Posts

Showing posts from December, 2021

Mange Kimambi "Jamani Wananiloga"

Image
Reposted from @mangekimambi_ Dah, I hope you are all having a great new year because I’m definitely not. I have lost 90% of my database. Including users. Alafu kumbe tulikuwa hatuback database so there’s no way to restore. Sijui hata nini kimetokea ila nimekaa hapa nashindwa kujua nilie au. I’m still in shock. Yani mpaka mimi mwenyewe username yangu ime deletiwa. Anyways, that’s not your problem it’s mine. Naombeni mnisamehe kwa tatizo hili. Elfu moja ni hela nayo na nna deserve better than this. Sina kingine cha kufanya zaidi ya kutoa free service ya App na website kwa mwezi mzima. Nasubiria developers wa website ambao wako Tanzania waamke wabadilishe iwe bure na nasubiri developers wa App ambao wako India waamke wabadilishe pia iwe bure. Karibia woote mliokuwepo mwanzoni itabidi mfungue tena account mpya sababu account zenu hazipo tena. Nitaacha website na app ziwe free mpaka hapo ambapo teknolojia itakaa sawa. To my team don’t worry, I got you. Shemeji yenu atas

Tanzania Kupandikiza Mimba, Ukomo wa Ugumba

Image
  Wanawake wametakiwa kutafuta ushauri wa kitaalamu wanapokua katika wakati wa kutafuta ujauzito na kuacha tabia ya kusikiliza maneno ya mitaani au kuiga mifano ya wanawake wengine ambao wamepata Watoto kwa njia kadha wa kadha. Rai hiyo imetolewa na daktari Edmund Isaya alipozungumza katika mahojiano maalumu na Dar24 akielezea mfumo wa kupandikiza ujauzito kwa wanawake kitaamu IVF. “Mimi naamini kuwa vidole havifanani na wanawake hawafanani hata kila ujauzito haufanani hivyo hakikisha humuigi mtu linapokuja swala zito kama hili la IVF,” alisema Dkt. Edmund. Alifafanua kuwa IVF kwa lugha ya kitaalamu ni In Vitro Fertilization; na kwa lugha inayoeleweka kwa haraka ni upandikizaji wa mimba kwa njia ya teknolojia ya kulitoa yai nje ya mwili wa mwanamke na kutengeneza kiumbe ambacho hurudishwa tena kwa mwili wa mwanamke ili kulea kiumbe hicho mpaka kizaliwe. “IVF mara nyingi inafanyika pale ambapo wanandoa wamekosa kupata mtoto pamoja na kushiriki tendo la ndoa siku za urutubisha

Mwigizaji The Rock Ajitoa Kuigiza Filamu ya Fast & Furious Sehemu ya 10

Image
Muigizaji Dwayne Johnson maarufu kama the “The Rock” amekataa ombi la kurejea kuigiza muendelezo wa filamu ya Fast & Furious sehemu ya 10. The Rock katika interview yake na CNN iliyochapishwa siku ya jana amekataa ombi la Vin Diesel kurejea katika Fast & Farious na kumkosoa kwa kitendo chake cha kuongolea suala hilo katika mitandao ya kijamii kwa kuwahusisha watoto na marehemu Paul Walker. “Nilishangazwa sana na post ile ya Vin Diesel, mwezi wa sita mwaka huu niliongea nae faragha na kumwambia sitaweza kuigiza tena filamu hiyo ila nitatoa ushirikiano wangu katika kuandaa filamu hiyo ili kuhakikisha inafanikiwa na hata washirki wengine wote niliongea nao na walinielewa,” Majibu ya The Rock. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3pI7ivo via IFTTT

Kipindi cha XXL kupitia Clouds FM, kimetoa orodha yake ya nyimbo 20 bora za Bongo Flava zilizotoka mwaka 2021. Unaionaje orodha hii?

