Posts

Showing posts from June, 2022

Alichokisema Mpole baada ya kumfunika Mayele

Image
Mpole amemaliza na mabao 17 na assisti tatu katika michezo 30 ya Ligi Kuu ya NBC msimu huu. Mwanza. MSHAMBULIAJI wa Geita Gold, George Mpole ameibuka kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2021/2022 baada ya kufunga mabao 17 katika michezo 30. Mpole amejihakikishia nafasi hiyo baada ya kutupia bao muhimu leo katika mchezo wa mwisho timu yake ikimaliza kwa sare ya 1-1 dhidi ya Coastal Union ya Tanga huku mpinzani wake wa karibu, Fiston Mayele wa Yanga aliyemaliza na mabao 16 akishindwa kucheka na nyavu leo wakati mabingwa hao wa Ligi wakiichapa Mtibwa Sugar 1-0. Akizungumza baada ya mchezo huo ambao umepigwa uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Mpole amesema wakati msimu unaanza alijiwekea malengo ya kuwa mfungaji bora hivyo kutimia kwa jambo hilo ni mafanikio makubwa huku akishukuru Mungu kwa kumuepusha na majeraha. "Najiskia vizuri ni kitu ambacho nilikiwekea malengo na ilikuwa ni ndoto yangu tangu naanza mechi yangu ya kwanza ya Ligi nilijiwekea kuwa mfun

Mombasa: Makahaba Waongeza Bei Kutokana na Hali Ngumu ya Kiuchumi

Image
Makahaba hao walisema kuwa kupanda kwa bei za bidhaa za msingi nchini kumewafanya kuongeza bei kwa huduma zinazotolewa Bei hizo mpya zitaanza kutekelezwa Alhamisi, Juni 30 na tayari wamewapa wateja wao notisi ya siku 3 siku ya Jumatatu Kupitia shirika la kutetea haki yao, wameombwa kuzingatia kwa dhati bei mpya zilizowekwa, na iwapo watakiuka watachukuliwa hatua za kinidhamu Wafanyabiashara ya ngono kutoka kaunti ya Mombasa wametoa wito kwa wateja wao kuchimba zaidi mifukoni mwao ili kufurahia huduma zao kutokana na hali mbaya ya kiuchumi inayoshuhudiwa nchini. Mombasa: Makahaba Waongeza Bei Kutokana na Hali Ngumu ya Kiuchumi. Mombasa: Makahaba Waongeza Bei Kutokana na Hali Ngumu ya Kiuchumi. Picha: UGC. Shirika la kutetea haki za wafanyabiashara ya ngono Nkoko Injuu Africa (NGO), kupitia kwa mratibu wake Lucy Kiragu, ilisema kuwa kupanda kwa bei za bidhaa za msingi nchini kumewafanya kuongeza bei kwa huduma zinazotolewa. Nkoko Injuu lina zaidi ya wanachama 4000 waliosajil

Breaking: Rais Samia ateua Mkuu wa Majeshi mpya, mrithi wa Mabeyo

Image
Ni June 29, 2022 ambapo Rais Samia amempandisha cheo Meja Jenerali Jacob John Mkunda kuwa Jenerali na amemteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ( Chief of Defence Forces- CDF). from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/FAQTuvj via IFTTT

Kesi ya kina Mdee kusikilizwa siku 14 mfululizo

Image
HATIMA ya endapo Halima Mdee na wenzake 18 wataendelea kusalia kuwa wabunge itajulikana ndani ya siku 14 za usikilizaji wa shauri namba 27 la mwaka 2022. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea). Shauri hilo linalosikilizwa na Jaji Mustapha Ismail katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam limefunguliwa na Halima Mdee na wenzake 18 dhidi ya Bodi ya wadhamini ya Chadema, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Halima na wenzake wanapinga kuvuliwa uanachama wa chama hicho mara baada ya Baraza Kuu la chama hicho kubariki uamuzi wa Kamati Kuu ya kuwafukuza uanachama kwa makosa ya usaliti. Leo Alhamisi tarehe 29 Juni, 2022, Mahakama hiyo imetoa kibali kwa wajibu maombi wote kuwasilisha viapo kinzani kesho Alhamisi tarehe 30 Juni, 2022 tayari kwa kuanza kusikiliza shauri hilo.   Hatua hiyo imejiri baada ya Kibatala kuiomba Mahakama hiyo kuondosha mapingamizi waliyowasilisha awali ili kupisha usikilizwaji wa shauri hilo kwa kuwa limefunguliwa

