Posts

Showing posts from January, 2022

Steve Nyerere: Nguvu ya Wema Sepetu imeonekana, Aristote Ameshajifunza, Tumsamehe

Image
  Steve Nyerere: Nguvu ya Wema Sepetu imeonekana, Aristote ameshajifunza, tumsamehe VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/NjekXYP51 via IFTTT

Nape Nnauye "Rais Samia Kaniagiza na Nimefanya Mabadiliko"

Image
  Waziri wa Habari Nape Nnauye, amesema kuwa wamefanya mabadiliko na kwamba chaneli za bure kama ITV na East Africa TV zimeanza kuonekana tena kwenye king'amuzi cha DStv baada ya hapo awali kuondolewa. Taarifa hiyo ameitoa hii leo Januari 31, 2022, na kusema kuwa mabadiliko yaliyofanyika ni ya kanuni namba 18 ya mwaka 2018, na kusema kuwa Rais Samia amemwagiza kufanya mabadiliko na kanuni zimeshasainiwa na tayari zimeanza kutumika ili kuongeza wigo kwa Watanzania kupata habari. "Tumefanya mabadiliko, chaneli ambazo hazilipiwi zianze kuonekana kwenye king'amuzi cha DStv, mtakumbuka baadhi ya chaneli ziliondolewa kwenye king'amuzi chenu na hili jambo limekuwa kilio kikubwa kwa wananchi, Rais kaniagiza na nimefanya mabadili," amesema Waziri Nape from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/JBzfT297G via IFTTT

Ujio mpya wa meli ya MV Mbeya II

Image
  .Serikali imetumia zaidi ya Billioni tisa kufanya matengenezo ya meli ya Mv Mbeya II iliyopata hitilafu iliyotokea wakati wa dhoruba mwezi Machi mwaka 2021 ilipokuwa ikitia nanga katika bandari ya Matema. Akizindua safari za meli meli hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera, leo januari 31, 2022 amesema kukamilika kwa matengenezo ya meli hiyo imekuwa ni ukombozi kwa wakazi wa Wilaya na Mkoa kwani waliokosa huduma hiyo kwa muda mrefu. Akizungumza Katika uzinduzi wa meli hiyo ambayo tayari imepewa cheti na taasisi ya udhibiti wa vyombo vya maji TASAC,Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Bandari ya Itunge Abdalah Mohamed, amesema tayari matengenezo yamekamilika kwa asilimia mia moja na utoaji huduma utaendelea. Meli ya Mv Mbeya II leo imeanza kufanya safari zake mkoa wa Ruvuma na Njombe baada ya kupata hitilafu miezi tisa iliyopita ikiwa na abiria zaidi ya mia moja na hamsini. Amewataka wafanyakazi wa meli hiyo kuwa waaminifu na wazalendo katika kutoa taarifa pale wanapobaini kuna uhari

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo February 1, Polisi Kujinyonga Mahabusu Kaa la Moto

Image
  Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo February 1, Polisi Kujinyonga Mahabusu Kaa la Moto from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/SueIsyxDg via IFTTT

Makubwa... ‘Ambulance’ Yatumika Kusafirisha Nanasi

Image
  Maafisa wa polisi nchini Uganda wamemkamata dereva mmoja ambaye alipigwa picha akishusha mananasi kutoka kwenye gari ya wagonjwa ya Hospitali ya Kebisoni Center IV wilayani Rukungiri. Kulingana na msemaji wa polisi wa eneo la Kigezi, Elly Maate, dereva huyo kwa jina Matayo Barekye ni mkazi kutoka mjini Kebisoni, wilaya ya Rukungiri. Daily Monitor inaripoti kuwa Barekye alinaswa kwenye picha mnamo Januari 27, 2022, katika soko la Nyamunuka akishusha mananasi kutoka kwa ambulensi yenye usajili wa nambari ya UG 3797M. Barekye anadaiwa kusafirisha mananasi baada ya kumfikisha nyumbani mgonjwa ambaye aliyefanyiwa upasuaji na akiwa safarini kurejea, aliamua kubeba mzigo wa mananasi na wakati alipokuwa akiushusha alipigwa picha na kuzua ghadhabu mtandaoni. “Polisi walimkamata mshukiwa huyo baada ya picha za kupakuliwa kwa mananasi kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii na mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi yametajwa dhidi yake,” alisema Maate. Msemaji wa polisi pia aliongezea