Image
Kipindi cha XXL kupitia Clouds FM, kimetoa orodha yake ya nyimbo 20 bora za Bongo Flava zilizotoka mwaka 2021. Unaionaje orodha hii? VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3HoJgvp via IFTTT

Ray Vanny azua gumzo baada ya kumuita Zuchu ‘Shem’

Image
  Ray Vanny azua gumzo baada ya kumuita Zuchu ‘Shem’` VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3Jz0Oqs via IFTTT

Taji Liundi "Mama Yetu Alitunywesha Sumu Mimi na Wadogo Zangu, Nilipona Wadogo Zangu Wakafariki"

Image
Kwa mara ya kwanza mtangazaji nguli nchini Taji Liundi amefunguka kuhusu maisha yake binafsi na mchango wake katika tasnia ya muziki. Taji Liundi aka Master T ambaye amefanya kazi na vituo mbalimbali vya redio ikiwemo Redio one na Times fm toka miaka ya 1980 amefunguka mengi wakati akihojiwa na kipindi cha Salama Na cha Salama Jabir. Taji Liundi amesimulia kisa cha kusisimua na kusikitisha ambapo mama yake mzazi aliamua kuwanywesha sumu yeye na wadogo zake watatu tukio lililopelekea wadogo zake watatu kufariki dunia huku yeye (taji) akiponea chupu chupu. Tukio Hilo lilitokana na mgogoro wa ndoa baina ya mama yao na baba yao kutokana na kukosekana kwa uaminifu hasa upande wa mzee wake, baada ya mama Taji maarufu sana nchini Agnes Doris Liundi kugundua hilo aliazimia kujiua yeye na wanaye na ndiyo kisa cha kuwanywesha sumu wanaye. Mama Taji alihukumiwa kunyongwa mpaka kufa na Mahakama kabla ya kupewa msamaha wa Rais na Hayati Baba wa Taifa J K Nyerere. Baba yake Taji Liundi alik

Anthony Diallo "Aliyesema Nchi Itapigwa Mnada Ametumia Lugha ya Kihuni"

Image
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Anthony Diallo ametoa tamko kuhusiana na nchi kukopa, Diallo amesema huyo aliyesema Tanzania itapigwa mnada hakutumia lugha ya kiuongozi bali ametumia lugha ya kihuni na kwa sababu CCM ni chama kikubwa basi atanyooshwa ili arudi kwenye mstari. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3zfmHq0 via IFTTT

Kagere, Wawa, Banda wavunjiwa mikataba Simba

Image
KLABU ya soka ya Simba imevunja mikataba ya nyota wake wanne wa kigeni wakiwemo mastaa wao aliokuwa tegemeo katika kikosi hicho kwa misimu kadhaa, beki wake Raia wa Ivory Coast, Pascal Wawa na mshambuliaji wake, Mnyarwanda, Meddie Kagere. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).  Mbali na mastaa hao wawili tegemeo, nyota wengine wa kimataifa waliotemwa ni Peter Banda aliyesajiliwa kwenye dirisha kubwa la usajili mwezi Agosti na kiungo mshambuliaji Dancan Nyoni Raia wa Malawi ambaye ameshindwa kuonesha makali yake toka asajiliwe klabuni hapo. Simba imeamua kuvunja mkataba na wachezaji hao, ili kupata nafasi ya kusajili wachezaji wengine wa kigeni kwenye dirisha dogo la usajili. Pascal Wawa Ikumbukwe hivi karibuni klabu hiyo ilivunja mkataba kwa makubaliano maalumu na kocha wake msaidizi Thiery Hitimana raia wa Burundi.   Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara wameamua kufanya maboresho kwenye kikosi chao kufuatia kusuasua hivi karibu. from UDAKU SP

