoni kuwa kwanini aliachana na Aunt, ambapo alijibu kuwa sababu zipo nyingi ila moja ni kwamba mrembo huyo alikuwa anapenda sana kuwatawala wanaume lakini kwake haikuwezekana kwa hiyo ndio maana wakaachana. “ Aunt like to control men, me Alfo no possible,” aliandika Alfo kwa kimombo. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2HRS4AU via IFTTT

RC DSM atoa onyo kwa watakaotaka kuvuruga amani

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge, ametoa onyo kwa watu au vikundi vya watu vilivyopanga kufanya vurugu na kusema kuwa yeyote atakayejaribu kuvuruga amani kwenye mkoa huo atawajibishwa kwa mujibu wa Sheria. RC Kunenge, ametoa kauli hiyo hii leo Oktoba 31, 2020, wakati wa uzinduzi wa baraza la wafanyakazi wa shirika la uwakala wa Meli Tanzania, na kuongeza kuwa kwa kuwa hali ya usalama ndani ya jiji hilo ni shwari, hivyo asitokee yeyote atakayevuruga hali hiyo. "Tumeona hali ni shwari, tumemaliza kupiga kura na washindi wametangazwa, kwahiyo kwa lugha inayotumika sasa ni kuwa Dar es Salaam ni ya kijani, naomba tuendelee kuwa watulivu, serikali imejipanga na vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga vizuri, ila yeyote ambaye ataonekana kuhatarisha usalama au atakayefanya matendo yatakayopelekea kuvunjika kwa amani hatutamvumilia aache Jiji letu liendelee kuwa na amani", amesema RC Kunenge. Wakati huohuo RC Kunenge, ametembelea ujenzi wa stand mpya ya

Polepole: JPM Kuapishwa Novemba 15 “Hakuna Sherehe”

Image
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema kuwa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ataapishwa rasmi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, Alhamisi ijayo Novemba 5, 2020. Polepole amesema hayo leo Jumamosi, Oktoba 31, 2020, jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanahabari na kuongeza kuwa ushindi uliyopatikana kwa CCM ni historia kubwa na heshima kwa chama hicho tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini. “Tangu tukiengia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa, haijawahi kutokea, CCM tumeshinda maradufu (zaidi ya asilimia 84) Urasi wa Tanzania na zaidi ya asilimia 76 nafasi ya urais Zanzibar, tumepata takribani viti vyote, ni heshima kubwa sana kwa chama chetu. “Kesho Dkt. Magufuli atapokea hati ya ushindi kuwa ndiye Rais Mteule wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sherehe itakuwa ndogo tu ya takribani watu 400 kwa ajili ya kuwakilisha, h

Shamsa, Faiza Wafarijiana Kutendwa na Wanaume

Image
STAA wa filamu za Bongo Muvi, Shamsa Ford amefarijiana na staa mwenziye ambaye ni mjasiriamali, Faiza Ally kuwa kutendwa na wanaume ambao wamezaa nao kumewafanya wakawa wanawake wenye maendeleo na ndoto kubwa sana. Akizungumza na Amani, Shamsa alisema kuwa yeye na Faiza wakizungumza wanaweza kusikilizana sana kwa sababu wamepitia machungu ya kulea wao watoto wenyewe tena kwa shida lakini wamesimama. “Mwanamke yeyote ambaye amepitia matatizo ya kulea mtoto mwenyewe anaweza kujua nazungumza nini na ndivyo ilivyokuwa kwa mimi na Faiza, tunaweza tukazungumza lugha moja na tukaelewana na pia ni watu tunaofarijiana sana kwa kweli na tutatoboa tu tukiwa wenyewe hivihivi bila mwanaume pembeni yetu,” alisema Shamsa ambaye analea mtoto wake Terry mwenyewe bila baba. Kwa upande wa Faiza alisema kuwa anapenda siku zote kumchukulia mfano Shamsa kwa sababu amepitia hali hiyo na mpaka sasa anapitia lakini hatetereki. “Tukiwa na kitu chochote kigumu kinatukabili mimi na Shamsa, tunaangaliana

Kaze Atafuta Rekodi Mpya Leo Yanga

Image
LEO Jumamosi, Kocha Mkuu wa Yanga anatarajiwa kuandika historia mpya wakati timu hiyo ikijiandaa kuwavaa Biashara United ya mkoani Mara katika mchezo wa raundi ya nane ya Ligi Kuu Bara.   Mchezo huo ni muhimu kwa Yanga ambao kama watashinda, watafi kisha pointi 22, na kuzidiwa mchezo mmoja na Azam ambao jana walitarajia kucheza na JKT Tanzania. Yanga hadi hivi sasa ikicheza michezo saba, hajaipoteza na imefanikiwa kushinda michezo yake sita mfululizo huku wakitoa sare ya 1-1 dhidi ya Prisons ikiwa ni mechi yao ya kwanza ya msimu huu.Hata hivyo mchezo dhidi ya Biashara hautarajiwi kuwa mwepesi kutokana na ubora wa timu zote.   Biashara wanashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakiwa wamejikusanyia pointi 16 wakicheza michezo nane. Rekodi anayoisaka Kaze ni kupata ushindi wa kwanza kwenye Uwanja wa Karume, Musoma ambao tangu Biashara imepanda kucheza ligi, Yanga haijawahi kupata ushindi wowote.Yanga wamekutana na Biashara kwenye uwanja huo mara mbili kati ya mic