Rais Samia kuhudhuria Tamasha hili, RC aomba Wananchi

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye Tamasha la Utamaduni la kwanza kitaifa na Siku ya Kiswahili Duniani linalotaraji kuanza July 01-07 Jijini humo na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan. Akizungumza na Waandishi wa habari, RC Makalla amesema Tamasha Hilo litazinduliwa Julai 02 na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kwenye Uwanja wa Uhuru likihusisha Matembezi ya Utamaduni, Maonyesho ya vyakula vya asili na ngoma za asili. Aidha RC Makalla amesema Julai 03 kutakuwa na Usiku wa Taarabu katika ufukwe wa Coco Beach ukihusisha burudani ya Mziki mwanana kutoka kwa wasanii mbalimbali akiwemo Khadija Kopa, Isha Mashauzi, Patricia Hilary, Mzee Yusuph na wasanii na vikundi ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson. Hata hivyo RC Makalla amesema Julai 04 Kutakuwa na maandamano ya Amani kuhusu Lugha ya Kiswahili na Utoaji haki kutoka Temeke mwisho mpaka Uwanja wa Uhu

George Mpole Mfungaji Bora Ligi Kuu Tanzania...Mayele Chali

Image
Kwa misimu miwili mfululuzo vijana wazawa wananyakua kiatu cha mfungaji bora. Bocco 16, Mpole 17. Fantastic Job kwa wazawa from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3CtL8TI via IFTTT

Ndege Kutoka Nje Zaongezeka Kutua Tanzania..Royal Tour Yajibu

Image
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Zuhura Yunus pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Waziri wa Nishati, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda pamoja na Viongozi Wakuu wa Taasisi za Serikali leo wamezungumza na Vyombo vya Habari kuhusu ziara ya Rais Samia nchini Oman pamoja na matokeo ya Filamu ya The Royal Tour katika ukumbi wa Jakaya Kikwete, Ikulu Dar es salaam leo June 28,2022. Miongoni mwa yaliyosemwa ni ongezeko la Watalii na Ndege za Mashirika mbalimbali nchini baada ya Royal Tour “Baada ya Royal Tour Watalii wameongezeka na Wawekezaji wameongezeka sana, Watu wa Viwanja vya Ndege wanaangalia miruko ya ndege, kwa vipimo vyao inaonedha miruko imeongezeka na Wageni wanaofika Uwanja wa Dar es salaam wameongezeka” “Ndege zinazofika nchini baada ya Royal Tour kwa taarifa ni kwamba Mashirika mengi yameongeza sana ndege zinazokuja, Fly Dubai zilikuwa ndege 10 sasa ndege 14 , Oman Air zilikuwa ndege mbili sasa ndege 7 kwa Wiki,

Kocha Mpya Simba na rekodi ya mataji barani Afrika

Image
KLABU ya Simba siku ya jana ilimtambulisha Zoran Maki Manojlovi, raia wa Serbia kuwa kocha wao mkuu ambaye anakuja kurithi mikoba ya Pablo Franco Martin ambaye alitimuliwa kwenye klabu hiyo kufutai matokeo mabovu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea) Kocha huyo amepewa mkataba wa mwaka mmoja, ambaye atajiunga na timu hiyo katika maandalizi ya msimu mpya wa mashindano 2022/23, ambao unatarajia kuanza Tarehe 17 Agosti 2022. Zoran ni moja ya kocha mwenye uzoefu na soka la bara Afrika, mara baada ya kuhudumu ndani ya mabara hili katika kipindi cha miaka 10 na kupata mafanikio tofauti. Ikukumbukwe kabla ya mchakato kuanza wa kumtafuta kocha ndani ya klabu ya Simba, uongozi wa timu hiyo uliweka bayana kuwa kocha watakayemuhitaji ni yule ambaye analijua vizuri soka la abarani Afrika. Mafaniko makubwa ya kocha huyo ndani ya bara Afrika, alifanikiwa kutwaa taji la Ligi Kuu nchini Angola msimu wa 2018/19, akiwa na klabu ya De Agosto ambayo pia alifanikiwa kuifikisha hatua ya nusu faina