Daraja la Tanzanite Kuanza Kutumika KESHO, Kupita ni Bure Hakuna Malipo

Image
  Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa Daraja la Tanzanite linalopita juu ya Bahari ya Hindi limekamilika na litaanza kutumiwa na wakazi wa Dar es Salaam kuanzia Februari Mosi 2022. Daraja hilo linatarajiwa kupunguza msongamano wa magari katika Barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Barack Obama wakati wa kuingia na kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam. Daraja la zamani la Selander linapitisha zaidi ya magari 45,000 kwa siku, hivyo kukamilika daraja jipya kutasaidia sana kupunguza idadi ya magari yanayopita katika daraja la zamani la Selander na hivyo kuepusha kabisa msongamano wa foleni. Mbali na foleni, pia litasaidia kukuza sekta ya utalii kwa sababu eneo hilo liko pembeni ya fukwe ya bahari ambapo watu wengi watakuwa wakienda kujivinjari. Daraja hilo lina urefu wa kilometa 1.03, lina njia nne za magari na njia mbili za watembea kwa miguu na limejengwa pamoja na barabara unganishi zenye jumla ya kilometa 5.2. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/Pf

Zuchu, Mbosso Kundi Moja Burna Boy na Davido

Image
  Wanamuziki mahiri wa muziki wa Bongo fleva kutoka WCB Zuhura Othman maarufu Zuchu pamoja na Mbwana Yusuf Kilungi maarufu Mbosso wamefanikiwa kuingia kwenye orodha ya vijana 100 wenye ushawishi mkubwa zaidi barani Afrika kwa mwaka 2021. Hii ni kwa mujibu wa Evance Media kutoka nchini Ghana ambao wamechapisha taarifa hiyo kwenye mtandao wakiambatanisha na orodha ndefu yenye jumla ya vijana 100 kutoka mataifa mbali mbali  barani Afrika. Katika orodha hiyo wamo waigizaji, wachekeshaji, Wafanyabiashara, wabunifu wa mavazi, wanamitindo na wengine wengi. Wengine waliotajwa kwenye orodha hiyo ni pamoja na wasanii kutoka nchini Nigeria akiwamo Tems,  Burna Boy, Davido, Wizkid, Joe Boy pamoja na Facolistic kutoka Afrika kusini. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/A5P91imHt via IFTTT

Prof: Ndalichako: “Vijana Jiungeni Kwenye Vikundi Mpate Mikopo”

Image
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Mhe,Prof, Joyce Ndalichako amewataka vijana waliopata mafunzo ya ukuzaji ujuzi katika vyuo mbalimbali nchini kujiunga kwenye vikundi ili kunufaika na fursa za mikopo na vifaa kwa kujiendeleza kiuchumi. Ametoa wito huo jana (29 Januari, 2022) mkoani Kigoma  mara baada ya kutembelea maeneo mbalimbali ambapo vijana wa programu hiyo wanapata mafunzo kwa vitendo na kusisitiza kuwa lengo la  serikali ni kuona elimu hiyo inawanufaisha vijana. ‘Mheshimiwa Rais tayari ametupatia fedha kwa ajili ya kununua vifaa ambavyo tutavigawa kwa baadhi yenu, na kwenye ofisi ya Waziri mkuu kuna mfuko kwa ajili ya kuwawezesha vijana hivyo jiungeni kwenye vikundi ili mnufaike na fursa hizo niwambie tu mama hawezi kuwaacha  vijana wake” ,alisema Waziri Ndalichako. Aidha amesema progamu hiyo ni endelevu ambapo awamu ya kwanza imepangwa kugharimu shilingi za Kitanzania bilioni tisa kwa matarajio ya kuwan

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo January 31 "Pole Pole Aibua Mjadala Kula Urefu Kwa Kamba"

Image
  Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo January 31 from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/PpwQTcMXS ya Leo.html via IFTTT

Utafiti...Unaambiwa Wanaume Wanaochepuka Sana Wako Kwenye Kundi la Binadamu Wenye Akili Ndogo "Lower IQs"

Image
#UNAAMBIWA: Mwanaume ambaye humsaliti Mpenzi,Mchumba au Mke wake mara nyingi huenda akawa kwenye kundi la Watu wenye akili ndogo (Lower IQs) kwa mujibu wa Mwanasaikolijia Satoshi Kanazawa kutoka London School of Economics and Political Science. Mwanasaikolojia huyo anasema kadri Mwanaume anavyokuwa smart na mwenye akili kubwa ndivyo uwezekano wa yeye kuchepuka unavyokuwa mdogo "Mwanaume mwenye akili kubwa huwa ni ngumu kumsaliti Mwenza wake" from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/XkACSjJPM via IFTTT

Mtu Wangu Ndoa Inachangamoto zake Lakini Haziondoi Faida Kubwa Zitokanazo na Ndoa