Rais wa Belarus “anayemgusa Askari au Mwanajeshi angalau aondoke bila mikono”

Image
Wakati mamia ya wananchi wakiandamana kushinikiza ajiuzulu, Rais wa Belarus, Alexander Lukashenko amesema yeyote anayemgusa Askari au Mwanajeshi angalau aondoke bila mikono. Wanafunzi, Wafanyakazi wa Viwandani na Wastaafu wametikia wito wa Kiongozi wa upinzani, Sviatlana Tsikhanouskaya na kugoma ili kumlazimisha Rais Lukashenko kufanya Uchaguzi mpya kufuatia miezi ya maandamano. Belarus imeingia katika mgogorowa kisiasa baada ya Rais huyo ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 26 kutuhumiwa kuiba kura katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika. Hata hivyo, amekanusha mashtaka hayo na kuendelea kubaki madarakani. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/34K0tPC via IFTTT

Wasanii Alikiba na Harmonize waandika ujumbe huu wa kumpongeza Rais Magufuli baada ya kushinda uchaguzi

Image
Baada ya matokeo kutangazwa ya kuwa kwa awamu ya pili Dkt. John Pombe Magufuli anaenda kuliongoza taifa la Tanzania tena na watu wengi kumpongeza kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii Wasanii Alikiba na Harmonize hawakuwa nyuma na wao wamempongeza Rais Magufuli kwa kuchaguliwa na wananchi kulingooza taifa la Tanzania kwa mara nyingine tena. Kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii wameandika haya. ALIKIBA. Hongera kwa ushindi wa kishindo Mheshimiwa Rais Mteule, Dr John Pombe Magufuli na Makamu wa Rais Mteule @samia_suluhu_hassan. Watanzania tumeonyesha imani kubwa nanyi kwa kuwaongezea miaka mengine 5 ya kuliongoza taifa letu, nawaombea kwa Allah awaongoze katika kila hatua ya uongozi wenu kwenye taifa hili, muongoze kwa amani, upendo na busara zaidi katika kuisogeza Tanzania katika maendeleo makubwa zaidi. Mwenyezi Aibariki Tanzania 🇹🇿, Dr John Pombe Magufuli na viongozi wote waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu. Tudumishe Amani na Upendo. @asas_dairies @ccmtanzania. @

Morrison Aipa Bodi ya Ligi Mamilioni

Image
MBALI na kupigwa faini ya Sh 500,000, nyota wa Simba, Bernard Morrison amehusika moja kwa moja kwenye kusababisha adhabu ya wachezaji wengine watatu kwa mwezi Oktoba waliokutana na rugu la kutoa kiasi hicho cha fedha na kufungiwa michezo mitatu ya ligi. Adhabu hiyo iliyotolewa na Kamati ya Uendeshaji wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TBLB) inamfanya Morrison ahusike kwenye jumla ya Sh 2m kati ya shilingi milioni 6,500,000 zilizokusanywa kutokana na makosa mbalimbali Morrison alikutana na balaa hilo baada ya kumpiga ngumi nyota wa Ruvu Shooting, Juma Nyosso kwenye mchezo wa ligi uliochezwa Uwanja wa Uhuru, wakati Simba ikifungwa bao 1-0, Oktoba 26. Pia Nyosso naye amelimwa faini ya Sh 500,000 kwa kosa la kumkanyanga mguuni Morrison pamoja na kufungiwa mechi tatu za ligi. Nyota mwingine ni Shaban Msala ambaye naye alimpiga teke Morrison kwenye mchezo huo na kupigwa faini ya Sh 500,000 pamoja na kufungiwa mechi tatu na alionyeshwa kadi nyekundu. Kiraka wa Tanzania Prisons, Salum Kimeny

