Posts

Showing posts from April, 2021

The Industry yamtambulisha msanii wake mpya, isikilize ngoma yake hapa

Image
  The Industry yamtambulisha msanii wake mpya, isikilize ngoma yake hapa VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3e7lcBu via IFTTT

Irene Uwoya acharuka,azungumza kwa ukali ‘Mimi ni mkorofi, iwe mwanzo na mwisho’

Image
Ni Headlines za Mwigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Irene Uwoya ambae time hii ameonekana kuongea kwa ukali baada ya  jina lake kutumiwa vibaya na watu kwanjia ya kutapeli mashabiki zake. ‘Naomba niongee haraka haraka sana kuna watu wanakera tena wananikera sana tena wanahisi mimi ni mpole naomba wajue mimi ni mkorofi sana, nimechoka na tabia za watu kufanya utapeli kwa kutumia jina lako huko Facebook sijapenda nimechoka’– Irene Uwoya from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/335i8zG via IFTTT

Rais Samia atakuwa Mgeni Rasmi Mei Mosi leo Jijini Mwanza.

Image
  Rais Samia atakuwa Mgeni Rasmi Mei Mosi leo Jijini Mwanza. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2Rg6gYE via IFTTT

Ugonjwa wa kisukari ni tatizo linalopakana na matatizo yaliyopo kwenye mfumo wa utoaji vichocheo

Image
•ðŸ‘‰hata hivyo tatizo hili limeonekana kuwa kubwa na kuongezeka kutokana na sababu lukuki ambazo watu ushindwa kuziepuka  ðŸ‘‰kama lilivyo jina kisukari hutokana na kuongezeka kwa sukari kwenye damu kuzidi kiwango cha kawaida kinachotakiwa kuwepo  DALILI ZA KISUKARI 👉 Kiu ya maji isiyoisha 👉Njaa Kali Sana 👉Kwenda haja ndogo mala Kwa mala 👉Vidonda au michubuko inayochelewa kupona 👉Ukungu machoni 👉Kupoteza uzito bila sababu  MADHARA YA UGONJWA WA  KISUKARI 👉 kupata ukipofu 👉 vidonda vya kudumu ambavyo hupelekea kukatwa kwa baadhi ya sehemu za mwili kama vidole na miguu  👉 kuathirika kisaikolojia    ðŸ‘‰pia kwa wanaume kukosa nguvu za kiume Pindi uonapo ishara izi tutafute mapema tukupe dawa upone kabisa tatizo ili Na Kwa wale wagonjwa wa KISUKARI wa muda mrefu tuna dawa za kuponesha tatizo kabisa  Pia tuna dawa ya kutibu matatizo ya nguvu ZA kiume na sababu zake zote kama vile  👉Kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa 👉 Maumbile kusinyaa

Serikali Yafunga mtambo wa kisasa JKCI wenye thamani ya shilingi bilioni 4.6

Image
Serikali imefunga mtambo wa kisasa wenye thamani ya shilingi bilioni 4.6 wa uchunguzi na matibabu ya moyo (Catheterization Laboratory – Cathlab) uliounganishwa na mtambo wa  Carto 3 System 3D &  mapping electrophysiology System  ambao unauwezo wa kufanya uchunguzi na  kutibu hitilafu ya mfumo wa umeme  wa moyo. Fedha za kununuliwa kwa mtambo huo ambao umefungwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) zilitolewa na Serikali mwanzoni mwa mwaka jana. Akizungumza na waandishi wa habari jana  jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi alisema mtambo huo umeshaanza kutumika, licha ya kutibu mfumo wa  umeme wa moyo pia utafanya uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo, kuweka vifaa visaidizi vya moyo pamoja na kuzibua mishipa ya damu ya moyo iliyoziba. “Tunaishukuru Serikali kwa kuiwezesha JKCI na kufunga mtambo huu wa kisasa   ambao unauwezo wa kufanya uchunguzi na  kutibu hitilafu ya mfumo wa umeme  wa moyo.Kufungwa k

Katibu Mkuu CCM Daniel Chongolo aanza kazi, aongoza kikao cha utambulisho kwa Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM

Image
 Katibu Mkuu mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo, jana jioni ameripoti ofisini na kuendesha kikao maalum cha utambulisho kwa Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa katika ofisi za makao makuu ya chama hicho jijini Dodoma. Kikao hiko kimehudhuriwa na Wajumbe wapya akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), -Christina Mndeme na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka. Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Viongozi wastaafu wa CCM wakiongozwa na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), – Rodrick Mpogolo na aliyekuwa Katibu wa NEC, Oganaizesheni Pereira Silima. Chongolo amechaguliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuwa Katibu Mkuu mpya wa chama hicho, kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Bashiru Ally. Kabla ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, Chongolo alikuwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es salaam. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2QDCyNC via IFTTT