Image
Anasema japokuwa Ndoa ina changamoto zake lakini haiondoi faida ambazo hutokana na Ndoa. Mdau ametoa wito kwa Vijana kuacha woga kwa kuwa wanaweza kuimudu Familia hata kwa kipato kidogo Ametaja faida za kuoa ikiwa ni pamoja na kuwa na matumizi bora ya Fedha. Anasema wasiooa wanaweza kutumia Fedha ovyo lakini ukiwa umeoa utafikiria Familia na kuwa na Nidhamu ya Fedha Kuoa kunakupa Usalama wa Afya yako kwa Magonjwa ya zinaa ambayo hutokana na Ngono Zembe. Pia, Mtu huwa na Afya nzuri kutokana na kupata mlo kamili tofauti na mtu akiishi peke yake. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/LsZV1EkvG via IFTTT

Serikali Kukabiliana na Uhalifu Mtandaoni..Matapeli na Wanaodhalilisha Watu Mitandaoni Kukiona

Image
Uhalifu wa kimtandao umetajwa kuwa suala kubwa katika siku za karibuni, na kadri Teknolojia inavyozidi kutanuka ndiyo matatizo ya uhalifu wa kimtandao yanavyoongezeka Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Masauni amesema lazima Jeshi liwe tayari kukabiliana na mabadiliko ya aina yoyote kudhibiti uhalifu huo ambao haukubaliki na hauwezi kuachwa uendelee Ameeleza, "Wapo watu wamekuwa wakitumia mitandao vibaya kudhalilisha watu. Wengine ni watu wazima wanaweza kuwa Wazazi wao. Wapo wanaotumia mitandao kufanya wizi na utapeli" from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/4n0EdlL3s via IFTTT

Hii ndiyo tofauti kati ya WCB Wasafi na Konde Music

Image
Kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa mashabiki wamekuwa wakizishindanisha lebo za WCB Wasafi na Konde Music Worldwide kutokana na ushindani wa wamiliki wake katika Bongofleva. WCB Wasafi iliyomtoa Harmonize kimuziki mwaka 2015 ni ya Diamond Platnumz. Baadaye Harmonize alianzisha Konde Music na hapo ndipo ushindani ukaibuka. Hata hivyo, ukweli ni kwamba lebo hizi zina tofauti kubwa katika baadhi ya mambo kama ifuatavyo; 1. Hadi sasa WCB imefanikiwa kutoa albamu tatu na Extended Playlist (EP) nne za wasanii wake sita, huku Konde Music ikitoa albamu moja na EP tatu za wasanii wake wanne.   2. Konde Music imefanikiwa kumsaini msanii kutoka nje ya Tanzania, Young Skales (Nigeria) lakini WCB haijafanya hivyo, licha ya kuwapo taarifa za kufungua tawi lao Kenya. 3. Kwa sasa WCB inasimamia wasanii sita ambao ni Diamond, Rayvanny, Queen Darleen, Lava Lava, Mbosso na Zuchu, huku Konde Music ikisimama na wasanii sita ambao ni Harmonize, Ibraah, Young Skales, Cheed, Killy na Angella. 4. T

UTEUZI: Raos Samia Afeua Vigogo Hawa Serikalini

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wafuatao: - 1. Amemteua Prof. Ulingeta Mbamba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE). Prof. Mbamba anachukua nafasi ya Dkt. Ng'wanza Kamata Soko aliyemaliza muda wake. Prof. Mbamba ni Profesa Mshiriki na Amidi wa Shule Kuu ya Biashara, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 2. Amemteua Bi. Zuhura Sinare Muro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL). Bi. Muro ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Ushauri Elekezi ya Kazi Service Limited na Mkufunzi wa muda katika Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute), Dar es Salaam. 3. Amemteua Prof. Leonard James Mselle kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya TEHAMA. Prof. Mselle ni Mhadhiri, Rasi Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu, Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Uteuzi huu unaanza tarehe 29 Januari, 2022. UTEUZI: Raos Samia Afeua Vigogo Hawa Serikalini fro

Breaking: Babu Juma Duni Haji ameshinda nafasi ya Uenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa

Image
Babu Juma Duni Haji ameshinda nafasi ya Uenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho unaoendelea usiku huu Dar es salaam, nafasi hiyo ilikuwa wazi baada ya kifo cha Maalim Seif Shariff Hamad. Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman ameshinda nafasi ya Umakamu Mwenyekiti Zanzibar wa Chama cha ACT Wazalendo Kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa ACT unaofanyika leo Dar es salaam, Msafiri Mtemewa ameshinda nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/l4boWXSsY via IFTTT

Wezi Wawili wa Simu Kenya Waingia Choo Cha Kike Baada ya Kuwaibia Polisi, Watandikwa Risasi Muguuni