Makala Agness: Nililipwa Mil 11 Kwenda Kufanya Mapenzi Nigeria

Image
KAMA ni mfuatiliaji wa mambo yanayoendelea mitandaoni, basi jina la Aggy Baby siyo geni kwako. Akifahamika zaidi kwa jina la Agness wa Mahari Milioni 500, alikuwa gumzo mitandaoni baada ya kutangaza kwamba mwanaume anayetaka kumuoa anapaswa kulipa mahari ya shilingi milioni 500. Kama hiyo haitoshi, akazua tena gumzo kwa kumpa ofa mchezaji wa Yanga, Feisal Salum ‘Fei Toto’ ya kumuoa bure kutokana na kukoshwa na uwezo wake uwanjani. Mbali na drama za hapa na pale, Aggy Baby ambaye jina lake halisi ni Agness Suleiman amejitwalia umaarufu kupitia Tamthiliya za Panguso na Huba zinazorushwa DSTV. Kubwa kabisa ni msanii mkali wa Bongo Fleva akiwa amesikika kwenye ngoma kadhaa zikiwemo Wanipa na Watajuaje zinazokiwasha kwenye miandao mbalimbali;   Gazeti la IJUMAA limepiga stori na Aggy Baby ambapo amefunguka mambo mbalimbali kuhusu maisha yake; IJUMAA:  Tukio gani kubwa ambalo hutalisahau maishani mwako? AGGY BABY: Nakumbuka, nilitumiwa Dola za Kimarekani 5000 ambazo ni saw

Ndoa ya Dida SHAIBU Iko Shwari Ajaachwa Wala nini, Muheshimiwa Meya Athibitisha

Image
  June 10 mwaka huu,watu walianza maisha rasmi ya ndoa kati ya mtangazaji maarufu nchini wa kipindi cha mashamsham cha Wasafi Fm, @didahshaibutz pamoja na Diwani wa Vingunguti na Meya wa jiji la Dar es salaam,mh. Omary Kumbilamoto. Huku na huku hivi karibuni wambea wakanasa ubuyu kuwa wawili hao wamepeana kikono,mh! ni mapema sana mjue,maneno kibao kwa Dida kuwa ana nyota ya kaniki,haeleweki msafi ama mchafu, ndoa zote za bando. Hasa kupitia U-HEARD ya XXL na @soudybrown , Mh. Kumbilamoto ameweka sawa kuwa ndoa yao ipo na inanoga kila leo, wao pia wanaona tu maneno mitandaoni na wanayazika. Mbali na Mh., shemeji mtu (kaka wa Dida) alikuwa ofisini kwa shemeji yake (sijui alikuwa anachezesha mzinga wa sikukuu) akapewa mkonga na Kumbilamoto na kuthibitisha kuwa hata wao wanashangaa mahasidi wa penzi la Dida, maana penzi lilivyo, ndoa kama imefungwa leo hata Honeymoon bado. Uheaard.... from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3sPJ98l via IFTTT

Rema Aingia Kumi na Nane za SHATTA Wale, Baada ya Kutweet Kutaka Wanawake 10 wa Ghana wa Kumpooza Akili

Image
Ikiwa ni siku chache tu,tokea msanii wa Ghana mwenye miondoko ya Reggae Dancehall, @shattawalenima kusema hataki wasanii wa Nigeria nchini Ghana kutokana na vitendo vyao vya kutosupport wasanii wengine wanaotoka nje na taifa lao, msanii Kinda tokea Nigeria, @heisrema ameyavagaa baada ya tweet yake kutaka wanawake 10 wa Ghana wataomtuliza akili punde tu atapotua nchini humo hapo kesho. Tweet hiyo imemfanya Shatta Wale aone ni kauli ya kuwavunjia heshina wanawake wa taifa lake la Ghana, huku akimuuliza kama hana pesa za kwenda kufanya massage hadi anatweet ujinga kwa kuwa tu yeye ni star. Pia Wale amedai kama wanamjua vizuri basi hawawezi zungumzia ishu za chuki,maumivu n.k anachofanya anawaambia ukweli mashabiki wa Nigeria na kama hawautaki wakanywe pamba. Pia jamaa ameahidi wakiendelea na ujinga huo,atawabebea mabango kwa miaka 30 kama wanatazama mchekeshaji wao pendwa wa kinaigeria. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3qHC07o via IFTTT