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 01

Image
chn  Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 01 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3eJpL3V via IFTTT

Breaking News: Shaka Hamdu Shaka ameteuliwa kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi

Image
Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM katika kikao chake maalumu kilichoketi leo baada ya Mkutano Mkuu wa Chama hicho chini ya Mwenyekiti Samia Suluhu imeridhia mapendekezo yaliyotolewa na Mwenyekiti (Rais Samia) katika Sekretarieti Kuu kuwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM Morogoro, Shaka Hamdu Shaka ndiye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM- Taifa akichukua nafasi ya Humphrey Polepole. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3t1CDYx via IFTTT

Christina Mndeme ateuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM- Bara

Image
Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM katika kikao chake maalumu kilichoketi leo baada ya Mkutano Mkuu wa Chama hicho chini ya Mwenyekiti Samia Suluhu imeridhia mapendekezo yaliyotolewa na Mwenyekiti (Rais Samia) katika Sekretarieti Kuu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ndiye Naibu Katibu Mkuu wa CCM- Bara. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3e4y9vH via IFTTT

Daniel Chongolo ateuliwa Katibu Mkuu CCM

Image
Chama cha Mapinduzi  CCM kimemteua mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo kuwa katibu mkuu wa chama hicho tawala kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Bashiru Ally. Chama hicho pia kimemteua Christina Mndeme kuwa naibu katibu mkuu Bara huku  Abdallah Juma Sadala akiendelea kuhudumu nafasi hiyo upande wa Zanzibar Katibu wa itikadi na uenezi iliyokuwa ikishikiwa na Humprey Polepole, sasa itashikiliwa Shaka Hamidu Shaka na katibu wa uchumi na fedha ni Frank Hawasi. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3ujXFTm via IFTTT

IDADI ya waliokufa kutokana na janga la virusi vya corona nchini Brazil imefikia watu 400,000L

Image
IDADI ya waliokufa kutokana na janga la virusi vya corona nchini Brazil imefikia watu 400,000 hadi jana katika wakati ambapo taifa hilo linapambana kupata chanjo za kutosha kudhibiti kuenea zaidi kwa kadhia hiyo.   Jana wizara ya afya ya nchini humo iliripoti vifo vya watu 3,001 ndani ya muda wa saa 24 na kufanya jumla ya watu waliokufa kufikia 401,186, idadi inayoifanya Brazil kuwa taifa la pili kwa idadi kubwa ya vifo vya Covid-19 nyuma ya Marekani.   Taifa hilo lenye uchumi mkubwa kwenye kanda ya Amerika ya Kusini limeshuhudia ongezeko la kutisha la maambukizi ya virusi vya corona tangu kuanza kwa mwaka 2021 huku hospitali karibu zote zikizidiwa kwa wingi wa wagonjwa.   Serikali ya nchi hiyo inahangaika kutafuta shehena ya dozi za chanjo ya Covid-19 baada ya kufanikiwa kutoa chanjo ya kwanza kwa raia milioni 28 pekee ambayo ni asilimia 13 ya watu wa taifa hilo.   from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2PGdMfc via IFTTT

Bwalya: Tutafanya Maajabu Kimataifa… Droo Ya CAF Leo

Image
KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Larry Bwalya amesema kuwa timu hiyo ina nafasi kubwa ya kufanya maajabu katika Hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo inatarajiwa kupangwa leo Ijumaa.   Bwalya alijiunga na Simba mwanzoni mwa msimu huu baada ya kiwango chake kufurahishwa na mabosi wa timu hiyo.   Akizungumza na Championi Ijumaakuelekea kwa droo hiyo ambapo Simba ndiyo itajua mpinzani wake, Bwalya alisema: “Imekuwa heshima kwangu na timu pia kuona tunafanikiwa kutinga hatua ya robo fainali katika michuano ya kimataifa. “Kwa sasa tunasubiri ratiba na timu ambayo tutacheza nayo katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.   “Bado tunayo nafasi ya kutwaa ubingwa wa michuano hiyo kutokana na maandalizi mbalimbali ambayo tunaendelea kufanya, “ alisema Bwalya.   Katika droo ya leo Simba inatarajiwa kupangwa na wapinzani kati ya hawa, CR Belouizdad au MC Alger zote za Algeria au Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini Stori: Leen Essau,Dar