BABU Sefu Ni Mkombozi wa Kitiba za Asili Wengi Wamefanikiwa..Wasiliana nae Mweleze Tatizo Lako

Image
  BABU SEFU Ni mkombozi wa kitiba wengi wamefanikiwa  Mnakalibishwa wote wenye matatizo mbali mbali ya kidunia   USIKATE TAMAA WAHI SASA Je? (1)umeachwa au kutelekezwa na mme/mke au mchumba mludishe sasa ndani ya masaa 4 tu ataludi na kuomba msamaha (2)Mvuto wa mapenzi na biashara (3)Unateseka mardhi sugu? (3)Unafeli katika masomo yako (4)Kuludishwa kazini Migogoro kazini na kupata kazi  (5)Kushinda kesi (6)Dawa za Nguvu za kiume Kurefusha na kunenepesha uume kwa saiz uitakayo  (7)Dawa za Kuongeza hipsi na makalio Miguu pamoja kuondoa Mabaka Chunusi na Michilizi (8)Zindiko la mwili Nyumba na mashamba KWA HAYO NA MENGINE MENGI USISITE Kumuona πŸ’₯  BABU SEFU πŸ’₯πŸ’₯ Piga sim 0769111403 POPOTE ULIPO HUDUMA ITAKUFIKIA from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/VWmO9iZ via IFTTT

Rasmi Tanzania Mwenyeji Tuzo Za (MAMA) MTV AFRICA Music Award 2023

Image
  Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa amekutana na kufanya mazungumzo na makamu wa Rais na meneja mkuu wa Paramount Africa and Peer Lead BET International, Monde Twala,  na kukubaliana kushirikiana katika kuiwezesha Tanzania kuwa mwenyeji wa tuzo za MAMA- MTV Africa Music Award kwa mwaka 2023.   Waziri Mchengerwa amekutana na Monde Twala Jijini Los Angeles   katika jimbo la California nchini Marekani wakati wa hafla ya utoaji tuzo za BET kwa mwaka 2022.   Katika mazungumzo hayo Waziri Mchengerwa amemwelezea nia na sababu ya Tanzania kutaka kuwa mwenyeji wa tamasha hilo la utoaji wa tuzo hizo kubwa za burudani kwa Afrika, kuwa ni kuongeza ushawishi kwa vijana wa kitanzania kuendelea kufanya vizuri katika sekta za burudani Pamoja na kuitangaza zaidi Tanzania na uzuri wake katika ulimwengu.   Katika mazungumzo hayo pande zote mbili zimekubaliana  kuungana kwenye kutafuta washirika katika kuendesha tuzo hizo, na kuridhia kuwa maandalizi yaanze mara moja,

Breaking Huyu Hapa Mwamba Ndio Kocha Mpya wa Simba

Image
Jana Jumanne (Juni 28) Simba SC imemtambulisha Zoran Maki raia wa ureno kwa mkataba wa mwaka mmoja ambaye amekuja kuchukuwa nafasi ya Pablo Franco alie ondoshwa klabuni hapo kwa kushindwa kufikia malengo alio pewa na Viongozi wa Simba Zoran Maki akiwa kocha wa Simba SC anatakiwa kuchukuwa ubingwa wa NBC Premier league na kuifikisha timu nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika ndiyo malengo aliyo wekewa na uongozi wa Simba Lakini Je! Viongozi wametimiza Mambo ya kuweza kufanikisha kocha kutimiza malengo hayo walio mpatia tena kwa mwaka mmoja ambao ni muda mfupi sana leo hii Klabu kama Real Madrid, Al Ahly, Manchester United zinafukuza makocha kwa sababu Viongozi wanatimiza majukumu yao kwa kumpatia kila kitu kocha ndy maana wanawafukuza Viongozi wa Simba SC wanatakiwa kufanya sajili Bora za wachezaji, Preseason Bora, Kambi Bora ya wachezaji, Benchi zuri la Ufundi na kumpa ushirikiano mzuri kocha ili aweze kufanikisha malengo walio muwekea na sio kusubiri maajabu NB: Usa

