Posts

Showing posts from November, 2022

Mhadhiri SAUT adaiwa kuuawa kwa kunyongwa

Image
Mwanza. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) Mwanza, Hamida Mussa maarufu 'Mama Mwakitosi' (64) anadaiwa kuuawa kwa kunyongwa na mtandio shingoni na mfanyakazi wa ndani ambaye alitokomea kusikojulikana baada ya tukio hilo. Mwili wa Hamida ulikutwa jana Jumanne Novemba 29, 2022 nyumbani kwake Mtaa wa Buzuruga Mashariki wilayani Ilemela mkoani Mwanza ukiwa umelala sakafuni kifudifudi ukiwa na mtandio shingoni mwake. Taarifa zinaeleza mhadhiri huyo wa Idara ya Uhandisi Kitivo cha ICT, SAUT alikuwa anaishi na msaidizi wa kazi ambaye baada ya tukio hilo kutokea ametokomea kusikojulikana. Akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumatano Novemba 30, 2022, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Buzuruga Mashariki, Martin Muya amethibitisha kutokea tukio hilo. Amesema pamoja na kujua Hamida alikuwa anaishi na mfanyakazi wa ndani ila hakuwahi kumtambua kwa sura japo anajua alikuwa na umri kati ya miaka 15 hadi 18 kwani hakuwahi kumtambulisha ofisini kwake. Mtoto wa

Mume Wangu Aliniacha Siku Tisa Baada ya Kupoteza Kazi Yangu

Image
Tuiishi pamoja na mume wangu Kibet katika kaunti ya Lamu ambapo nilifanya kazi ya udaktari katika hospitali moja ya kibinafsi katika kaunti ile. Mume wangu naye alifanya kazi ya uhandisi katika wizara ya ujenzi kwenye kauti ile.  Maisha yetu yalikuwa ya kutamaniwa kwani hakuna wakati ata moja tuligombana na mume wangu kwani hali ilikiwa shwari kabisa. Wakati mwingine nilimpaa mume wangu hata pesa za matumizi nay eye pia alinipa pesa kidogo kutoka kwa mshahara wake.  Hali ilikuwa ni imara zaidi kwani upendo ulikuwa umetufikisha pazuri. Siku moja nilienda afisini na nikakumbana na barua Fulani kwenye meza yangu. Niliifungua na kuisoma na hapo nikakumbana na ujumbe kwamba hospitali ile ilikuwa kasha nionyesha mlango na nilitakiwa nifuate masharti yale kabla siku haijhakamilika.  Niliporejea nyumbani na kumwarifu mume wangu yaliyonikumba alinipa moyo kwani alisema kuwa angewajibika kama kichwa cha ndoa ile kuhakikisha kwamba mahitaji ya nyumba ile yametimizwa. Nilipiga moyo kond

Hatimaye Talaka ya Kanye West na Kim Kardashian Yakamilika

Image
Hatimaye mastaa Kanye West (YE) na Kim Kardashian mchakato wao wa Talaka umekamilika Jumatatu hii, wameripotiwa na TMZ kufikia maridhiano ya Talaka huku Kanye West atatakiwa kumlipa Kim Kardashian kiasi cha $200k ambazo ni zaidi ya TZS Milioni 466 kila mwezi kwa ajili ya matunzo ya watoto wao. Lingine lilioangaziwa kwenye maridhiano hayo ni haki sawa katika malezi ya watoto wao. Tovuti ya TMZ imeeleza. Na iwapo mmoja wao atashindwa kushiriki vyema, mwingine anapewa nafasi ya kufanya uamuzi kwa chaguo la msingi. Itakumbukwa, Mwanamama Kim Kardashian mwezi Februari, mwaka jana alifungua shauri mahakamani la kudai Talaka baada ya kuwa kwenye ndoa kwa takribani miaka 7 na Kanye West. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/iWybTa1 via IFTTT

Zifahamu Faida 6 za Juisi ya Tangawizi, Halafu Nenda Kajaribu Uone Ajabu Yake..!!!

Image
Tangawizi ni kati ya viungo mahili vinavyochochea ladha nzuri katika vyakula vya aina mbalimbali na hivyo kuwavutia walaji kula chakula husika. Tangawizi pia inapowekwa kwenye vyakula vigumu kama nyama huifanya ilainike na hivyo kuweza kuiva kwa haraka zaidi. Leo nataka kukueleza msomaji wangu kuhusu hizi faida nyingine za kutumia juisi ya tangawizi kama ifuatavyo:- 1. Hutumika kama kituliza maumivu. 2. Husaidia kuboresha mmeng'enyo wa chakula tumboni 3. Huthibiti shinikizo la damu 4. Huboresha afya ya kinywa 5. Hukinga matatizo ya ngozi hasa chunusi 6. Husaidia kukuza nywele (kulinda afya ya nywele) from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/J8m3pRC via IFTTT