Si kweli Mzungu ana Akili Kuliko mtu Mweusi

Image
Hivi kwanini watu weusi mnajidharau sana, hivi leo hii ukizaa mtoto wako na ukaanza kumfundisha mzungu ni bora kuliko wewe unamtengenezea future gani, wenda ungempa ujasiri angeweza kuitawala dunia na kuwa prove wrong wazungu, nimesoma comments nyingi kwenye uzi mmoja umeandikwa "je mzungu ana akili kuliko mtu mweusi?" Majibu ya watu wengi yamenisikitisha sana jinsi Waafrika tunavojidharau, kuna kazi kubwa sana ya kubadilisha mitazamo ya waafrika especially watanzania otherwise tutaendelea kutawaliwa, just imagine mzungu anasoma comment zako na unaandika comment za kujishusha thamani tena kwa madaha na kufurahi. Nahisi hawa ndiyo wakikutana na wazungu wanachekacheka badala ya kuconcetrate kwe conversation na mwisho wa siku wana sign contract ambazo hawazielewi kisa tu kumuona mzungu kama Mungu, na wakati ni watu wa kawaida tu. Na yawezekana kabisa ukawa unamzidi hadi intelligence bila ww kujua kama unamzidi kutokana na imani potofu. Binafsi nimegundua watu wengi wanaju

Siri ya Herufi ya Mwanzo ya Jina Lako

Image
HERUFI A Mwenye jina linaloanziana na herufi A ni mtu anayependa mambo makubwa, anajiamini na mwenye uwezo wa kutimiza malengo yake. Ni mtu mwenye tahadhari, mchangamfu na mpenda matukio. Anapenda Kuheshimiwa, anapenda Mamlaka, na ana kiburi, na hasira. HERUFI B wenye jina linaloanziana na herufi B ni mtu, mkarimu, muaminifu, na hupenda kazi. Ni Jasiri, shujaa na mkatili katika vita au pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake. HERUFI C Mwenye jina linaloanziana na herufi C ni mtu wa kukubadilika badilika, mshindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda. Ni watu wa wabunifu na wanaopenda mawasiliano. HERUFI D Mwenye jina linaloanziana na herufi D ni mtu anayependa usawa, Biashara. Ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi. Ni jeuri na wenye msimamo. HERUFI E Mwenye jina linaloanzia na herufi E ni mtu mwenye roho nzuri ,yenye mapenzi na huruma. mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Kinyume na hivyo atakuwa ni mtu asiotegemewa na kigeu

Mambo Muhimu 11 Unayopaswa Kumwambia Mpenzi Wako Kila Siku

Image
Kutengeneza uhusiano wenye nguvu ni moja ya mambo yenye changamoto kubwa. Japo hakuna maelekezo maalum, kuna mambo machache na rahisi ambayo unaweza kumwambia mpenzi wako yakaujenga zaidi. Weka desturi ya kusema mambo haya kwa mpenzi wako na muda mfupi tu mtakuwa couple itakayowapa wivu marafiki zetu. 1. Nakupenda Nakupenda ni kitu rahisi na cha wazi cha kumwambia mpenzi wako. Hakikisha tu kuwa unamaanisha. Jaribu kulisema neno hilo pindi mpenzi wako anapokuchekesha au pale anapofanya kitu kinachokukumbusha kwanini mko pamoja. 2.Nilikuwa nakuwaza Ni muhimu kumjulisha mpenzi wako kuwa unamuwaza hata kama hamko sehemu moja. Ukiona kitu kizuri au cha kuchekesha katika siku yako ambacho kinakufanya umkumbuke, mjulishe. 3. Siku yako ilikuaje? Muulize masuala ambayo mpenzi wako anakutana nayo katika shughuli za kila siku. Muulize kuhusu huyo mfanyakazi mwenzie anayemkera au kazi kubwa waliyokuwa wakifanya. Kumpa nafasi mpenzi wako kushare sehemu zingine za maisha yake kutasaidia

Mmarekani Mweusi wa Kwanza Kuwekewa uso Bandia

Image
Robert Chelsea ndiye Mmarekani mweusi wa kwanza duniani na mtu wa 40 kufanyiwa pandikizi la uso mzima julai mwaka huu, tangu mapandikizi ya aina hiyo kuanza mwaka 2015. Upandikizaji huo uliofanyiaka kwa saa 16 chini ya uangalizi wa timu ya  madaktari 45 ndio ulioonekana kuwa na mafanikio makubwa zaidi duniani. Kabla ya hapo alifanyiwa upasuaji kwa zaidi ya mara 30 bila mafanikio, lakini upasuaji wa 31  ambao alifanyiwa hospitali ya Boston’s and Women’s. umeweza kuwa wa matumaini na mafanikio makubwa kwani hadi sasa anaendelea vizuri. Chelsea alipata ajali mwaka 2013 baada ya gari lake kugongana na gari jingine ambalo dereva wake alikuwa amelewa pombe na kusababisha apoteze uso wake pamoja na sehemu nyingine nyingi za mwili wake. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3gYAgj5 via IFTTT