Joyce Kiria Aonekana Mwenye Furaha Sana ndani ya Penzi Jipya Baada ya ndoa zake Mbili Kuvunjika

Image
  Joyce anaonekana mwanamke anayejali sana pale anapopenda, ila huwa kile kinachotokea baadae huwa nje uwezo wake. Sababu ya uwazi wake Mahusiano yanapoanza kuyumba huwa hakuna siri. Na sio kwamba huyaacha mahusiano yavunjike hivihivi. Huwa anapambana lakini sababu hamna anachoweza kubadili hishia kuvunjika moyo, kuugulia hadi anapoibuka tena na kitu kipya Achilia mbali mateso aliyosema aliyapata hadi kuachana na mumewe wa kwanza yule DJ Nelly, Joyce ameonekana kuwa mwanamama mkweli na muwazi anapokuwa kwenye mahusiano na hata pale yanapovunjika. Haijalishi nini itakua hatma ya mahusiano yake ila Joyce ni aina ya wale wanawake ambao akipendwa anataka ulimwengu wote ujue kwamba anapendwa na amepata mtu sahihi kwa wakati ule na ana furaha. Nakumbuka wakati siasa za chadema zimeshika kasi Tanzania aliyekua mume wa Joyce Henry Kileo akawekwa ndani Joyce alivyopambana kumnusuru, tena akiwa na watoto wadogo. Hata kwenye kampeni za ubunge kule Mwanga Joyce alipambana kwelikweli kumsaid

Ongeza Maumbile, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa

Image
ONGEZEA UUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA!!!! Idadi kubwa ya wanaume wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume, umme mdogo pamoja na uume kusimama kwa ulegevu. Wanaume wengi huwa wanashindwa Kusimamisha uume vyema wakati wote wa tendo kutokana na *Kujichua (masterbution) *Kisukari (diabetes) *Homoni kushindwa kufanya kazi vizuri (homon disorders) *Unene uliopitiliza n.k Hali hii imesababisha ndoa na mahusiano mengi kuvunjika kutokana na mke kwenda nje ya ndoa ili kupata mtu wa kumridhhisha. Kwa kutumia mimea na matunda NATURAL BEAUTY CO inakuletea tiba ya uhakika, ya kumaliza tatizo moja kwa moja kama ifuatavyo:- 1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 100% kuongeza dhakari kwa size uipendayo na kuimarisha misuli iliyolegea @270,000/= 2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @200,000/= 3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha m

Prince Dube, Tigere Waikosa Simba

Image
NYOTA watatu wa Azam FC, Prince Dube, Never Tigere na Bruce Kangwa, huenda wakaukosa mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba utakaochezwa wikiendi hii kutokana na kuwa na majukumu kwenye timu yao ya taifa ya Zimbabwe. Wazimbabwe hao tayari wameungana na wenzao katika kambi ya kujiandaa na michuano ya AFCON inayotarajiwa kuanza Januari 9 hadi Februari 6, mwakani nchini Cameroon. Hivi karibuni, nyota hao ambao wanacheza kikosi cha kwanza cha Azam FC, wamejumuishwa kwenye kikosi cha awali cha Zimbabwe kabla ya kufanyika mchujo kesho Jumatano kupata kikosi ambacho kitashiriki AFCON. Akizungumza na Spoti Xtra, Ofisa Habari wa Azam FC, Thabit Zakaria, amesema: “Tigere, Kangwa na Dube wameitwa katika timu ya taifa ya Zimbabwe kwa kambi ya muda kuchuja wachezaji watakaokwenda AFCON. “Mchujo wao utafanyika Desemba 29, kama watafanikiwa kupenya, watasalia hukohuko, lakini wakishindwa, watarudi haraka kuuwahi mchezo dhidi ya Simba.” from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3HnV68W