Yanga kuwakosa nyota watatu dhidi ya TZ Prisons leo

Image
Msemaji klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli amethibitisha kuwakosa wachezaji nyota watatu wa kikosi cha kwanza kwenye mchezo wa mtoano wa 16 bora wa kombe la Shirikisho dhidi ya TZ Prisons utakaochezwa saa 10:00 jioni ya leo kwenye uwanja wa Nelson Mandela mkoani Rukwa. Wachezaji hao watakaokosekana ni viungo wa kati,Tonombe Mukoko, Feisal Salum “Fei Toto” na mshambuliaji Michael Sarpong baada ya wachezaji hao kuoneshwa kadi za manjano tatu mfululizo hivyo kutumikia adhabu ya kukosa mchezo mmoja. Benchi la ufundi la Yanga linaloongozwa na kocha wake mpya, Mtunisia, Mohammed Nasruddine Nabi linatazamiwa kuwageukia viungo Zawadi Mauya kuchukua nafasi ya Tonombe Mukoko,Carlinhos kucheza nafasi ya Fei Toto na Ditram Nchimbi kama mbadala wa Sarpong. Kwa upande wa nahodha wa Prisons, Benjamin Asukile amejinasibu kuwaondoa Yanga na kutinga robo fainali kwasababu wamejiandaa vya kutosha ukizingatia na kusema wana uwezo wa kufanya hivyo tena kwenye dimba lao la nyumbani. Ikumbukwe kuwa,

Breaking: Nyalandu Atangaza Kurejea CCM Mbele ya Rais Samia

Image
Aliyewahi kuwa mwanachama wa CCM na Waziri wa Maliasili na Utalii na kisha baadaye kujiunga na Chadema Lazaro Nyalandu ametangaza rasmi kurejea CCM mbele ya Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Samia Suluhu kupitia Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Dodoma leo Aprili 30, 2021 akitokea CHADEMA. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3tcx6ys via IFTTT

Mke wangu aligawa watoto wangu kwa mwanaume mwingine baada ya kuachana

Image
Ni kweli katika Maisha huwezi pata mwanamke au mwanaume ambaye ataweza penda  unachokipenda na kuchukia kila unachokichukia,Kabla ujamuoa mwanamke siku zote kila mtu uwa  anaficha tabia yake hivyo ni vigumu kuweza kutambua upande wa pili.Mara nyingi mwenzako  anaweza sema jambo analolipenda na jambo ambalo halipendi kwa kuwa mpo katika mausiaoni na  wewe mwenyewe unasema unapenda kile alichosema na unachukia kile anachokichukia.  Mkisha anza kuishi wote ndipo mwanaume au mwanaume anatoa makucha yake aliyokuwa  ameficha mwanzo,kwa kuwa huwezi pata mwenza wako ambaye atapenda na kuchukia kila  unachokichukia hivyo inakuwa haina budi kuvumiriana kati yenu wawili.kwa ufupi mimi naitwa  Nelson mkazi wa Dodoma nilibahatika kumuoa Maria ambaye mwanzo kabisa tulipendana ikafikia  hatua ya kupata ridhaa kutoka kwa wazazi na hatimaye tukafunga ndoa kanisani.  Hapo mwanzo maisha yetu ya ndoa yalikuwa yamejaa amani na furaha,hivyo tulibahatika kupata  watoto wawili(lime,kike).Maria baada ya kuj

Malkia wa Zulu afariki dunia mwezi mmoja baada ya kuchukua majukumu ya kifalme

Image
Familia ya kifalme ya Zulu nchini Afrika Kusini imetangaza kifo cha Malkia wake aliyekuwa anaongoza eneo hilo Shiyiwe Mantfombi Dlamini Zulu, mwezi mmoja tu baada ya kutawazwa kuchukua majukumu ya kifalme. Malkia Mantfombi, 65, alikuwa kiongozi wa mpito wa kabila la Zulu ambalo ndilo kubwa zaidi nchini Afrika Kusini baada ya kifo cha mume wake, Mfalme Goodwill Zwelithini. Waziri mkuu wa malkia huyo amesema kifo chake kimeshutua familia ambayo ipo kwenye masikitiko makubwa kwa kumpoteza. Mrithi kama mtawala wa eneo la Wazulu lenye watu milioni 11 bado hajatajwa. "Ni huzuni na masikitiko makubwa kwamba Familia ya Kifalme inatangaza kifo ambacho hakikutarajiwa cha Malkia Shiyiwe Mantfombi Dlamini Zulu, wa Wazulu," Mwanamfalme Mangosuthu Buthelezi, waziri wake mkuu amesema kwenye taarifa. Aliongeza kuwa anataka kuhakikishia watu kwamba hakutakuwa na "ombwe la uongozi kwa eneo la Wazulu". Malkia Mantfombi alilazwa hospitalini wiki moja iliyopita baada ya