Barbara Afunguka Kuhusu Chama Baada ya Kumaliza Mkataba

Image
“Wanasimba wanapaswa kutulia, Chama haendi kokote. Kwa sasa bado ni mali ya Simba kwa vile mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu, lakini pia mwenyewe ameonyesha nia ya kuendelea kusalia kikosini na tumeshaanza mazungumzo ya kusaini mkataba mpya” “Mazungumzo hayo na wakala wake yapo pazuri na wakati wowote tutamalizana naye na kusalia katika timu yetu ambayo imepania kufanya vizuri katika michuano ya ndani na ile ya kimataifa” -:Maneno Ya  Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba sc Barbara Gonzalez from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2HQf5UR via IFTTT

Marapa Matajiri Zaidi Duniani Hawa Hapa

Image
KWA hapa Bongo, inaaminika mastaa wa wanaoimba, ndio matajiri zaidi kuliko wale wa kufokafoka (Hip Hop). Tofauti na mtazamo huo wa Kibongo, huko Marekani wapo mastaa ambao ni wa hip Hop lakini wana utajiri wa kutisha. Twende tukaitazame Top Five ya mastaa wa Marekani lakini pia duniani kote wanaotajwa na mitandao mbalimbali kuwa ndio wanaoongoza kwa utajiri: KANYE WEST Kanye West ni moja kati ya marapa bora wa muda wote. Mafanikio yake makubwa ya kwenye mitindo na fasheni ndiyo yamechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza utajiri wake. Kingine kilichochangia mapato yake, Kanye ameachia sokoni albamu 9 ambazo karibia zote zimeuza kwa kiwango cha juu (multi-platinum). Kanye ameuza karibu nakala milioni 100 duniani kote. Miongozi mwa dili zinazomuingizia mapato ni pamoja na ubalozi ikiwemo wa kampuni ya Adidas. Kwa ujumla, Kanye ana utajiri wa Dola Bilioni 3.2 (Shilingi Trilioni 7. 4) . JAY Z Mkali huyu kutoka pande za Brooklyn ambaye ni mjasiriamali ndiye rapa wa kw

Mwanamke Amwambia Mumewe Anatamani Wanaume Wengine

Image
 ANITA CASSIDY (40) mwanamke ambaye amekuwa katika ndoa kwa miaka ipatayo kumi, alimwambia mumewe aitwaye Marc (46) kwamba anaona maisha na ndoa ya mume na mke yamemchosha na alitaka kuwa na wenza wengine wa kufanya nao mapenzi. Katika mazungumzo ya wawili hao ambao ni raia wa Italia, mumewe alikubali kwamba wote wawili kila mmoja angekuwa na wapenzi wengine.    Lakini, je, katika ndoa moja panawezekana kuwa na watu zaidi ya wawili? Anita Cassidy (katikati) akiwa na mpenzi wake wa kiume Andrea (kushoto) na mumewe Marc (kulia) wakichangia penzi la watu watatu.  “Mwaka mmoja uliopita niliweka kila kitu bayana kwenye mtandao wa Facebook kwa picha niliyokuwa na mume wangu na watoto wetu wawili.  Marafiki zangu wakaanza kuniuliza kwamba mwanamme mwingine aliyekuwa katika picha alikuwa nani.  Niliwaambia alikuwa Andrea – mpenzi wangu wa kiume. … Watatu hao wakiwa pamoja kando ya bahari wakipunga upepo. “Nafahamu wengi watashangaa kwani walijua Marc ndiye mume wangu halisi.   Laki

Makosa Makubwa Wanayoyafanya Wanawake linapokuja Swala la Kupenda..!

Image
Je wewe ni mtu wa kupenda ghafla, yaani mwanaume anapokutamkia kwamba anakupenda huwa unamuamini kwa kiasi gani, unakuwa ni mwepesi wa kumuamini na kujitoa kwa ajili yake au unakuwa na kujivuta vuta ili kujiridhisha kabla ya kuingia katika uhusiano? Hebu fikiri kabla ya kuamua, jipe muda kwani hakuna jambo lililo jema kama subira linapokuja swala la kupenda. Subira itakuepusha kupoteza muda wako katika mahusiano ambayo hayana mashiko wakati dhamira yako ilikuwa ni kumpata mwenzi mwenye sifa muafaka, pale utakapoingia mahali ambapo sipo. Kwa kawaida kutoka katika uhusiano huo kuna gharama kubwa na kunaweza kukusababishia matatizo mengi yakiwemo ya kiafya. Hapa chini nitajaribu kueleza makosa kadhaa ambayo wanayafanya wanawake linapokuja swal la kupenda: 1.Kumbadili mtu awe vile utakavyo: Usije ukajidanganya kwamba unaweza kumbadilisha mtu mzima na akili zake. Kama umepata mwanaume ambaye kwa mtazamo wako unamuona ana sifa muafaka lakini anatabia ambazo huzipendi kwa mfano ulevi au

Mmea Mkubwa Unaokula Nyama....