Senegal yafuzu 16 bora Kombe la Dunia

Image
YAMETIMIA!! Baada ya takribani miaka 20, hatimaye Senegal imefuzu hatua ya 16 bora ya mashindano ya Kombe la Dunia, kufuatiwa ushindi wa mabao 2-1 waliopata dhidi ya Ecuador. Imekuwa timu ya kwanza Afrika kutinga hatua hiyo. Mwaka 2002 Senegal ikiwa chini ya kocha mfaransa, Bruno Metsu walipita hatua hiyo hadi robo fainali na kupoteza mchezo bao 1-0 dhidi ya Uturuki, bao lililofungwa na Ilhan Mansiz mturuki mzaliwa wa Ujerumani. Mabao ya Senegal yamefungwa na Ismail Sarr kwa penalty na Koulid Koulibaly kwa akiunganisha mpira wa kona. Wakati bao la Ecuador likifungwa na Moise Caicedo kiungo kutoka Brighton Hove Albion ya England. Kuanzia Kombe la Dunia la mwaka 2006 mpaka 2014, Senegal haikupata nafasi ya kufuzu, 2018 ilifuzu na kuishia hatua ya makundi, ambapo katika kundi H, Senegal ilipangwa na Colombia, Poland na Japan, na Senegal kumaliza akiwa na pointi nne. Baada ya Senegal sasa, timu nne zimebaki kutoka Afrika, Morocco ambao wako kundi F wakiwa na pointi nne, sawa na

Mafuta ya Kuvuta Pesa za Majini au Jini wa Utajiri (Money Drawing Oil)

Image
Haya ni mafuta Mapya kutoka Kampuni inayoshughulika kutengeneza Vifaa mbalimbali vya Nguvu za Asili na Za Kimiujiza vyenye uwezo mkubwa wa kumsaidia Binadamu kufikia malengo yake yawe Hasi ama Chanya Wanaitwa Lord's Divine wanapatikana Katika Maktaba Kuu kwenye baadhi ya Nchi 14 Duniani Kwa Uchache sana Africa Kazi ya mafuta haya ni Nyingi ila Nitaanisha baadhi kwa Uchache.. 👉kuwa na uwezo wa kuvuta Pesa kwa wingi na hivyo kuweza kukupatia Utajiri kwa haraka 👉Kukufanya uwe MVUTO na BAHATI kubwa sana ktk kila jambo lako utakalofanya linafanikiwa 👉Kukufanya uwe na mvuto na heshima kubwa katika Kazi, Kwa Wachungaji, Wanasiasa, Wasanii, au Mtu yoyote Maarufu Kwa wanayoyafahamu wanajua faida zake. Haya ni mafuta yanayotumiwa sana katika kuvuta pesa za majini ama kuita Jini wa Utajiri. Ni mafuta yenye kazi nyingi za umuhimu na kimaendeleo, shida ni kwamba hayapatikani kiurahisi sana kwa ajili ya umuhimu wake na mafanikio yake.. MATUMIZI YAKE KWA WALE WANAOTAKA PESA ZA

CCM yachukizwa na udhalilishaji wa Heche

Image
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimelaani vikali kitendo cha Mfuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuonekana katika video katika Mitandao ya kijamii akimnyima fursa ya kufanya kazi mwananchi moja kwa sababu alikuwa amevaa fulana ya CCM na kusema tukio hilo ni kuvuja katiba ya nchi. Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM, Shaka Hamdu Shaka ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma ambapo amesema tukio hilo licha ya kuvunja katiba linarudisha nyuma juhudi za Rais Samia na viongozi wa vyama vya siasa katika kuleta maridhiano na kusema vyombo vya Dola vinapaswa kumshughulikia. Kauli ya Shaka imekuja baada ya ‘video clip’ baada ya kusambaa kwenye mitandao ya kijamii iliyomuhusisha mwanachama wa Chadema Mwalimu Chacha Heche kaka wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema John Heche dhidi ya mzee mmoja mkoani Mara. Video hiyo inamuonyesha Chacha akimlazimisha mzee huyo kuvua fulana yenye nembo ya CCM aliyoivaa kwa mapenzi yake binafsi. “Kijana huyo ameonekana akimtweza na kumlazimisha kuvu

Dharau Yaiponza Yanga...Yachezea Kichapo Kutoka Timu ya IHEFU..Rekodi Yavunjwa

Image
HATIMAE klabu ya Ihefu imevunja rekodi ya Yanga ya kutokufungwa katika mechi ya 50 kwenye mechi za ligi kuu Tanzania bara baada ya kufungwa kwa mabao 2-1, mchezo ambao ulipigwa Mbarali mkoani Mbeya. Yanga Sc ilianza kupata bao kupitia kwa Yannick Bangala kabla ya Never Tigere kusawazisha kwa kupiga mpira wa adhabu uliomshinda kipa wa Yanga na kutinga nyavuni moja kwa moja. Bao la pili Ihefu Fc limefungwa na Kissu na kufanya matokeo kuwa 2-1. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/Y2XdcRo via IFTTT