Mwambusi Atoweka kimyakimya Yanga

Image
KWA kauli ya kiungwana aliyoitoa ya Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Haji Mfikirwa sasa ni wazi kuwa aliyekuwa Kaimu Kocha Mkuu wa Yanga, Juma Mwambusi atakuwa rasmi ameachana na klabu hiyo tangu zilipoibuka taarifa zake za kwenda kwao Mbeya kwa ajili ya kuhani msiba wa nduguye.   Tangu Mwambusi akabidhiwe mikoba ya aliyekuwa kocha wao, Cedrick Kaze amedumu na kikosi hicho kwa takribani miezi miwili, ambapo ameisaidia timu kuvuna pointi 7, kwenye michezo mitatu aliyohudumu kama mkuu wa benchi la ufundi.   Kwani kabla Yanga haijaruhusu kichapo cha pili kwenye Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC, Jumapili iliyopita timu ikiwa chini ya Mtunisia Nasreddine Al Nabi, kwenye mchezo uliyochezwa Jumapili iliyopita, Mwambusi aliiongoza kupata sare dhidi ya KMC na baadaye akavuna pointi tatu dhidi ya Mtibwa Sugar kisha dhidi ya Gwambina FC.   Championi Ijumaa limezungumza na Kaimu Mwenyekiti wa Yanga, Haji Mfikirwa ambaye ameweka wazi kuwa, wao kama klabu tayari wameshafanikisha nia yao ya

Breaking News: Rais Samia Suluhu achaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa CCM

Image
Rais Samia Suluhu amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kura zote 1862 za ndio za Mkutano Mkuu Maalum sawa na asilimia 100. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2RdPSbm via IFTTT

Msanii Harmonize achora Tattoo ya Hayati Magufuli

Image
 CEO wa lebo ya Konde Music Wordwide na msanii Harmonize amechora 'Tattoo' ya picha ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli. Tattoo hiyo ameichora kwenye mguu wake wa kulia akiwa Lagos nchini Nigeria, kisha ameandika maneno yafuatayo "Mimi nime-sacrifice maisha yangu kwa ajili ya watanzania maskini". Picha na video hizo akiwa anachora tattoo hizo amezishea kwenye 'Insta Story' ya ukurasa wake wa Instagram halafu mwisho wa picha hizo akaandika 'RIP Kamanda'. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3aQrpQh via IFTTT

Prisons: Tutawapiga Yanga Kwenye Mshono

Image
NAHODHA wa kikosi cha Tanzania Prisons, Benjamin Asukile amewachimba mkwara wapinzani wao katika mchezo ujao wa Kombe la FA, Yanga, kwa kusema kuwa wanapaswa kujiandaa kisaikolojia kwani baada ya kufungwa na Azam FC, kipigo kingine kinawasubiri huko Sumbawanga.   Prisons, leo Ijumaa itawakaribisha Yanga katika mchezo wa Hatua ya 16 Bora wa michuano ya Kombe la FA, utakaopigwa kwenye Uwanja wa Nelson Mandela uliopo Sumbawanga mkoani Rukwa.   Yanga itaingia katika mchezo huo ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kipigo cha bao 1-0 walichokipata kutoka kwa Azam FC, Jumapili iliyopita katika Ligi Kuu Bara (VPL). Kumbukumbu ya mwisho inaonyesha kwenye michezo miwili ambayo timu hizo zimekutana msimu huu kwenye VPL, zilitoa sare pacha ya bao 1-1 mara mbili, Septemba 6 na Desemba 31, mwaka huu.   Akizungumza na Championi Ijumaa,Asukile alisema: “Tunaendelea na maandalizi ya mchezo wetu ujao dhidi ya Yanga, tuko tayari na tunawasubiri kwa hamu kwa kuwa siku zote tunapokutana na Yang