Orodha ya majina ya waliopata ajira kada za Afya na Ualimu TAMISEMI

Image
OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) imetangaza majina 16,676 ya watumishi wapya waliopangiwa vituo vya kazi katika Sekta ya Elimu na Afya nchini. Orodha hiyo inatokana na waombaji wenye sifa waliokidhi vigezo baada ya Aprili, 2022 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kutoa kibali cha ajira kwa kada za Ualimu na Afya, kwa ajili ya kuajiri walimu 9,800 wa shule za msingi na sekondari na wataalam wa afya 7,612 Bonyeza Link Hizi Zifuatazo Kusoma Majina: TAMISEMI:Majina ya Walimu Walioajiriwa | List of Newly Employed Teachers 2022 TAMISEMI- Majina Ya Walioajiriwa Kada ya Afya | List of Newly Employed Health Sector 2022 from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/NoqYUAG via IFTTT

Soma Habari Kubwa Zilizopo Katika Magazeti ya Leo June 29

Image
  Soma Habari Kubwa Zilizopo Katika Magazeti ya Leo June 29 from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/mOlN5PD via IFTTT

Wahamiaji 46 Wapoteza Maisha Kwenye Lori Marekani

Image
Watu wapatao 46, wamekutwa wamefariki wakiwa kwenye lori liliotelekezwa katika mitaa San Antonio, Texas. Afisa mmoja wa zimamoto amesema watu 16, wakiwemo watoto wanne, pia wamepelekwa hospitali kwa matibabu zaidi. San Antonio ambayo ipo kilometa 250, kutoka mpaka wa Marekani na Mexico, ambayo ni njia kuu ya kusafirishia watu. Wasafirishaji haramu wa binadamu mara nyingi hutumia lori, kuwasafirisha wahamiaji wasio na vibali baada ya kukutana nao kutoka maeneo mbali mbali, mara baada ya kufanikiwa kuvuka na kuingia Marekani. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/nrPQy7l via IFTTT

Kutana na Miujiza ya Mtaalam Bahati Kutoka Morogoro, Mtaalam wa Tiba Asilia na Maombezi ya Dua

Image
KUTANA NA MIUJIZA YA MTAALAM BAHATI KUTOKA MOROGORO MTAALAM WA TIBA ASILI TANZANIA NA DUNIANI KOTE (Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU MTAALAM BAHATI KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: MTAALAM BAHATI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, πŸ”₯anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na majini, πŸ”₯Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, πŸ”₯nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, πŸ”₯anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa pete za bahati, zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, πŸ”₯pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA SIMU NO: +255 719 626 586 WhatsApp no:

Mume aoa wake zake wawili kwa siku moja

Image
Kijana wa miaka 22 Mustapha Ado ame-make headlines kwenye baadhi ya vyombo vya habari nchini Nigeria baada ya kufunga ndoa na wake zake wawili kwa siku moja. Picha za Mustapha akiwa na wake zake wawili wakiwa wanafunga ndoa zimeweza kwenda viral mitandaoni kwa watu kushangazwa na tukio hilo la aina yake. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/rjAu2zC via IFTTT

Mmoja afa ajalini gari ikiteketea kwa moto

Image
Mbeya. Mtu mmoja amefariki dunia na wengine kunusurika katika ajali baada ya roli  lililobeba  shehena za mizigo likielekea mkoani Dar  es Salaam  kuferi breki na  kugonga magari  manne na kisha kuwaka moto katika  mtelemko wa barabara kuu ya Mbeya-Iringa eneo la Pipe line Wilaya ya Mbeya Vijijini. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ,Urlich Matei amesema ajali hiyo imetokea leo Jumatatu June 27, 2022 saa 12 asubuhi. Amesema ajali hiyo ilihusisha roli la mizigo  likiwa linaendeshwa na Erick Ndasigwa (39) mkazi wa  Dar es Salaam  lilifeli breki na kisha kugonga magari manne likiwepo gari ndogo ambayo  dereva wake alipoteza maisha akiwa ndani ya gari. Matei ametaja watu walionusurika katika ajali ani madereva akiwemo  aliyesababisha ajali , Erick Ntasigwa, Yunus Amos, Philimon Bartazali  na Abdafik Mohammed (29) mkazi wa jijini Mbeya na dereva wa Shirika Water Reed Tanzania   Matei amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mtelemko mkali uliopo kwenye eneo ilipotokea ajali Matei a