Zitto Kabwe: Hatujafunga ndoa na CCM

Image
KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ameeleza kuwa chama hicho ni tofauti na Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja na vyama vingine vya siasa vya upinzani. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea). Mwanasiasa huyo ametoa kauli hiyo katika mahojiano yake na Kituo cha Televisheni cha ITV, yaliyorushwa mubashara jana Jumatatu kuhusu madai ya ACT-Wazalendo kuwa mshirika wa CCM. “Kwenye siasa kuna mitizamo tofauti na ni wajibu wa chama kuhakikisha kinasimamia yale malengo ambayo kinataka kuyafikia, sisi ni tofauti na CCM, Chadema, CUF na vyama vingine vyote. Tunafanya siasa zetu kwa mujibu wa maamuzi yetu. Kama kuna mtu ambaye anatutazama kwa hivi unavyosema ni mtizamo wake na sisi ni wajibu wetu kumuonyesha hapana sisi tuko tofauti,” alisema Zitto. Katika hatua nyingine, Zitto alisema ACT-Wazalendo hakina mgogoro na chama chochote cha siasa nchini, na kwamba wanachama na viongozi wake wanajibu hoja za wanachama wa chama kingine, pale ambapo shabaha na malengo ya

Familia Wafunguka Kuhusu Picha Aliyopost Profesor Jay "Ilipostiwa Kwa Bahati Mbaya"

Image
Saa chache zilizopita kwenye ukurasa wa Instagram wa Mkongwe wa Bongofleva Profesa Jay @professorjaytz upande wa Insta story kulipostiwa picha yake akionekana na Mke wake wakihojiwa kwenye red carpet, kitendo kilichoamsha furaha ya Mashabiki wengi kuona Mkali huyo ameimarika kiafya na wengine kuamini ameanza kuhudhuria matukio mbalimbali. Msemaji wa Familia ya Haule @blackchatta aliyepatikana kuzungumzia hilo ameiambia AyoTV kuwa ni kweli post hiyo (ipo kwenye swipe) ilichapishwa na Profesa Jay mwenyewe lakini kwa bahati mbaya kwa sababu anatumia simu zake zote kwa sasa na huwa anaingia kwenye mitandao kuperuzi japo hajawahi kupost chochote toka January 23 2022. “Anatumia simu zake zote sasa hivi na anaingia kwenye social media, anasoma anaona matukio yote lakini mambo ya kupost haya kwa sasa bado, anaruhusiwa kutumia simu kuangalia vitu, ile ni picha ya siku nyingi alipost kwa bahati mbaya iliteleza kwenye mikono yake lakini yuko fresh tunamshukuru Mungu” “Watu wasiwe na hofu

Rammy Galis " Filamu inawaka MOTO, Rosa Ree Rapa Bora wa Kike Bongo"

Image
Rammy Galis " Filamu inawaka MOTO, Rosa Ree Rapa Bora wa Kike Bongo" VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/8qK2j47 via IFTTT

Kocha wa Timu ya Taifa ya Cameroon Rigobert Song Afafanua Kumtimua Andre Onana

Image
  Kocha wa Timu ya Taifa ya Cameroon Rigobert Song amekanusha taarifa za kumtimua Mlinda Lango Andre Onana, kwa sababu za kukataa kutii amri ya kutimiza jukumu la ushirikiana na kupinga mpango wa Rais wa Shirikisho la Soka nchini humo Samuel Eto’o kufanya mazoezi ya timu hiyo. Onana aliondolewa kwenye kikosi cha Cameroon saa chache kabla ya mchezo pili wa Kundi G dhidi ya Serbia uliomalizika kwa timu hizo kufungana 3-3. ong amesema amelazimika kumuondoa Mlinda Lango huyo wa klabu ya Inter Milan ya Italia, kwa sababu za kinidhamu ambazo zilipelekea washindwe kuelewana, hasa alipokataa kucheza mchezo dhidi ya Serbia jana Jumatatu (Novemba 28). “Ni mchezaji muhimu, lakini tuko kwenye michuano migumu, hivyo ni bora akatupisha ili tumalize hili kwanza,” “Ninajua ninachopaswa kufanya, na hiyo ni kuhakikisha kuwa timu kwanza halafu mchezaji baadae.” alisema kocha huyo baada ya mchezo dhidi ya Serbia Alipoulizwa na Shirika la Habari la AFP iwapo angeanza mchezo wa jana dhidi ya Se