Ben Pol Afunguka Kwa Mara ya Kwanza Kuhusu Kuomba Ndoa yao na Arnelisa Ivunjike

Image
Ben Pol Afunguka Kwa Mara ya Kwanza Kuhusu Kuomba Ndoa yao na Arnelisa Ivunjike TAARIFA  SHAURI LA TALAKA  Ben Pol angependa kuthibitisha uwepo wa shauri la talaka dhidi ya mke wake linaloendelea katika Mahakama ya mwanzo hapa Dar es salaam. Mahakama bado HAIJATOA talaka/ maamuzi yoyote mpaka pale litakaposikilizwa na kukamilishwa. Masuala haya ni ya BINAFSI sana na kwa kuwa shauri linaendelea Mahakamani Ben Pol asingependa lizungumzwe zaidi kwa heshima ya pande zote na kwa kuheshimu kazi ya Mahakama. Pia anaomba nafasi na faragha kwake na kwa familia katika kipindi hiki kigumu. Anawashukuru wote kwa uelewa na pia kwa familia, marafiki na mashabiki wote kwa support mnayoendelea kuionesha. Uongozi wa Ben Pol. ______________________ By date: 29 April 2021  Headline: Ben Pol's divorce proceedings are ongoing.  At this time, Ben Pol would like to confirm that his divorce proceedings are in progress at the primary court but have not yet been finalised. These

Sheria ya uhujumu uchumi kufumuliwa

Image
Hatua ya Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria kufanyia tathmini sheria sita, ikiwamo ya uhujumu uchumi, imepokelewa kwa furaha na wadau wa sheria ikielezwa kuwa ni kilio cha muda mrefu cha kuondoa sheria kandamizi za muda mrefu. Hatua hiyo imetangazwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi jana, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2021/2022, akisema lengo ni kufahamu kama sheria hizo zinaweza kutumika katika kupunguza msongamano magerezani. Mbali na uhujumu uchumi, Profesa Kabudi alizitaja sheria nyingine zinazofanyiwa tathmini kuwa ni pamoja na Sheria ya Magereza, Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai na Sheria ya Huduma za Jamii, Sheria ya Bodi ya Msamaha na Sheria ya Kikomo cha Adhabu. “Madhumuni ya tathmini hii ni kubainisha kama sheria zilizopo zinaweza kutumika kupunguza msongamano magerezani na hivyo kupunguza gharama za kuendesha magereza,” alisema. Profesa Kabudi alisema k

Harmonize achora tattoo ya hayati Rais Magufuli

Image
Staa wa Bongo Fleva na CEO wa @kondegang @harmonize_tz ame share picha ikionyesha amechora tattoo ya hayati Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kwenye mguu wake. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3e3lSHW via IFTTT

Misri: Wanasayansi wagundua maiti ya kale ya mwanamke mjamzito

Image
  Timu ya wanasayansi nchini Poland imesema wamegundua maiti pekee ya kale ya mwanamke mjamzito huko Misri iliyokuwa imehifadhiwa. Ugunduzi huo umebainika na wanasayansi wa eneo la hifadhi ya maiti la Warsaw na kuandikwa katika jarida la Sayansi la Akiolojia. Hifadhi hiyo iliyoanzishwa mwaka 2015, na inatumia teknolojia ya kisasa kutathmini viti vya kale vilivyohifadhiwa katika Makubusho ya Taifa iliyopo Warsaw. Awali, maiti hiyo ilikuwa ikidhaniwa kuwa ya kasisi wa kiume lakini uchunguzi wa CT Scan ukaonesha kuwa ni maiti ya mwanamke aliyekuwa hatua ya mwisho ya ujauzito. Wataalam kutoka hifadhi hiyo wanaamini kuwa mabaki hayo yalikuwa ya mwanamke wa hadhi ya juu kati umri wa miaka 20 na 30, aliyefariki dunia karne ya kwanza kabla ya kristo. “Kinachooneshwa hapa ndio mfano pekee unaojulikana wa maiti ya kale ya mwanamke mjamzito,” makala katika jarida hilo imeandikwa ikitangaza utafiti wake. Kwa kutumia urefu wa kichwa cha mtoto aliyekuwa tumboni, walikadiria alikuwa

Kocha Yanga Aibuka na Mikakati Mipya

Image
KATIKA kuhakikisha wanafanya vizuri kwenye michuano ya Kombe la FA, Kocha wa Makipa wa Yanga raia wa Kenya, Razack Siwa, amesema wataingia uwanjani kucheza michezo hiyo kama fainali ili kufanikisha malengo yao ya kutwaa ubingwa.   Hiyo ikiwa siku chache katika kuelekea mchezo wa hatua ya 16 bora wa michuano hiyo utakaopigwa kesho Ijumaa kwenye Uwanja wa Nelson Mandela, Rukwa dhidi ya Prisons.   Akizungumza na Spoti Xtra, Siwa alisema licha ya kuupambania ubingwa wa Ligi Kuu Bara, lakini nguvu zao hivi sasa wanazielekeza katika michezo ya FA kwa lengo la kubeba kombe hilo. Siwa alisema katika michezo iliyobaki ya ligi na FA, watahakikisha wanacheza kama fainali ili kufanikisha malengo waliyojiwekea msimu huu ya kubeba ubingwa.   Aliongeza kuwa, anaamini haitakuwa kazi nyepesi, lakini watahakikisha wanapambana kwa kushirikiana na wachezaji, viongozi na mashabiki ambao ndiyo watu muhimu kwao. “Tumepoteza mchezo uliopita wa ligi dhidi ya Azam, lakini haitatufanya tu