Mwanamuziki Willy Paul Kugombea Ubunge Nchini Kenya

Image
 Kutoka kwenye post ya mwanamuziki @willy.paul.msafi ameandika “Are you ready Mathare? Let's bring that change. #levels” akiambatanisha na picha inayothibitisha nia ya kugombea kiti cha ubunge katika jimbo la Mathare nchini kenya mwaka 2022. Endapo mwanamuziki huyo atafanikiwa basi ataingi kwenye orodha ya wanamuziki walio geukia siasa akiwemo mbunge wa jimbo la starehe Charles Njagua Kanyi, (Jaguar). from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3HlKSpS via IFTTT

Rafiki wa Jana Ndie Adui Mkubwa Kesho, Makundi Kombe la Shirikisho Africa Yapangwa, Chama Uso Kwa Uso na Simba

Image
Klabu Ya Simba inatarajia kukutana na kiungo wake wa zamani, Clatous Chama baada ya kupangwa kundi D na  RS Berkane ya Morocco, hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika Mbali na Chama ndani ya kikosi hicho, pia Simba itakutana na winga wa zamani wa Yanga, Tuisila Kisinda. Chama aliuzwa na Simba katika klabu ya RS Berkane, ingawa hivi karibuni kulikuwepo na tetesi za kumrejesha ndani ya kikosi hicho cha Msimbazi, hivyo mashabiki watamshuhudia kupitia michuano hiyo ya Caf. Simba inashiriki michuano hiyo, baada ya kuanguliwa Ligi ya Mabingwa Afrika, hivyo iliangukia  michuano ya Kombe la Shirikisho, ambapo ilicheza na  Red Arrows ya Zambia na kuitoa kwa jumla ya mbao 4-2, ushindi uliwapeleka makundi. Simba imepangwa kundi D na RS Berkane, Asec Mimosas na Us Gendarmerick National. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3z55NdT via IFTTT

Diamond alihitaji ngoma 12 tu kwenye album yake, amerekodi 51, na sasa inabidi afanye hili

Image
Diamond alihitaji ngoma 12 tu kwenye album yake, amerekodi 51, na sasa inabidi afanye hili VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/345Sv5r via IFTTT

Kumekucha, Maua Sama na ALI KIBA Waungana Kuipinga AMAPIANO " Siwezi Fanya Hata Uje na SUMA JKT na wale makomando wa Miaka 60 ya Uhuru"

Image
  AliKiba amemuunga mkono mwimbaji Maua Sama katika kuupiga vita kali muziki wa Amapiano, Kiba amekaa upande wa @mauasama ambaye kupitia twitter aliileta hoja hiyo na kuweka msimamo wake kwamba kuimba kwenye biti ya Amapiano inabidi mtayarishaji aje na SUMA JKT na wale makomando wa Miaka 60 ya Uhuru from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3za0olz via IFTTT

Kisa Cha SODOMA..Mungu Aliwashushia Mvua ya Moto Kwa Kuendekeza USHOGA...Walitaka Kuwabaka Malaika

Image
#TheStoryBook #SodomaNaGomorrah  Hadithi kamili ya kisa cha Mji wa Washenzi Sodoma na Gomora, na jinsi Mungu alivyouangamiza kwa moto na kupindua Ardhi Juu chini Tazama VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/33y6aye via IFTTT

Taarifa Rasmi..Simba SC waachana na kocha msaidizi, Thierry Hitimana

Image
  Simba SC waachana na kocha msaidizi, Thierry Hitimana from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3Jp5gbm via IFTTT

Maiti 200 zafukuliwa Dar es Salaam

Image
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, imeanza kufukua makaburi zaidi ya 200 yaliyopo katika Mtaa wa Butiama, Kata ya Vingunguti ili kuyanusuru kutokana na kubomoka kwa kingo za Mto Msimbazi. Kazi ya ufukuaji miili hiyo imeanza leo, ambapo mamia ya wananchi walijokeza kufukua ndugu zao na hivyo kusababisha simanzi kutawala katika eneo hilo. Akizungumza katika eneo la tukio, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto,alisema miili hiyo itazikwa upya katika eneo la Mwanagati. “Tufukua miiili 200 kutoka makaburi haya ya Butiama, yaliyopo katika Kata ya Vingunguti kwenda kuzikwa upya katika eneo la Mwanagati. Kulikuwa na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi kutokana na Mto Msimbazi kubomoa makaburi haya na miili kuondoka na maji,” alisema Kumbilamoto. Alisema awali Jiji la Dar es Salaam, lililenga kufukua makaburi 189 lakini kutokana na wananchi wengi kujitokeza kuomba ndugu zao walio zikwa katika eneo hilo kufukuliwa na kuhamishwa hivyo huenda idadi ya miili ku