Kocha wa zamani wa Simba SC, Didier Gomez ala Shavu Uarabuni

Image
Kocha wa zamani wa Simba SC, Didier Gomez da Rosa ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa klabu ya Al Ain FC inayoshiriki ligi kuu ya Falme za Kiarabu (UAE)Unapenda Simulizi? Kuna NDOA YANGU na kuna INATOSHA, Zitakukosha sanaa. Bofya Hapa kufurahia sehemu ya 1 bure ndani ya group la telegram. Mbali na Simba SC Da Rosa amewahi kuvitumikia vilabu vya Rayon Sports, Horoya AC FC na timu ya Taifa Mauritania. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/zRP35uJ via IFTTT

Hatari Mikopo ‘Kausha Damu’

Image
Ongezeko la taasisi zinazotoa mikopo ‘chap chap’ yenye riba kubwa na kugeuka machungu kwa wakopaji, imeelezwa kuwa chanzo cha msongo wa mawazo kwa mdaiwa, kufariki kwa shinikizo la damu au kukimbia kusikojulikana. Dar es Salaam. Ongezeko la taasisi zinazotoa mikopo ‘chap chap’ yenye riba kubwa na kugeuka machungu kwa wakopaji, imeelezwa kuwa chanzo cha msongo wa mawazo kwa mdaiwa, kufariki kwa shinikizo la damu au kukimbia kusikojulikana. Mikopo hiyo iliyopachikwa jina la ‘kausha damu’ kutokana na maumivu wanayopata wakopaji wakati wa kurejesha fedha, baadhi ya taasisi zimekuwa zikitoa masharti magumu, ikiwamo kutaifisha mali zikiwemo nyumba, magari na samani za ndani endapo mhusika atashindwa kulipa kwa wakati. Uchunguzi uliofanywa na Mwanachi umebaini kuwa wanaoshindwa kurejesha mikopo kwa wakati, wamejikuta mali walizoweka kama dhamana zikitaifishwa na kuuzwa katika mazingira yasiyotoa fursa kuweza kupinga uuzwaji wa mali zao hizo. ALSO READ Mtoto anapenda soka? Njia sahi

Baada ya Ndoa na Mama Steve Kufeli, Barnaba Kumuoa Huyu Mrembo

Image
Mopao barnabaclassic yupo mbioni kuuaga ukapera baada ya jana kumvisha pete mchumba wake @rayatheboss ikiwa ni kiashirio cha kuelekea katika ndoa. Shughuli hiyo inatajwa kufanyika mwishoni mwa wikiendi na kuhudhuriwa na wasanii wenzake. Hongera kwa @barnabaclassic tunawatakia safari njema ya kuelekea kwenye ndoa yeye na mchumba wake. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/R0w8jTM via IFTTT

Serikali Yabariki Ndoa ya Bandari, TICTS Kuvunjwa

Image
Dar es Salaam. Siku moja baada ya taarifa kuhusu nia ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kutohuisha mkataba na kampuni binafsi ya kimataifa ya kuhudumia makontena Tanzani (TICTS), Serikali imebariki uamuzi huo. Hatua ya TPA kumalizana na TICTS iliyohudumu bandarini kwa miaka 22 imetokana na kufikia ukomo wa mkataba wa miaka mitano waliosaini Julai, 2017, pia ni kutoafikiana katika majadiliano ya kuongeza muda wa huduma. Mkataba kati ya TPA na TICTS ulikoma Septemba 30, mwaka huu na kabla ya hatua hiyo, vilifanyika vikao kadhaa kuuhuisha bila mafanikio. Jana, Mwananchi liliripoti kuhusu uamuzi huo wa manejimenti ya TPA, lililoupata kutoka katika chanzo cha ndani cha kuaminika kuwa TPA na TICTS walioanza kufanya kazi pamoja mwaka 2000, wanakwenda kuachana. Kulingana na chanzo hicho, uamuzi wa TPA kuachana na TICTS unatokana na wawili hao kushindwa kuafikiana katika vigezo na masharti kama vilivyoainishwa katika ibara ndogo ya 2.2.1 ya mkataba. “Kwa kuwa mkataba hautahuishw