Image
Mmea mkubwa unaokula nyama unajulikana kama 'Montane Pitche' wa aina ya 'Nepenthes Rajah' na una urefu wa sentimita 41 Ulionekana Kisiwa cha Borneo mwaka 2011. Mmea huu ambao una kama dibwi (Pitch) unatumia majimaji yake kuwavutia na kuwanasa wadudu warukao kama buibui wakati mwingine hukamata hata mijusi na vyura Mimea mingine inayokula nyama ni Flypaper Plant, Cobra Lily na Venus Flytrap Katika yote hiyo uliovunja rekodi ya kula viumbe wakubwa ni huo Nepenthes Rajah ambao umeingia kwenye Rekodi ya Dunia from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3btNhQl via IFTTT

Marekani yafanya majaribio ya kombora lenye uwezo wa kubeba nyuklia na kusafirisha angani

Image
Mamlaka ya Jeshi la Anga nchini Marekani imetangaza kufanya majaribio hapo jana ya kombora aina ya "Minuteman III" linaloweza kubeba nyuklia na kusafirisha angani. Kwa mujibu wa maelezo yalitolewa na mamlaka hiyo, iliarifiwa kuwa kombora hilo lililojaribiwa kwenye kambi ya jeshi la anga ya Vandenberg iliyoko California, halikubebeshwa nyuklia wakati wa majaribio. Maelezo zaidi yalibainisha uwezo na nguvu kubwa ya kijeshi iliyokuwa nayo Marekani, na kuthibitisha kuwa tishio kwa kipindi hiki cha karne ya 21. Chombo cha kilichotumiwa kubeba kombora hilo hewani, kilisafiri kwa masafa ya maili 4,200 angani hadi kufikia kisiwa cha Kwajelin. Mamlaka ya jeshi pia iliweza kuchapisha picha za urushaji wa kombora hilo katika mtandao wa kijamii. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3ecZo5L via IFTTT

Inasikitisha Sana Lakini Inatia Moto....Soma Kisa Hichi

Image
Kijana mmoja wa miaka 24 alikuwa akisafiri yeye na wazazi wake, toka Ifakara kwenda Mlimba kwa usafiri wa treni. Sasa alipojaribu  kuangalia katika dirisha la treni, Mara akahamaki....... _ Akasema: "Baba angalia, miti inarudi nyuma, tena inarudi Kwa kasi sana.....🌲🌲!!!" Baba yake akamwangalia Kwa furaha kisha akatabasamu!  Pembeni kidogo palikuwa na wapenzi wawili waliokaa karibu nao, Wakamuangalia yule kijana wa miaka 24  nakuanza kusemezana wenyewe: "Baby umemsikia uyo kaka, mbona ni mkubwa sana ila anatabia zakijinga ivyo?!" "Nashangaa ata Mimi, lazima atakuwa anamatatizo ya akili, ndio maana hata Baba yake ahangaiki naye.!" Waliongea wenyewe. Ghafla yule kijana akashangaa tena.......!!! Akasema..... "Baba, angalia mawingu nayo yanakimbizana na sisi pia ...☁!!" Basi wale wapenzi wawili wakashindwa kuvumilia, wakaamua kumwambia yule mzee.  "Kwanini usimpeleke kijana wako Kwa daktari mzuri, pengine anamatati

Watanzania Milioni 14.8 Hawajapiga Kura Uchaguzi Mkuu 2020

Image
Matokeo ya urais yaliyotangazwa usiku Ijumaa Oktoba 30, 2020 na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yanaonyesha kuwa Watanzania milioni 14.8 sawa na asilimia 49.8 hawakujitokeza kupiga kura.   Idadi hiyo ya watu milioni 14.8 ni kati ya Watanzania milioni 29.8 waliojiandikisha kupiga kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 28, 2020.   Uwiano huo wa watu ambao hawakujitokeza ni mkubwa ikilinganishwa na asilimia 33 ya ambao hawakujitokeza katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Hata hivyo uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 waliojiandikisha kupiga kura walikuwa milioni 25.5.   NEC imemtangaza mgombea wa CCM, John Magufuli kuwa mshindi wa kiti cha urais baada ya kupata kura 12,516,252 sawa na asilimia 84.4 kati ya kura halali 14,830,195. Kwa mujibu wa matokeo hayo mgombea wa Chadema, Tundu Lissu amekuwa mshindi wa pili baada ya kupata kura 1,933,271 na kufuatiwa na mgombea kupitia ACT- Wazalendo, Bernard Membe aliyepata kura 81,129 na Leopord Mahona wa NRA kura 80,787.   Matokeo

Waangalizi wa Afrika Mashariki: Uchaguzi wa Tanzania umefanyika kwa kufuata utaratibu zote