Bwege: Wapinzani tusijaribu kumzingua Rais

Image
Na Ahmad Mmow, Lindi.  Viongozi wa vyama vya upinzani vya siasa nchini wametahadharishwa wasimuamrishe Rais afanye wanayotaka.  Wito na tahadhari hiyo imetolewa na aliyekuwa mbunge wa jimbo la Kilwa Kusini, Seleman Bungara (Bwege) leo alipozungumza na Muungwana Blog kwa simu kutoka Kilwa Kivinje.  Alisema kuna dalili kwa baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kutaka kumshinikiza Rais badala ya kumuomba na kushauri afanye wanayotaka wao.  Bwege alisema wapinzani hawana haki wala sababu ya kumshinikiza Rais Samia Suluhu Hassan. Bali wamshauri, wamshawishi na wamuombe afanye ambayo wanadhani yana tija kwa taifa. Bila kuwataja   viongozi hao, alisema wanamshinikiza Rais Mama Samia Suluhu Hassani badala ya kumkumbusha,  Kumshawishi na kumuomba.  Huku wakijua kwamba Rais hashinikizwi, bali anauoneshwa ukweli na kuambiwa kiustarabu na heshima. Alisema wapinzani wanatakiwa watambue ukweli kwamba  Rais ni kama mtu aliyeshika mpini wakati wapinzani ni kama mtu alishika kis

Shomari Kapombe aongeza mkataba Simba

Image
Beki wa pembeni wa Simba, Shomari Kapombe amesaini dili jipya baada ya kukubaliana na uongozi kuongeza mkataba. Beki huyo mzawa chaguo namba moja la Kocha Mkuu, Didier Gomes mkataba wake ulikuwa unafika ukingoni mwishoni mwa msimu wa 2020/21. Alikuwa anatajwa kuingia rada za FAR Rabat ya Morocco pamoja na timu nyingine nchini Afrika Kusini ambazo zilikuwa zinahitaji saini yake. Baada ya makubaliano mazuri na mabosi wake wa sasa nyota huyo amesaini dili jipya na inaelezwa ni kandarasi ya miaka miwili. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3nx1fHs via IFTTT

DC Hai Sabaya: akamata vifaa vya kutoa mimba na kung’oa meno ,alijifanya anafanya biashara ya mpesa

Image
Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya na Kamati ya Ulinzi na Usalama imeongoza operesheni maalumu iliyofanikiwa kupatikana kwa vituo vya Afya Bubu ambavyo awali wamiliki waliendesha maduka yao kana kwamba wanafanyabiashara ya M-pesa/kubadili fedha kwa njia ya Mtandao huku kiuhalisia wanaendesha biashara ya kutibu na kuuza madawa ya binadamu kinyume cha kanuni na Taratibu za Afya. Ole Sabaya ameelekeza mmiliki wa duka hilo Othaman Kimaro kushikiliwa na vyombo vya Dola ili atoe ushirikiano kwa matukio mbalimbali ikiwemo maelezo kuhusu vifaa maalum vya kutoa mimba, kung’oa meno, pamoja na kupatikana na madawa maalum ambayo kwa mujibu wa taratibu hutolewa kwa kibali maalum. Ni daktari feki akitoa huduma za kibingwa. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3u3F79P via IFTTT

Tanzania, Marekani Mambo Safi

Image
SERIKALI ya Tanzania imewahakikishia Wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Marekani mazingira mazuri na kuwasihi kuendelea kuwekeza hapa nchini.   Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula alipokutana kwa mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Donald Wright katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.   Balozi Mulamula amesema makampuni mbalimbali kutoka Marekani yameonesha nia ya kuwekeza katika sekta za nishati, miundombinu, afya na kilimo hususani katika zao la korosho.   “Katika kikao changu na Balozi tumejadili na kusisitiza umuhimu wa Kampuni za Marekani kuwekeza nchini Tanzania……… na Balozi amenihakikishia baadhi ya kampuni hizo zipo tayari kuwekeza hapa nchini,” amesema Balozi Mulamula   Aidha, Waziri Mulamula amewataka wafanyabiashara na wawekezaji wa Kitanzania kujipanga kutumia fursa ya kuuza Marekani bidhaa mbalimbali zinazozalishwa hapa nchini.   Kwa Upande wake Balozi wa M

JE ni Sahihi Kuzima Simu Usiku Unapokwenda Kulala?