Watu Maarufu Duniani Waliofariki Kabla ya Kufikisha Miaka 50

Image
1.Aaliyah, miaka 22. Alikuwa ni mwimbaji wa muziki, alifariki kwa ajali ya ndege. 2.Malcom X, miaka 39. Alikuwa ni mwanaharakati wa haki za biinadamu. Aliuwawa. 3.Martin Luther King, miaka 39. Alikuwa pia mwanaharakati. Aliuwawa na watu wasiojulikana 4.Whitney Houston, miaka 49. Mwanamuziki. Alifariki kwa madawa. 5.2pac, miaka 25. ALikuwa mwanamuziki, Aliuwawa kwa kupigwa risasi. 6.Bob Marley, miaka 36. Mwanamuziki maarufu wa Reggae. Alifariki kwa Kansa. 7.Bruce Lee, miaka 32. Actor wa filamu za mapigano, sababu za kifo zake bdo ni utata mpaka leo. 8.John F. Kennedy, miaka 46. Rais wa Marekani. Aliuwawa kwa risasi. 9.Princess Diana, miaka 36. Alikuwa ni mke wa mtoto wa Malkia wa Uingereza. Alifariki kwa ajali ya gari, wengi wanashuku ajali hiyo ilipangwa. 10.Ernest Che Guevara, miaka 39. Mwanamapinduzi wa Argentina. Aliuwawa na CIA. 11. B.I.G, Miaka 23. Taja wengine. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/trUXyiQ via IFTTT

Picha 8 za Mabehewa Mapya ya Daraja la Tatu Reli ya SGR

Image
Picha 8 za mnato za mabehewa mapya ya daraja la 3 kwa ajili ya kutumika katika reli ya SGR. Mabehewa haya sio ya kizamani kama baadhi ya watu wanavyojaribu kupotosha. Waliopo nchi ambazo tayari zinatumia njia hii ya usafiri wanaujua ukweli. Na haya ni mabehewa ya daraja la 3, fikiria ya daraja la pili (Business class) yatakuwaje na ya daraja la kwanza (First class) yatakuwaje? from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/8QgzFbS via IFTTT

Kocha Juma Mgunda Atoa Msimamo wake Simba

Image
KOCHA Mkuu wa Simba, Juma Mgunda ametoa msimamo mkali wa kusimama na wachezaji wake kwa matokeo yoyote yale huku akiwaonya mashabiki kuacha kuwashambulia badala yake wawape sapoti. Simba ilirejea Dar es Salaam juzi Jumatano usiku ikitokea jijini Mbeya ilipotoka sare ya bao 1-1 na Mbeya City na jana iliondoka kwenda Moshi kwaajili ya mechi dhidi ya Polisi Tanzania. Baada ya mchezo na Mbeya City mashabiki mitandao na kwenye eneo la klabu ya Simba Kariakoo Jijini Dar es Salaam, walionyeshwa kutoridhishwa na kiwango lakini Mgunda amewataka kutulia na kuacha kuwatupia lawama wachezaji kwani bado ligi ni ndefu na hawapaswi kubabaika. “Hakuna kocha yeyote asiyependa kuona timu yake ikishinda, hivyo mashabiki wanapaswa kulitambua hilo na kuacha kuanza kuwatoa wachezaji kwenye mstari,” alisema Mgunda ambaye muda wowote kuanzia sasa anaweza kuwasili bosi wake, raia wa Ureno. “Ni kweli mabeki wangu waliruhusu bao jepesi kwa sababu kwa kaliba na uwezo wao sio watu wa kufanya vile lakini n

Polisi Watatu Wauawa Kwenye Msafara, Kiongozi Atekwa

Image
Kundi la watu wenye silaha wamewaua Polisi watatu waliokuwa wakisindikiza msafara na kisha kumteka Meneja wa kampuni ya mafuta ya IGPES Group of Oil and Gas, Seni Awosika aliyekuwa na kiasi kikubwa cha pesa na kisha kutokomea kusikojulikana. Maafisa wa upelelezi wa Kamandi ya Polisi ya Rivers wamesema wameanza msako wa kuwatafuta watu hao ambao walifanya tukio hilo kwenye barabara ya juu ya Rumuokoro iliyopo eneo la Port Harcourt, ambao ni mji mkuu wa jimbo hilo majira ya saa tatu usiku wa Novemba 24, 2022. Eneo la tukio juu ya Daraja la Rumuokoro lililopo jimbo la River Port Harcourt, Nigeria. Picha ya Within Nigeria. Mashuhuda wa tukio hilo wamesema, watu hao wenye silaha waliufuata msafara huo ambapo walifanikiwa kuunasua na kuwapiga risasi Polisi hao kabla ya kumteka nyara Meneja huyo na walikuwa wamevalia sare za kijeshi. Kwa mujibu wa Msemaji wa Polisi wa eneo hilo, Grace Iringe-Koko amesema, “Polisi watatu waliokuwa wakimsindikiza mtendaji huyo waliuawa huku mwanamume