Okwi, Aucho watoswa Uganda Cranes

Image
KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’, Milutin Sredojevic ‘Micho’ ameita kikosi cha wachezaji 23, kitakachoingia kambini kwaajili ya michezo ya kimataifa dhidi ya Gabon Desemba 30 na Mauritania Januari Mosi. Katika kikosi hicho Kocha Micho amemuita kiungo Chris Pius Akena, kikosini kwa mara ya kwanza huku Khalid Aucho wa Yanga na Emmanuel Okwi anayecheza Kiyovu ya Rwanda wakiachwa. Akena anayecheza katika kikosi cha Ahly Shabab FC, ambacho kinashiriki Ligi Kuu ya Falme za Kiarabu (UAE) amewashtua wengi baada ya kuitwa na kocha Micho.   Akena ni miongoni mwa wachezaji watatu walioitwa mapema kikosini pamoja na kiungo wa URA, Shafik Kuchi Kagimu na nahodha wa BUL George Kasonko. Nyota huyo wa zamani wa Maroons, aliyekulia katika kituo cha kukuzia vipaji cha Pro-Way Soccer Academy chini ya usimamizi wa Aspire kutoka nchini Qatar alijiunga na Ahly Shabab Januari mwaka huu. Kiungo huyo tayari ameshinda taji la UAE Pro League akiwa katika kikosi cha vijana ch

Ndo hivyo Chama kufuata nyayo za Okwi

Image
HABARI za kurejea nchini kwa kiungo fundi raia wa Zambia, Clatous Chama ‘Mwamba wa Lusaka’ zimepamba moto kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo ambapo timu mbalimbali inakitumia kuimarisha vikosi vyao. Klabu za Simba na Yanga ndio ambazo zimekuwa zikihusishwa na kiungo huyo ambaye anaichezea RS Berkane ya Morocco inayonolewa na Florent Ibenge. Simba inaonekana kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kupata huduma ya Chama kutokana na kipengele cha kimkataba (wa Chama) ambacho kinaeleza ikiwa fundi huyo atataka kurejea tena Tanzania basi chaguo la kwanza ni timu hiyo. Kipengele hicho kinaelezwa kuwa kiliwekwa wakati ikifanyika biashara ya uhamisho wa Chama kutoka Simba na kwenda Morocco kuungana na kocha wa zamani wa AS Vita na timu ya taifa ya DR Congo, Ibenge ambaye alivutiwa naye. Chama anatajwa kutokuwa na furaha huko Morocco na yote hiyo inatokana na kutokuwa chaguo la kwanza la Ibenge kwenye kikosi chake. Mbali na Chama ambaye muda wowote anaweza kurejea Simba hawa hapa

NEW VIDEO: Rosa Ree Feat. Abby Chams - Mulla

Image
  Rosa Ree Feat. Abby Chams - Mulla Tazama Hapa: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3pwTJig via IFTTT

Mwanamuziki Barnaba Amjibu Eric Omondi "Bongo FLAVA Ina Nguvu Kuliko Amapiano"

Image
"Nadhani Bado Bongo Flavor Ina nguvu Sana kuliko Amapino Kingine lazima Watu wajue Amapiano SIO aina Ya muziki Bali kwa lugha Rahisi Ni mixing Za Dj’s wa SouthAfrica WAKIWA Kwenye Gigis zao So haitaweza Kuuwa muziki halisi kama zook Rhumba Rege / Dans Pop Rock NK : kwasababu SIO haina Ya muziki Bali ni vionjo tu katika milindimo ya mziki ✊🏿💥💥 BONGO FLAVOR BACK 2022 : tena To the maximum Kwa Duania ✊🏿💥💥'' from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3z2zqMO via IFTTT