Image
Baadhi ya wadau  wanasema ni tabia mbaya kuzima simu usiku kwasababu unaweza ukatokea uvamizi nyumba ya jirani na wakashindwa kukupata hewani ukaonekana hauna ushirikiano wakati wa shida Wengine wanasema, kila jambo na wakati wake. Wakati wa kulala si wakati wa kuhangaika na simu ambayo kutwa nzima umeikodolea macho na kuigusagusa, nayo iache ipumzike. Wanasema taarifa ya msiba, hata ukipewa usiku haikusaidii lazima utasubiri kuche tu Je, unadhani ni sawa kuzima simu usiku au kuiacha wazi? from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3bRVe4n via IFTTT

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH SHARIFU FIKILI NGHAMBI wa MKOANI MOROGORO

Image
Ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu Anatibu kwa kutumia visomo na dua pia  UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika. ............................... JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na  SHARIFU FIKILI NGHAMBI ujionee muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 72 TU.  ............................... Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.  Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi .............................. SHARIFU FIKILI NGHAMBI ANATUMIA  Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako, Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, DAWA za ASILI na DAWA za KIARABU, Pia ni mkuvunzi wa kutafsiri Ndoto. Pia anatoa pete za bahati zilizo ambatanishwa na JINI MALI, kum

Fahamu tabia za kimbunga, sababu za kuyeyuka kwa jobo

Image
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imesema kuwa wataendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na dhoruba mbalimbali za mambo ya hali ya hewa kama kimbunga ili wananchi wawe na ufahamu wa elimu lakini pia kuwa na utayari endapo majanga kama vimbunga yakitoa. Akizungumza katika kipindi cha mahojiano na Dar24Media kuhusu tabia za kimbunga, Meneja kituo kikuu cha utabiri TMA Samwel Mbuya, amesema kuwa kimbunga kina tabia ya kusafiri kwa kasi tofauti kutoka eneo moja kwenda eneo lingine. Aidha amesema kuwa kadiri mazingira yanavyobadilika na kimbunga hubadilika. “Kadiri kinavyokutana na mazingira rafiki kinaweza kuongeza nguvu, mwendo, mzunguko wake ukaongezeka kinapokutana na mazingira kinzani kinaweza kikapungua nguvu na pia hata kupunguza mwendo kinapokutana na vikwazo ambavyo ni mifumo mingine ya hali ya hewa,” amesema Mbuya. Ameongeza kuwa kimbunga kina tabia ya kuambatana na dhoruba ya upepo pamoja na mvua nyingi. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3t0DhW3 via

GSM wamefanya kazi kubwa sana Yanga, basi tu..

Image
  Na Gift Macha Baada ya Manji kuondoka Yanga, hali ilikuwa mbaya sana.. Yanga haikuwa na uwezo wa kusajili wachezaji wa maana.. Haikuwa na uwezo wa kuweka kambi nzuri wala kusafiri vizuri kwenda mikoani.. Hali ilikuwa mbaya kweli kweli. Hata hivyo baada ya kuja GSM mambo yamebadilika sana.. Haya ni maeneo ambayo GSM wamewekeza msimu huu. 1. Usajili Wachezaji wote wanaotamba Yanga msimu huu wameletwa na nguvu ya GSM. Tazama mabeki Kibwana Shomary, Yassin Mustapha, Bakari Mwamnyeto, Dickson job. Viungo Mukoko Tonombe, Feisal Salim ameongezewa mkataba na GSM. Kina Tuisila Kisinda, Saido Ntibazonkiza na Yacouba Sogne pia ni matunda ya GSM. Bahati mbaya ni kwamba wachezaji wengine waliosajiliwa kwa mategemeo makubwa kama Michael Sarpong, Waziri Junior, Fiston Abdoul Razack na wengineo wamewaangusha GSM. 2. Makocha Yanga msimu huu imekuwa chini ya makocha watatu wa kigeni na wote wameletwa na GSM. Alianza Zlatko Krmpotic, Cedric Kaze na sasa Mohammed Nabi. Zlatko na Kaze wa

Ugonjwa wa kisukari ni tatizo linalopakana na matatizo yaliyopo kwenye mfumo wa utoaji vichocheo