Serikali yatangaza Rasmi vita na Al-Shabaab

Image
  Vita kamili dhidi ya wanamgambo wa Al-Shabaab imetangazwa rasmi, na kuidhinishwa kwa juhudi za kupambana na ugaidi ambazo licha ya ya mafanikio yake ya kijeshi ya siku za mwanzo huenda ikawa vigumu na vikadumu kwa muda mrefu kutokana na uhalisia. Vita hiyo imetangazwa na Serikali ya Somalia, kulikabili kundi hilo lenye mafungamano na al-Qaeda lililofukuzwa kwenye miji mikubwa muongo mmoja uliopita lakini bado linashikilia maeneo mengi ya mashambani ambako makundi ya wanamgambo yameungana kwa ajili ya mapambano. Aidha, inaarifiwa kuwa koo mbili za nchini humo ambazo zimechoshwa na utawala wa Al-Shabaab, zilianzisha uasi dhidi ya kundi hilo uliosambaa haraka katika mikoa ya Hirshabelle na Galmudug na mwezi Septemba ulipata usaidizi wa makomandoo waliopewa mafunzo na Marekani. Kwa upande wake, Mtafiti kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Migogoro (ICG0, Omar Mahmood amesema nia ya Serikali ni kuendeleza kasi ya sasa na kuondoa uasi kama huo katika maeneo yote yanayoshikiliwa na Al-Sha

Yanga Wabaya Sana, Waichapa Mbeya City ikiandika rekodi mpya

Image
MATOKEO ya leo Yanga ikiichapa Mbeya City mabao 2-0 inafikisha mechi 49 bila kupoteza mchezo wowote kwenye ligi pia inazidi kujiimarisha kukaa kileleni, ikifikisha pointi 32, katika mechi 12 iliyozocheza. Ukiachana na kichapo cha leo ilichopata Mbeya City, mara ya mwisho kuifunga Yanga ilikuwa Novemba 2, 2016 Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya. Wakati matokeo ya misimu miwili iliyopita, Mbeya City 1-1 Yanga (Juni 25,2021/ 22),Yanga 0-0 Mbeya City (Februari 5,2021/22),Yanga 1-0 Mbeya City (Septemba 13, 2020/21),Mbeya City 1-1 Yanga (Februari 13, 2020/21). Hata hivyo matokeo hayo kwa Mbeya City, yataifanya kushuka nafasi za chini, kwani katika mechi 13 ilizocheza imeshinda nne, sare sita, imefungwa mitatu inamiliki mabao 18 imetikiswa mara 16 na pointi 18. Mayele amefunga mabao saba katika michezo mitatu ya ligi akianza na hat-trick dhidi ya Singida BS, mawili dhidi ya Dodoma Jijj na leo dhidi ya Mbeya City. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/lHaQrUI via IFTTT

Baraka the Prince Akamatwa na Polisi Uzinduzi wa Album ya Rosa Ree

Image
Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva @barakahtheprince_ adaiwa kukamatwa na Polisi Usiku wa Kuamkia leo katika Uzinduzi wa Album mpya ya @rosa_ree kwa kosa la Kumpiga Mwandishi wa Habari kutoka kituo cha Habari cha #EATV. Inasemekana @barakahtheprince_ amelazwa Kituo cha Polisi kwa kosa la kumshambulia Mwanahabari kutoka #EATV baada ya Kumuomba kufanya nae Mahojiano ndio #Baraka akamvuta Pembeni na Kumshambulia. . . from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/DXhqjf3 via IFTTT

Nyangasa: Igeni Mfano wa Meridianbet

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Fatma Nyangasa ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kuiga mfano wa Kampuni ya Meridianbet Tanzania, Ameyasema hayo wakati akiongoza zoezi la Usafi katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo kwa kushirikiana na Kampuni ya Meridianbet Tanzania kama vile maeneo ya kituo cha daladala cha Kivukoni Feri. Katika zoezi hilo la kuweka mazingira safi Mkuu wa Wilaya Mh Fatma Nyangasa alitoa shukrani zake kwa kampuni ya Meridianbet kwa kutoa msaada wa vifaa vya kufanyia Usafi pamoja na maji ya kunywa pia na kwa kujitoa kwao kushiriki kikamilifu kwenye zoezi hilo. "Kampuni ya Meridianbet imekuwa mstari wa mbele kwenye kushiriki shughuli za kijamii, kama hili la leo, wameungana nasi kufanya usafi na kutupa msaada wa vifaa vya usafi, hivyo nawashukuru kwa kujitoa kwenu hiki mlichokifanya ni kikubwa sana, naomba muendelee kama hivi na kampuni zingine zipate kuiga mfano wenu"- Fatma Nyangasa. Nae Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Meridian

DOZEN ajibu namna anaweza kurudi CLOUDS Fm au kwenda radio nyingine, aleta Tamasha hili kubwa

Image
  DOZEN ajibu namna anaweza kurudi CLOUDS Fm au kwenda radio nyingine, aleta Tamasha hili kubwa VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/ueAZ2gV via IFTTT