Serengeti Girls kundi moja na Ufaransa

Image
Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limepanga makundi ya Fainali za Kombe la Dunia kwa Wasichana chini ya umri wa miaka 17. Fainali hizo zitazopangwa nchini India baadae mwaka huu, zitashuhudia Tanzania ikishiriki kwa mara ya kwanza ikitokea Barani Afrika. Timu ya taifa ya Tanzania chini ya miaka 17 (Serengeti Girls) imepangwa Kundi D na timu za Ufaransa, Canada na Japan. Timu nyingine kutoka Afrika zitakazoshiriki Fainali hizo ni Morocco iliyopangwa Kundi A na Nigeria iliyoangukia Kundi C.   Fainali hizo zimepangwa kuanza kuunguruma Oktoba 11 hadi 30. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/z5LVSUN via IFTTT

Hii ndo Gharama ya Kuleta basi la Ubingwa la Yanga kwa Siku Moja

Image
Moja kati ya vivutio katika sherehe za Ubingwa wa Yanga ni pamoja na basi la wazi ambalo wamelikodi kutokea Uganda kuja Tanzania katika parade ya Ubingwa na watu wengi wamekua wakitamani kujua gharama za kuleta basi hilo nchini kwa siku ni kiasi gani, Dereva wa basi hilo katika mahojiano na Ayo TV amefafanua kuwa, kwa makadirio, kukodi basi hilo ni kiasi cha dola elfu moja kwa siku ambayo ni zaidi ya Milioni mbili na laki moja tatu za kitanzania. Amesema, matumizi ya basi hilo kwa Uganda ni pamoja na Kufanya tour za mjini na za shule, sherehe mbali mbali zikiwemo harusi, za kuzaliwa na hata mikutano vyote vinafanyika ndani ya basi. Dereva huyo amefafanua kuwa aliwahi kuja Tanzania kama abiria, lakini kuja na gari hiyo kwa shughuli hizo za mpira kwake ni mara ya kwanza na amesema jambo hilo ni zuri sana na hajawahi kuona kwao Uganda. “Ni jambo zuri sana, aina ya Mashabiki na sapoti wanayotoa kwa timu kama hivi, sijawahi kuona,” Alisema dereva huyo. from UDAKU SPECIAL https

Collabo ya Diamond Platnumz na Ney wa Mitego Haitawahi Tokea Tena

Image
  Kuna 'kolabo' nyingi. Lakini ya Ney na Mondi ya "Muziki", inabaki kuwa bora kwa miaka 10 hii. Undava wa Ney na 'ulaini' wa Mondi. Umezalisha kitu tofauti chenye sanaa kubwa. Ney akiigiza nunda, Mondi akicheza 'sini' inayofanya Ney aonekane hana facts. NEY Muziki wenu ushirikina, ndo umetawala, Q-Chillah analalama, anasema umemroga, Mganga wako aliyekutoa, umemkimbia hujamlipa, Bila skendo za magazeti, basi husikiki... DIAMOND Ah, mi ni mti wenye matunda, milele siogopi kupigwa mawe, Ubaya wenu wengi "kayumba", elimu mlitupa sadakalawe... Ney na porojo za ushirikina kwenye 'gemu'. Zinajibiwa kikatili, kwa lugha laini na sauti 'bembelevu'. Ni kama Mondi kamchoresha Ney kuwa hayo ni mawazo ya waliokimbia umande. Kwamba ukosefu wa elimu hufanya watu waamini mafanikio huletwa na uchawi. NEY Bado hujanishawishi, Bongo Fleva inanipa kichefuchefu, Kwanza nyie malimbukeni wa umarufu, Mnaleta maringo mpaka kwa mashabiki,