Image
Rais wa zamani Silvestre Ntibantunganya ambaye ndiye Mwenyekiti wa ujumbe wa waangalizi kutoka Afrika Mashariki, amesema kuwa uchaguzi mkuu Tanzania ulifanyika kwa kufuata taratibu. Ujumbe wa waangalizi wa EAC ulikuwa na wajumbe 89 waliosambazwa maeneo mbalimbali , kufuatilia mchakato wa upigaji kura lakini pia utangazaji wa matokeao ya kura hizo. Bwana Ntabitunganya amesema walikutana na wadau wa uchaguzi ikiwemo tume na vyama vya kisiasa na waangalizi wengine. Ujumbe huo umesema umeshuhudia hali ya usalama kaika maeneo mbalimbali, watu wakifanya kampeni kwa uhuru kabla ya kuanza shughuli ya upigaji kura. Katika siku ya kupiga kura vituo vilifunguliwa kwa muda muafaka, masuala ya ya kiufundi yalifanywa kwa weledi. Waangalizi walishuhudia wapiga kura wakitekeleza wajibu wao bila kutishwa wala hofu. ”Baadhi ya vyama vya siasa au wagombea wamelalamikia kuhusu namna uchaguzi ulivyoandaliwa na namna matokeo yalivyotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi.Ujumbe wa waangalizi

Twaha Kiduku Ambomoa Mthailand kwa TKO, Amtaka Mwakinyo – Video

Image
Bondia Mtanzania, Twaha Kiduku amemtwanga bondia Sorimongkhon kutoka Thailand kwa TKO raundi ya saba from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3mQNwd5 via IFTTT

Mimba ya Aunt Hatarini!

Image
KITENDO cha staa wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel kunaswa ‘club’ ya starehe ya usiku akigida pombe za hatari ilihali ni mjamzito wa kujifungua muda wowote, kimeibua gumzo kubwa juu ya hatari ya kuchoropoka kwa mimba hiyo. Wikiendi iliyopita, Aunt alinaswa akitandika bia kama zote kwenye Club ya The Base iliyopo Makumbusho jijini Dar, usiku wa manane ambapo kulikuwa na shoo ya msanii wa Bongo Fleva anayedaiwa ndiye mwenye ujauzito huo aitwaye Salmin Said ‘Kusah’. Bila kujali ukubwa wa kitumbo chake, pia Aunt ndiye alikuwa MC wa shoo hiyo kabla ya kuweka kambi kwenye moja ya kona na kuanza kutandika ulabu aina ya bia ambazo zina sifa ya kuwa na kilevi kikubwa. Hata hivyo, baada ya ishu hiyo kuibua mjadala mkali, gazeti hili liliibeba hadi kwa daktari ambaye amefunguka kinagaubaga juu ya madhara ya unywaji wa pombe kwa mwanamke mjamzito kama Aunt. Dk Geofrey Charles ‘Dk Chale’ ni daktari bingwa wa magonjwa ya akina mama na watoto ambaye anasema kuwa, mama kutumia kilevi wakati wa

BREAKING: NEC yamtangaza Dr Magufuli kuwa mshindi kiti cha urais

Image
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemtangaza aliyekuwa mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM Dkt.John Pombe Magufuli kuwa mshindi wa nafasi hiyo baada ya kupata kura 12,516,252 akifuatiwa na Tundu Lissu wa CHADEMA mwenye kura 1,933,271 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3mDwxKT via IFTTT

Sio Kila EX Wako Anayeomba Mrudiane Anamaanisha! Wengine Huomba Kurudi Ili Wakutesti Tu

Image
Sio Kila EX Wako Anayeomba Mrudiane Anamaanisha! Wengine Huomba Kurudi Ili Wakutesti Tu Jinsi Ulivyo Mbulula,Jinsi Usivyo Na Msimamo Na Jinsi Ulivyo CHEAP Na Huna Misimamo Wala Future. Jitu Mmeachana Miezi 6,Leo Linakutesti Lirudishe Majeshi,Na Wewe Ulivyo Kiazi,Upo-Upo Tu,Ina Maana Miezi Yote Hii Ulikuwa Umeganda Unasubiria Rehema Zake Ama?? Kurudia Matapishi Ya EX Ukitegemea Amebadilika Ni Sawa Na Kupika Sufuria La Makande Kwa Mshumaa,Utaambulia Masizi Tu.. Kipi Kipya Kakiona Kwako Hadi Arudi??Nini Kilimshinda Huko Nyuma Ambacho Leo Anakiweza Anataka Kurudi??Akafie Mbele Huko. KUWA NA MSIMAMO,Ukisema Its Over Umaanishe,Sio Unakuwa Na Hisia Zinapepea Tu Kama Bendera Ya Katibu Kata Wa Kishumundu... Mtu Kama Hajielewi Achana Nae,Siku Akijirudisha Mwambie Kwanza Akapimwe Minyoo Ya Kinyarwanda. Umekazana Kuwaambia Marafiki Zako 'Siku Hizi Hakuna Mapenzi Ya Dhati Watu Wote Majanga Tu',Nani Amekwambia Hayapo?? Yapo Sana Ila Wewe Unatumia Mbinu Tofauti.. Huwezi Kusoma Degr