Makamu wa Rais wa Malawi Saulos Chilima Akamatwa kwa Tuhuma za Rushwa

Image
Makamu wa Rais wa Malawi Saulos Chilima amekamatwa kwa tuhuma za rushwa. Ofisi ya kupambana na rushwa nchini humo inasema kuwa kati ya Machi na Oktoba mwaka jana, alipokea zaidi ya dola 280,000 na vitu vingine kama malipo baada ya kusaidia kampuni mbili kupewa kandarasi za serikali. Taarifa kutoka kwa ofisi hiyo inasema Bw Chilima atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka kadhaa yakiwemo makosa matatu ya ufisadi. Hapo awali alihojiwa na wachunguzi kutoka ofisi hiyo lakini hajazungumzia madai hayo. Chilima aligombea kiti cha urais mwaka 2019 lakini akashika nafasi ya tatu katika uchaguzi uliokuwa na ushindani mkali. Baadaye aliungana na Rais wa sasa Lazarus Chakwera katika kama mgombea mwenza. Lakini uhusiano wa hivi karibunu kati ya Makamu wa Rais na Bw Chakwera umezorota kutokana na shutuma za ufisadi na upendeleo serikalini. Bw.Chilima amewahi kufanya kampeni katika jukwaa la kupinga ufisadi akiahidi kumaliza miongo kadhaa ya ulafi serikalini na kumaliza umaskini katika

Kilimo Kilichogeuka Mahangaiko

Image
  Muda wote ule unapotaja kilimo,hutowacha kutaja uti wa mgongo wa nchi yeyote ile kwa njia moja ama nyingine.Katika umri wangu wa makamo ilinibidi kujitosa katika ulimwengu huo wa kilimo kwani hakukuwa na jinsi nyingine ambayo ningeweza kuweka chochote mezani kwani wavyele wangu ndiyo iliyokuwa shughuli yao ya kila uchao. Nilianza kwa kufanya vibarua kwa matajiri waliokuwa wakifanya kilimo kama biashara na wala sio kupata lishe ya kila siku.Mwenyezi Mungu alinineemesha kwa kunipa nguvu ya kuchapa kazi na hata kuweza kuhifadhi kiwango cha shillingi mia mbili kwa siku kwa muda wa miaka takribani minne. Baada ya kupata kwamba nilikuwa na fedha ambazo zingeniwezesha kukodi kipande kidogo cha ardhi,Pamoja na bidii nilizokuwa nazo niliamua kukodi robo ya hekari na  kuanzisha ukulima wa kibinafsi kutafta mtaji wa kuniwezesha kukua na kuinua kilimo changu. Nilijaaliwa neema kubwa kwani kila nilipowekelea mkono kulima mmea, kwa kweli ulinawiri sana na hata kutoa mazao mengi sana ukili

WACHEZAJI wa Uhispania waruhusiwa kufanya mapenzi usiku mmoja kabla ya mechi

Image
Kikosi cha kwanza cha Uhispania Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uhispania Luis Enrique ameweka wazi kwamba anawaruhusu wachezaji wake kushiriki mapenzi na wapenzi wao kabla ya mechi. “Sijali wachezaji wakifanya tendo la ndoa usiku wa kuamkia mechi lakini ninaweka mstari kwenye karamu,” alisema kocha wa Uhispania Luis Enrique katika mtiririko wake wa hivi punde kwa mashabiki kutoka Qatar. Meneja huyo wa Uhispania pia alikiri angependa kuhamia Uingereza katika siku zake za kucheza akiongeza uvumi kwamba ataishia kufundisha klabu moja katika Ligi ya Premia siku moja. Kocha huyo asiye wa kawaida alikuwa akizungumza kwenye Twitch, akitimiza ahadi yake kwa mashabiki ya kuendelea kutiririka kwa muda wote Uhispania ikiwa kwenye Kombe la Dunia. Alipoulizwa pia ikiwa wachezaji wanapaswa kuambiwa wasifanye mapenzi kabla ya michezo alisema: “Ni ujinga (kuipiga marufuku). Ni kitu ninachokiona cha kawaida kabisa. Ikiwa uko kwenye tafrija usiku mmoja kabla ya mechi basi ni wazi hilo si jam

Rais wa nchi aliyeua raia wake kwa kosa la kuvaa miwani,alijitangaza yeye ni Mungu,alisafiri na pesa

Image
  Rais wa nchi aliyeua raia wake kwa kosa la kuvaa miwani,alijitangaza yeye ni Mungu,alisafiri na pesa   from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/WFcDSsU via IFTTT

Wachezaji wa Saudi Arabia Kuzawadiwa Magari aina ya Rolls Royce Phantom

Image
Wachezaji wa Saudi Arabia watazawadiwa gari aina ya Rolls Royce Phantom baada ya kuifunga Argentina kwenye Kombe la Dunia la Fifa 2022. Rolls Royce itazawadiwa kwa kila mchezaji mmoja mmoja na Mfalme wa nchi hiyo, na hii si mara ya kwanza kwa zawadi za gharama kubwa kuzawadiwa wachezaji wa nchi hiyo. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/ofRweMy via IFTTT