Job Ndugai "Kuna Siku Nchi Hii Itapigwa Mnada"

Image
  Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema tozo za miamala ya simu zilipitishwa ili nchi iweze kutekeleza miradi yenyewe, badala ya kutegemea mikopo ambayo imekuza deni la Taifa kufikia TZS trilioni 70. Amesisitiza haiwezekani miaka 60 baada ya uhuru nchi bado iwe ya kutembeza bakuli. “Kipi bora, sisi Watanzania kuzidi kukopa na madeni au tubanane banana hapahapa tujenge wenyewe bila madeni haya makubwa makubwa yasiyoeleweka, ni lini sisi tutafanya wenyewe and how? “Tutembeze bakuli, ndiyo heshima kisha tukishakopa tunapiga makofi…, kuna siku nchi itapigwa mnada hii,” Spika wa Bunge, Job Ndugai from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/314WQol via IFTTT

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo 28 Dec 2021

Image
  Job Opportunity at Dangote Cement, Executive Assistant For The Country Manager/ CEO Job Opportunity at African Trade Insurance Agency, Chief Risk Officer (CRO) Job Opportunity at Bulyanhulu Gold Mine, Process Plant Operators Job Opportunity at MUHAS, Assistant Nurse / Clinical Assistant Job Opportunity at Appen Tanzania, Appen Work From Home Opportunities Job Opportunity at Vodacom, SME Sales Lead from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3sG3woe via IFTTT

TANZIA: Mwanamuziki Defao Afariki Dunia

Image
Mwanamuziki na mtunzi wa nyimbo kutokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Defao Matumona amefariki dunia. “Bwana ametoa,Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe” from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3JnUORp via IFTTT

Siri Wanawake Kuwa ‘Single’ yafichuka

Image
“Sasa niko ‘single’ naenjoy, mwenzenu niko ‘single’ naenjoy, bora niko single naenjoy. Nikitaka kwenda kidimbwi, naenda naparty mpaka asubuhi halafu siulizwi.” Hicho ni kibwagizo cha wimbo unaofanya vizuri kwa sasa kutoka kwa msanii Lavalava akieleza furaha yake ya kuishi bila mwenza. Mbali na kibwagizo hicho, msanii Saraphina kwenye wimbo alioshirikishwa na The Baddest ameimba, “Oooh tuacheni utani, ‘single’ ni amani, hata nichelewe kurudi... na tukiwa na party popote nakwenda, kutoana roho kisa penzi haifai mwenzenu niko ‘single’ jamani napenda.” Nyimbo zote mbili zinafanya vizuri kwa sasa kwenye vituo vya redio, runinga na chati mbalimbali za muziki kwa kuwa zinabeba ujumbe unaoelezea hali halisi inayoendelea kwenye jamii kwa sasa. Kuna watu ambao wamekata tamaa ya kuwa na wenza au kupitia maumivu mbalimbali yanayowafanya waamini kuishi bila kuwa kwenye uhusiano ndiyo kitu salama zaidi kwao. Licha ya kuwa suala hili liko kwa pande zote mbili, wanawake ndio wanaoonekana

Huu Hapa Uhalifu Mkubwa Uliowahi Kutokea Duniani na Kuishangaza Dunia...Opera Heist