Mpenzi Halindwi na Alarm wala Hawekewi Tracker, Analindwa na Mahaba na Care Unazompa

Image
Mpenzi halindwi na Alarm wala hawekewi Tracker,analindwa na Mahaba na Care unazompa. Ukimpa Mahaba Niue Nife Nayo basi atakuwa wako daima dumu,atajilinda mwenyewe na hataenda nje maana hakuna kipya kule ambacho kwako hapati, Ukimpa Mahaba ya Kibaba cha Mafuta shallow,basi atatafuta mtu wa kujazilizia kwenye gepu! Usipoteze muda kukaba nyendo za mpenzi wako kama beki wa Yanga, Invest kumridhisha Mpenzi wako kwenye kila idara ya Penzi lenu ili Mahaba yenu yabaki salama lasivyo jiandae kuwa mlinzi wa KK Security Night Shift bila gwanda! from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3heh00Z via IFTTT

Wapiga kura zaidi ya milioni 80 wamemaliza kupiga kura Marekani

Image
Zaidi ya wamarekani millioni 80 wamepiga kura ya mapema kabla ya uchaguzi wa rais wa tarehe 3 Novemba, kulingana na takwim zilizokusanywa jana na taasisi ya chuo kikuu cha Florida inayofwatilia uchaguzi wa marekani. Kiwango hicho kimevunja rekodi, ni zaidi ya asilimia 58 ya watu waliojitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi wa mwaka 2016, na inaonyesha umuhimu wa uchaguzi wa mwaka huu ambapo kinyanganyiro ni kati ya rais Donald Trump, mrepublican na mdemocrat makamo rais wa zamani Joe Biden. Idadi kubwa ya watu walipiga kura kwa njia ya posta au kwenye vituo vya kura, kutokana na hofu kwamba virusi vya corona vinaweza kusambaa siku ya uchaguzi. Wataalamu wanatabiri kuwa idadi ya wapiga kura mwaka huu itazidi millioni 138 waliopiga kura kwenye uchaguzi wa rais wa 2016, alioshinda Donald Trump. Kura millioni 47 pekee ndizo zilipigwa kabla ya siku ya uchaguzi mwaka 2016. Imetayarishwa na Patrick Nduwimana, VOA, Washington DC from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2TztTtk vi

Lil Wayne azua tafrani mtandaoni

Image
Rapa kutoka nchini Marekani Lil Wayne amezua tafrani mtandaoni baada ya kutangaza kuwa amekutana na rais wa Marekani Donald Trump huku akiafikiana na mpango wa Rais huyo unao fahamika Kama "Platinum Plan" unao lenga kuwasaidia wamarekani wenye asili ya Afrika. “Nilikuwa na kikao na Trump ukiachana na yale aliyofanya mpaka sasa mpango wake “The plutnum plan” unakwenda kuipa jamii umiliki halali. Amesikiliza tulichotaka kusema na ametuhakikishia atatekeleza.” Mapokeo ya wafuasi wake hasa nchini Marekani yalikua ni ya kumzomea na kumcheka huku wengine wakimtengenezea vibonzo vya kumdhihaki. Pia wapo ambao walihisi ukurasa wake wa twitter umedukuliwa. Hata hivyo baadhi ya wafuasi wa Trump wamefurahishwa huku wakiamini ni fursa hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi wa Marekani. Rapa wengine wenye asili ya Afrika walio wahi kumuunga mkono trump ni Kanye West ambaye baadae alibadili mawazo na kuamua kusimama kama mgombea urais nchini Marekani. Mwingin

James Mbatia Aangushwa Ubunge Vunjo, Kimei wa CCM Ashinda

Image
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Vunjo amemtangaza Dkt. Charles Kimei wa Chama cha Mapinduzi-CCM  kuwa mshindi wa Ubunge katika Jimbo hilo baada ya kupata kura 40,170 – Grace Kiwelu wa CHADEMA amepata kura 8,675, James Mbatia wa NCCR amepata kura 4, 949 na Agustino  Mrema kutoka TLP kura 606 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3ebYA18 via IFTTT

Malaria Yamuendesha Carlos Carlinhos

Image
KIUNGO Mshambuliaji wa Yanga, Carlos Carlinhos, amejikuta katika wakati mgumu kutokana na kuteswa na Ugonjwa wa Malaria uliosababisha asiwemo katika sehemu ya kikosi cha timu hiyo kinachojiandaa na mechi za Ligi Kuu Bara huko Kanda ya Ziwa.   Awali Carlinhos alikuwa nje ya uwanja kutokana na kupata majeraha ya kisigino katika mazoezi yaliyofanyika katika kambi yao iliyopo AVIC Town, Kigamboni jijini Dar.   Siku chache kabla ya kwenda Mwanza kucheza na KMC, kiungo huyo aliugua ghafl a Malaria ambayo inamtesa hadi sasa. Akizungumza na Spoti Xtra, Daktari wa Yanga, Shecky Mngazija, amesema, Carlinhos bado hayupo fi ti kutokana na kuendelea na matibabu ya malaria kulikomlazimu kutokuwa sehemu ya kikosi.   “Wachezaji wengine wapo fi ti isipokuwa Mapinduzi Balama ambaye anaendelea na matibabu pamoja na Carlinhos ambaye yeye bado anaendelea na dozi ya malaria na yupo Dar akiendelea kujiuguza. “Kurudi kwake ku-nategemea na jinsi atakap-opata nafuu kwa mapen-zi y