Mwigizaji Ray Kigosi Afunguka Kauli ya Kubebwa na Kanumba "Mimi Ndio Nilimtoa Kanumba"

Image
Muigizaji mkongwe kutokea kwenye kiwanda cha Bongo Movie, @raythegreatest hii leo Nov 25 ameongea na waandishi wa habari kwaajili ya kutangaza dili lake na kampuni ya ulinzi nchini #k4ssecurity kama balozi mpya wa kampuni hiyo. Mbali na Jambo hilo ambalo ndilo lililokuwa lengo hasa la press conference yake, Ray amedokeza ujio wa kazi zake mpya na kubwa, lakini pia ametaja sababu kubwa ya kudumaa kwa tasnia ya uigizaji nchini, ni kutokuzalishwa kwa waigizaji wapya wenye vipaji vya kufikia levo za kina Wema Sepetu. Ray amedai anarudi kwenye sanaa kuiboresha upya kwa kuleta vipaji vipya kwasababu ana karama hiyo ya kuibua talents kali, Pia amedai anashangaa watu wakisema alikuwa anabebwa na Kanumba, wakati haipo hivyo sababu Kanumba alitokea kwenye mikono ya Ray, waigizaji kama Uwoya, Wolper, Johari na wengine kibao wakubwa kama Thea walitokea kwenye mikono yake. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/Pm6hwCJ via IFTTT

RC Makalla: Hakuna tena mgawo wa maji Dar

Image
Pwani. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla ametangaza kuanzia sasa hakuna mgao wa maji ndani ya mkoa huo na kuitaka Mamlaka ya Majisafi na Mazingira Dar es Salaam (Dawasa) kuelekeza nguvu kuimarisha miundombinu na miradi mikubwa ikiwemo Mabwepande. Oktoba 24, 2022, RC Makalla alitangaza kuwepo kwa mgawo huo baada ya kutembelea vyanzo vya kuzalisha maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu na kujionea upungufu katika uzalishaji wa maji kulikosababishwa na ukame. Leo Ijumaa, Novemba 25, 2022, mara baada ya kutembelea chanzo cha maji Ruvu Chini, RC Makalla ametangaza kuisha hali hiyo baada ya kuona ujazo wake umerejea kwenye hali yake ya kawaida kufuatia mvua zilizonyesha siku za hivi karibuni. "Maji yamerejea katika ujazo wake wa kawaida na zaidi na kama mnavyojua vyanzo vya maji vinavyotegemewa ni Ruvu Juu inayochangia lita196 milioni na hapa Ruvu Chini inachangia maji lita 270 milioni na kufanya jumla kuwa lita za ujazo 466 milioni na sasa tuna maji ya kutosha," a

Pinga Ukatili wa Kijinsia kwa Wanawake na Meridianbet!

Image
Hauko peke yako – Meridianbet ina ujumbe mzito kwa wanawake wahanga wa matukio ya ukatili wa kijinsia. Popote ulipo, mtaani, maeneo ya kazi, maeneo binafsi… Wanawake wanne kati ya watano hupitia ukatili mitaani. Mmoja kati ya wanawake watatu huathiriwa na ukatili wa kijinsia na kimwili. Mmoja kati ya wanawake watano amepitia unyanyasaji mtandaoni, lakini pia aslimia 50 ya wanawake wamepitia unyanyasaji wa kimwilini maeneo yao ya kazi!  Ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake hujidhihirisha kwa njia na aina mbalimbali, sio ya kimwili tu. Pinga Ukatili dhidi ya Wanawake! Meridianbet  wamekuwa wamekuwa wakifanya kazi kwa miaka mingi kupaza sauti kuhusu swala hili ili kupinga ukatili dhidi ya wanawake na kuongeza ufahamu wa umuhimu wa kupambana na ukatili bila kusubiri tatizo linapotokea. Kampuni imedhihirisha azma yake ya kushiriki kikamilifu kama kampuni inayowajibika kwa jamii kwa zaidi ya miongo miwili, ikikazia umuhimu wa usawa wa kijinsia, uwezeshaji wa kiuchumi wa wanaw

Neymar anaongoza kwa kuchezewa madhambi World Cup Qatar

Image
  Neymar ndiyo mchezaji aliyechezewa rafu nyingi zaidi mpaka sasa kwenye michuano ya Kombe la Dunia Qatar 2022. Staa huyo wa Brazil amechezewa madhambi zaidi ya mara tisa (9) dhidi ya Serbia. Dakika ya 79 Neymar ametolewa kwenye mchezo huo kufuatia majeraha ya ankle. Kwa mujibu wa daktari wa timu, Rodrigo Lasmar Wabrazil watalazimika kusubiria saa 24 hadi 48 kufahamu hatma ya majeraha ya nyota huyo. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/ACTJ359 via IFTTT