Mwijaku 'Mganga wa Kajala ni Wakweli Kaharibu Ubingwa wa Yanga"

Image
Jana, kupitia ukurasa wa Instagram @mwijaku amepost post picha na kuandika, "Tukubaliane kua Harmonize kaharibu ubigwa wa Yanga. Sioni kelele wala nderemo, au mganga wa kajala ni wa kweli sio muongo? Au ubigwa ni wa magumashi? Hehehe." Vipi ni kweli ubingwa wa Yanga umefunikwa na Konde boy? from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/UefQN4c via IFTTT

Mwanamuziki Nandy Afurahishwa na Tukio la Harmonize na Kajala..Afunguka Haya

Image
Mwanamuziki @officialnandy ameonyesha kufurahishwa na tukio la #harmonize na #kajala Jana kuvishana pete usiku wa jana. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, amewapongeza wawili hao na kuandika "AaaaaawπŸ₯° love birds! hongereni sana kwa hatua impendezayo Mungu na mkawe na furaha milele." from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/6hNa4jg via IFTTT

Alikiba: Pesa Zinatosha Ndugu Zangu wa Kahama, Acheni Nipafomu Kwanza

Image
Alikiba akiimba jukwaani Kahama mkoani Shinyanga Staa wa Bongo Fleva, Alikiba usiku wa kuamkia leo amefanya bonge moja la shoo katika Mji wa Kahama mkoani Shinyanga katika sherehe ya kutimiza mwaka mmoja kwa kiwanja maarufu cha burudani katika mji huo cha The Magic 101. Vibe la mashabiki kumtuza staa huyo lilikuwa kubwa kiasi cha mwenyewe kunyoosha mikono na kusema: “Pesa zimetosha ndugu zangu wa Kahama, acheni nipafomu.” Licha ya Alikiba kuwataka mashabiki wasiendelee kumtuza, bado waliendelea kumiminika jukwaani na kumpa fedha pamoja na kupiga naye picha, wakionesha furaha waliyokuwa nayo kwa staa huyo kufanya shoo katika kiwanja hicho cha kipekee na cha kisasa cha burudani katika Mji wa Kahama from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/Arf1yQI via IFTTT

Mwanamuziki wa Nigeria Osinachi Hatimaye Azikwa Mumewe Akikosa Kuhudhuria

Image
Mwanamuziki wa Nigeria Osinachi Hatimaye Azikwa Mumewe Akikosa Kuhudhuria Mwanamuziki Osinachi Nwachukwu alizikuwa alikozaliwa bila uwepo wa mumewe.  Mazishi hayo yalifanyika Isochi Umunneochi, mji ambao alizaliwa, bila uwepo wa mumewe ambaye anazuiliwa rumande kwa tuhuma za dhulma za nyumbani na kusababisha kifo cha msanii huyo, japo amezidi kukana. Mtoto wa kwanza wa Osinachi, alisema kuwa baba yao Peter Nwachukwu, alikuwa akiwaambia kuwa kuwapiga na kuwatesa wanawake ni sehemu ya maisha.   Kwa mujibu wa mtoto huyo baba yao alizoea kumpiga marehemu hata kwa ugomvi mdogo tu na kwa wakati mmoja alimsukuma nje ya gari wakiwa safarini na kumwamuru arudi nyumbani. Mumewe Osinachi kuendelea kuwa rumande Kifo cha Osinachi kilichochea hasira kubwa ndani na nje ya Nigeria baada ya familia yake kudai kuwa alikuwa mwathiriwa wa dhulma za kindoa. Mwaka 2017, Marehemu aliimba wimbo wa Injili uliovuma sana kwa jina Ekweume ambao umetazamwa mara milioni 77 kwenye mtandao wa vi