Mafuta ya Kuvuta Pesa za Majini au Jini wa Utajiri

Image
Kwa wanayoyafahamu wanajua faida zake. Haya ni mafuta yanayotumiwa sana katika kuvuta pesa za majini ama kuita Jini wa Utajiri.  Ni Mafuta yenye kazi nyingi za Umuhimu na kimaendeleo,  shida ni kwamba hayapatikani Kiurahisi sana kwa ajili ya Umuhimu wake na Mafanikio yake. MATUMIZI YAKE : Tafuta Kitambaa Cheupe mita moja kitandike katikati ya sakafu ndani ya Chumba, kisha nyunyuzia Poda(maalum) katika Kitambaa chote. Chukua noti ya pesa ya nchi yoyote iweke katikati ya kitambaa hicho Dondosha tone moja la mafuta ya Shantar Washa mshumaa warangi ya Njano, Mwekundu na Mweusi mbele ya kitambaa hicho. Nuwia ukitakacho huku ukiwa umefumba macho takribani dakika 7 kisha fumbua macho yako toka Nje Dakika 15 tu. Kisha Rudi ndani Uone Maajabu yake... Kwa mahaitaji ya mafuta haya piga ☎️ 0746 753 790 CHIEF SULTAN MAKATA ...ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA   Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na

Kimbunga Molave chaua watu 31

Image
Mchakato wa uokozi unaendelea nchini Vietnam hii leo, baada ya maporomoko ya ardhi yaliyosababishwa na KimbungaMolave. Death toll in Vietnam from Typhoon Molave reaches 13 Mamia ya wanajeshi wenye vifaa vizito wametumwa katika maeneo ya ndani ya jimbo la Quang Nam kulikotokea maporomoko ya ardhi na ambako watu 19 wameuawa na wengine 48 hawajulikani walipo. Aidha miili ya wavuvi 12 imeopolewa baharini hii leo na wengine 14 hawajulikani walipo baada ya boti yao kuzama. Kimbunga hicho kinatajwa kuwa ni kibaya kuwahi kushuhudiwa kwa miongo kadhaa. 21 killed, dozens missing after Typhoon Molave lashes Vietnam | Vietnam |  Al Jazeera Na kimepiga katikati mwa nchi, ambako tayari kumekuwa kukinyesha mvua kali kwa wiki kadhaa zilizosababisha vifo vya watu wapatao 160. Zaidi ya watu milioni moja wameathiriwa na dhoruba hizo kali ziliozopiga kwa wiki kadhaa. Mashirika ya kutoa misaada nayo yameelemewa kutokana na idadi kubwa ya walioathirika. from UDAKU SPECIAL BLOG h

Hawa ndio Wabunge 28 wa CCM waliopita bila kupingwa Uchaguzi Mkuu 2020

Image
Mpaka hivi sasa Chama tawala CCM kimeshinda zaidi ya viti 188 vya Ubunge Tanzania nzima huku Upinzani wakishinda viti viwili tu yaani CHADEMA kiti kimoja Nkasi na CUF kiti kimoja Mtwara vijijini. Wafuatao ni Wabunge 28 wa Chama cha Mapinduzi CCM ambao walipita bila kupingwa au kwa Lugha nyingine, walikua ni Wagombea pekee katika Majimbo yao baada ya Wagombea wa Vyama vingine kushindwa kusimamisha Wagombea au kutotimiza vigezo vya Kugombea . HAWA NDIO WABUNGE 28 WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM , AMBAO WALIPITA BILA KUPINGWA . 1. Job Ndugai (Kongwa) 2. Cosato Chumi (Mafinga Mjini) 3. Isaack Kamwele (Katavi). 4. Nape Nnauye (Mtama) 5. Kassim Majaliwab (Ruangwa) 6. Pauline Gekul (Babati) 7. Daniel Sillo (Babati Vijijini,) 8. Jummane Sagini (Butiama) 9. Ahmed Shabiby (Gairo,) 10. Prof Palamagamba Kabudi (Kilosa) 11. Godwin Kunambi (Mlimba) 12. Innocent Kalogeris (Morogoro Kusini) 13. @babutale (Morogoro Kusini Mashariki). 14. Jonas Van Zeland (Mvomero) 15. Ale