Image
Wezi wawili wa Nairobi wanaugulia maumivu ya risasi za mguu Hospitalini mida hii baada ya kuwaibia simu Askari Polisi ambao hawakuwa wamevaa kipolisi kwa kuikwapua kwa kuwavizia wakiwa kwenye foleni ya magari eneo la Allsopps Nairobi Kenya jana. Wawili hao walipigwa risasi za mguu kila mmoja baada ya kuiba simu ya Inspekta Elizabeth Lumumba na kukaidi amri ya kusimama baada ya kumuibia Inspekta huyo ambaye alikuwa amebebwa na Koplo Hassan Mbwana kwenye gari binafsi. Imeelezwa baada ya kumuibia Inspekta huyo Wezi hao waliendelea kuwaibia Watu wengine waliokuwa wamekwama katika foleni ya magari na ndipo Inspekta Lumumba pamoja na Polisi mwingine aliyekuwa kwenye gari waliposhuka na kuwapiga risasi kwenye mguu baada ya kukaidi amri ya Polisi hao iliyowataka kusimama. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/PCkTuJm7Y via IFTTT

Kiwango cha Chama Kudaiwa Kuporomoka, Staa Simba Aanika Haya

Image
  LICHA ya baadhi ya mashabiki wa soka kuonyesha kutoridhishwa na kiwango cha kiungo, Cleotus Chama kwenye mchezo ambao Simba ilikubali kipigo cha bao 1-0 ugenini dhidi ya Kagera, kiungo fundi wa zamani wa Simba, Mtemi Ramadhan amekuwa tofauti na kiwango alichokionyesha Chama kwenye mchezo huo. Chama ambaye amerejea Simba msimu huu wa usajili wa dirisha dogo baada ya kuuzwa na timu hiyo mwaka 2021, jana alikuwa miongoni mwa nyota waliochapwa kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Kagera, Januari 26, 2022. Baada ya mchezo huo, baadhi ya mashabiki wa soka walionekana kutoridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na Chama na wengine wakiamini sio yule aliyekuwa Simba kabla ya kuuzwa nchini Morocco. Hata hivyo Mtemi amemkingia kifua nyota huyo raia wa Zambia akisisitiza kuwa kiwango cha Chama wa mechi Kagera ni kile kile alichoondoka nacho Simba mwaka jana. “Bado yuko vizuri, hajachuja na mashabiki tutarajie pasi nzuri za mwisho na mabao kutoka kwake. Juzi alipata nafasi moja, japo viwanja vya ny

Je ni Sahihi Kufanya Mapenzi na Mwenza Kama Majaribio Kabla ya Kuoana na Kufunga ndoa?

Image
Katika mahusiano kumekuwa na tabia ya kufanya mapenzi kama majaribio kabla ya kuoana na kufunga ndoa na hii inahusisha jinsia zote mbili. Mwanaume wakati mwingine anajaribu kujiridhisha kama mwanamke anaendana na vigezo vyake hali kadhalika kwa wanawake pia. Vijana wengi wamekuwa wakitumia kauli za dhihaka kama (Usiniuzie mbuzi kwenye gunia) Mara nyingi majaribio kama haya yamekuwa yakifanyika na wakati mwingine ndoa nyingi zimekuwa zikifungwa huku wanandoa walishapata watoto hapo awali. Wakati mwingine ndoa inawekewa vikwazo kwasababu za kujificha lakini ukweli ni kuwa wanandoa walishashindwana kwenye majaribio. Je wewe una maoni gani kuhusu tabia ya kufanya mapenzi kama majaribio kabla ya kuoana na kufunga ndoa? from UDAKU SPECIAL https://bit.ly/35mTbDZ via IFTTT

Maduka 16 ya Wafanyabiashara wa soko Mkoani Geita yameungua kwa moto

Image
Maduka 16 ya Wafanyabiashara wa soko la CCM kakubilo lililopo Wilaya ya Geita Mkoani Geita yameungua kwa moto na kuteketea kwa moto ambao hadi sasa bado chanzo chake hakijajulikana. Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ikiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Geita, Wilsoni Shimo imefika katika eneo hilo na kujionea hali halisi huku maduka 16 yakiwa yameungua na baadhi ya vitu kuibiwa. Aidha Shimo ameliagiza Jeshi la polisi kwa kushirikiana na uongozi wa soko hilo pamoja na Viongozi wa kata kuahakikisha wanashirikiana kuwasaka wote waliokwenda kutoa msaada na kuiba mali ambazo zilikuwa hazijateketea. "Mwenzio alitarajia umekuja kuchukua zile nguo ambazo hazijaungua moto uzitunze mahala uumpe lakini wewe zile nguo unachukua unapeleka unakojua wewe mwenyewe huo ni wizi tabia hii na hii roho sio nzuri sana si jambo jema na huo si utanzania wetu ni bora hii tabia ikafichuliwa" ——— Shimo, Mkuu wa wilaya. from UDAKU SPECIAL https://bit.ly/3rXyLJC via IFTTT