Image
Kuna wakati unaweza kujiuliza wezi wamewaza nini, kisha kuja na mpango flani wa uvamizi. Kwa sababu mtu anapanga tukio la wizi mpaka unabaki kujiuliza huyu ni binadamu mwenzetu kweli au ametoka sayari nyingine? Hili ni kutokana na akili kubwa iliyotumika katika upangaji wa matukio mpaka wizi wenyewe! Na ndicho kilichotokea kwenye wizi huu. Opera house ni jengo kubwa la kifahari huko jijini Mumbai nchini India, ambapo ndani yake kuna duka la kuuzia vito vya thamani kama mikufu, bangili, pete, madini n.k. ndani ya jengo kwenye duka hilo ndiko kulikofanyika wizi wa akili kubwa ambao ulishangaza dunia nzima na kubaki kuwa moja ya wizi uliotumia ustadi wa hali ya juu kabisa, nah ii ni kuanzia mipango hadi kuvamia ndani ya Opera house. Wizi huu haukuhitaji washirika wa kupanga namna ya kuvamia na kuiba, kwani mpangaji wa wizi huu hakuwa na haja ya kufanya hivyo ila akaamua kufanya peke yake na bila kutumia silaha ya aina yoyote ile. Mkurugenzi mtendaji mstaafu wa Central Bureau of I

Rais Samia asamehe wafungwa 5,704

Image
RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa msamaha kwa wafungwa 5,704, katika kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wa Tanzania Bara. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea). Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 27 Desemba 2021 na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam. “Rais Samia kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45 (1) (d) ya Katiba, ametoa msamaha kwa wafungwa 5.704 kwa masharti,” amesema Simbachawene. Hata hivyo, Simbachawene amesema Seriksli inaweka utaratibu wa kufuatilia mienendo ya wafungwa watakaosamehewa na ikibainika wamerudia tena kujihusisha na makosa ya jinai, watarudishwa tena gerezani.   “Kumuachia mfungwa kama ameonesha tabia njema hatuwezi acha. Tutaweka utaratibu wa kuwafuatilia ambao wanajihusisha na makosa ya jinai, ili kabla hawajafanya makosa zaidi tuwarudishe gerezani,” amesema Simbachawene. Simbachawene ametaja masharti ya kyachwa huru wafungwa ikiwemo,

Davido Kuanza Mwaka na Collabo Kubwa na Drake, Athibitisha Kwa Kupigiana Video Call

Image
Mwanamuziki nyota kutoka Nigeria @davido amethibitisha uwepo /ujio wa collabo yake na rapper kutoka canada #Drake mwakani 2022. Kupitia insta story yake Davido ameshare sehemu ya video akiwa anazungumza na rapper huyo kupitia video call na kusindikiza na ujumbe unao ashiria uwepo wa collabo baina yao ifikapo mwaka 2022. Kama collabo hiyo itafanikiwa basi Davido atakua msanii wa pili mkubwa kutoka Nigeria kufanya kazi na #Drake ,nyuma ya #WizKid ambae tayari amekwisha fanya nae kazi miaka kadhaa nyuma kwenye nyimbo kama 'Closer & One dance' from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3zaaOlu via IFTTT

Askofu Shoo ataka haki vyombo vya dola

Image
  Moshi. Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Fredrick Shoo, amevitaka vyombo vya dola wakiwamo mahakimu na majaji kutenda haki na kuepuka kuwaonea na kuwatesa wengine kwa kufikiri Mungu haoni. Askofu Shoo aliyasema hayo  wakati akitoa ujumbe wa Krismasi kwenye ibada iliyofanyika katika Usharika wa Moshi mjini akivitaka vyombo na dola kuacha vitendo vyote vya hila vinavyosababisha maumivu kwa wengine. Katika ujumbe wake huo, Askofu Shoo alivitaka vyombo hvyo kuwatendea haki wananchi. “Ni wito wangu kwa wazazi, walezi, vyombo vya dola, mahakimu na majaji niwaombe tendeni haki acheni kuwaonea watu, acheni kuwatesa wengine kwa hila mkifikiri Mungu haoni,”alisema Askofu Shoo ambaye pia ni mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini. Kwa mujibu wa Askofu Shoo, Mungu anaona kilio na huzuni kutoka kwa wale wote wanaoonewa na kwamba anao uwezo na nguvu za kubadilisha machungu na huzuni zao kuwa furaha na furaha za wale wanaowatesa na kuwaonea kuwa huzuni. “Tuache na ku