Image
•ðŸ‘‰hata hivyo tatizo hili limeonekana kuwa kubwa na kuongezeka kutokana na sababu lukuki ambazo watu ushindwa kuziepuka  ðŸ‘‰kama lilivyo jina kisukari hutokana na kuongezeka kwa sukari kwenye damu kuzidi kiwango cha kawaida kinachotakiwa kuwepo  DALILI ZA KISUKARI 👉 Kiu ya maji isiyoisha 👉Njaa Kali Sana 👉Kwenda haja ndogo mala Kwa mala 👉Vidonda au michubuko inayochelewa kupona 👉Ukungu machoni 👉Kupoteza uzito bila sababu  MADHARA YA UGONJWA WA  KISUKARI 👉 kupata ukipofu 👉 vidonda vya kudumu ambavyo hupelekea kukatwa kwa baadhi ya sehemu za mwili kama vidole na miguu  👉 kuathirika kisaikolojia    ðŸ‘‰pia kwa wanaume kukosa nguvu za kiume Pindi uonapo ishara izi tutafute mapema tukupe dawa upone kabisa tatizo ili Na Kwa wale wagonjwa wa KISUKARI wa muda mrefu tuna dawa za kuponesha tatizo kabisa  Pia tuna dawa ya kutibu matatizo ya nguvu ZA kiume na sababu zake zote kama vile  👉Kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa 👉 Maumbile kusinyaa

Beki wa Simba SC afungiwa mechi tatu

Image
Beki wa Simba SC Ibrahim Amme Mohamed amefungiwa mechi tatu kucheza soka baada ya kukutwa na hatia kwa kosa la kumzuia muamuzi msaidizi kufanya kazi yake katika mchezo Gwambina 0-1 Simba SC, uliyochezwa April 24 2021 katika Uwanja wa Gwambina Misungwi jijini Mwanza. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3aNJ8Yp via IFTTT

Rais wa Marekani aionya China kuwa hatavumilia chokochoko

Image
Rais wa Marekani Joe Biden amelihutubia bunge la nchi hiyo kwa mara ya kwanza akiwa rais na kutumia sehemu ya hotuba yake kuwaonya washindani namba moja wa kibiashara wa Marekani nchi ya Uchina. Biden amesema kuwa Marekani haitakaa kimya wakati makampuni ya kichina yakitia usalama wa makampuni ya kimarekakani na hata ajira za raia wake. Rais huyo amelieleza taifa lake kupitia hotuba hiyo ya bungeni kuwa katika mazungumzo yake na rais Xi Jinping wa Uchina, ameweka wazi msimamo wake kuwa japo Marekani haitafuti mgogoro na Uchina, lakini pia atalinda maslahi yake ya kibiashara kwa nguvu zake zote. "Marekani itasimama kidete dhidi ya tabia zisizo za mizania katika biashara kutoka Uchina. Mambo ambayo yanawaminya wafanyakazi wa Marekani na viwanda vyao. Mambo hayo ni kama kutoa ruzuku kwa viwanda vinavyoeindeshwa na serikali, wizi wa teknolijia ya kimarekani paoja na hatimiliki ." Mahusiano baina ya Marekani na Uchina yapo katika kilele cha migogoro kwa sasa. Mwezi Ma

Makala: Urafiki, Aadui wa Osama Bin Laden na Marekani; Al-Qaeda na ‘Ushetani’

Image
Na Josefly “Alikuwa mtoto mwenye sura ya mvuto, mpole na mwenye nidhamu. Ilikuwa nadra kutazamana naye moja kwa moja machoni. Alikuwa na aibu, msikivu na neno lake halikutoka kinywani mwake bila mpangilio,” alisema Bi. Alia Ghanem, mama mzazi wa Osama Bin Laden, aliyekuwa kiongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda akielezea maisha ya utotoni ya mwanaye, miaka nane baada ya kuuawa na makomando wa Marekani waliomsaka kila kona ya dunia kwa kipindi cha miaka kumi. Kwa mujibu wa mama huyo ambaye amebarikiwa kuishi hadi leo, tangu alipomzaa mwanaye Osama, Machi 10, 1957 katika mji wa Riyadh nchini Saudi Arabia, aliiona baraka na neema kwenye maisha ya mwanaye. Kila alipokuwa akivuka rika moja, alionesha kuwa na upeo wa hali ya juu. Darasani alikuwa na akili za kipekee na alifanikiwa kumaliza Shahada ya Uchumi kwa ufaulu mzuri katika Chuo Kikuu Cha King Abdulaziz kilichoko Jiddah, Saudi Arabia. Akiwa na umri wa miaka 20, alianza kuonesha makucha ya uwezo wake na alifanikiwa kuwa na ush