Watu 18 Wamefariki Wakijaribu Kuvuka Kuingia Uhispania

Image
Wahamiaji 18 wamefariki na wengine kujeruhiwa wakati umati mkubwa ulipojaribu kuvuka eneo la Melilla nchini Uhispania Kaskazini, maafisa kutoka nchi jirani ya Morocco wanasema. Ripoti zinasema baadhi ya waliofariki walikuwa wameanguka kutoka juu ya uzio wa mpaka. Maafisa kadhaa wa usalama na wahamiaji wamelazwa hospitalini kwa matibabu kufuatia makabiliano mapema siku ya Ijumaa. Ilikuwa ni mara ya kwanza kushuhudiwa kwa majaribio kama haya ya kuvuka kwa wingi tangu Uhispania na Moroko kuanza tena uhusiano wa kidiplomasia mnamo Machi. Kushuka kwa mahusiano kulikuja baada ya Uhispania kuunga mkono mpango wa kujitawala wa Morocco kwa eneo linalozozaniwa la Sahara Magharibi. Maafisa wa Uhispania wanasema mamia ya watu walijaribu kupenya ndani ya eneo hilo baada ya kukata uzio. Wengi walilazimishwa kurudi lakini zaidi ya 100 walifanikiwa na walikuwa wakishughulikiwa katika kituo cha mapokezi, waliongeza. Melilla na Ceuta, eneo jingine la Uhispania, katika miaka ya hivi ka

Somo la Historia ya Tanzania Kuanza Mwakani

Image
Somo la Historia ya Tanzania kama somo linalojitegemea litaanza kufundishwa katika shule za msingi na sekondari Januari mwakani. Maandalizi ya somo hilo kuanza kufundishwa kama somo linalojitegemea yamekamilika kama alivyoagiza Rais wa awamu ya tano, John Magufuli kwamba lianze kufundishwa kama somo linalojitegemea. Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omari Kipanga alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chumbuni, Ussi Salum Pondeza (CCM). Pondeza alitaka kujua ni lini somo hilo la historia litaanza kufundishwa kama Rais John Magufuli alivyoagiza lianze kufundishwa kama somo linalojitegemea shuleni. Kuhusu swali la nyongeza la lini mitaala ya elimu iliyoboreshwa itaanza kutumika kufundishia, Kipanga alisema mitaala hiyo mipya imekamilika na itaanza kutumika Januari mwakani. Kipanga alisema kinachofanyika sasa ni kufanya maandalizi ya vifaa vinavyotakiwa kutumika katika kufundisha kwa kutumia mitaala hiyo mipya ya elimu. Pondeza pia alitaka

Barua ya Profesa Shivji kwa Rais Samia

Image
  Kwa heshima na taadhima pokea barua yangu nikikutumia kwa nia njema na katika kutekeleza wajibu wangu kama mwananchi na mwanazuoni kwa mujibu wa Ibara 26 ya Katiba “kuhakikisha hifadhi ya Katiba na sheria za nchi.” Awali ya yote nakutakia maisha marefu yenye afya njema na furaha tele ili uendelea kutuongoza kwa busara na hekima na kwa kulinda Katiba yetu bila hofu au upendeleo. Katika sakata la Loliondo na Ngorongoro nimesikia mara kwa mara Waheshemiwa Mawaziri husika wakitamka Bungeni kwamba ardhi yote nchini ni mali ya umma na hakuna mwenye ardhi. Kwa heshima, kwa maoni yangu, tafsiri hiyo ya sheria sio sahihi. Ni kweli kwamba Sheria ya Ardhi inasema ardhi yote nchini ni ‘public lands’ yaani ardhi ya kiumma na imewekwa mkononi mwa Rais kama mdhamini kwa niaba ya wananchi.  Kifungu 4, kifungu kidogo 1,  cha Sheria ya Ardhi 1999 (sura 113) kina tamka kwamba ardhi yote nchini Tanzania itaendelea kuwa ardhi ya kiumma na itaendelea kuwa mkononi mwa Rais kama mdhamini kwa nia

Paula akimpongeza Mama yake baada ya kuvalishwa pete ya uchumba

Image
Wengi walidhani binti huyo hajaridhia Mama yake @kajalafrida kurudiana na @harmonize_tz kutokana na mgogoro uliojitokeza na kupelekea wawili hao kuachana. Mastaa mbalimbali wamewapongeza wawili hao kwa hatua hiyo. from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/NT9427v via IFTTT

Breaking News: Harmonize Amvalisha Pete ya Uchumba Kajala Masanja

Image
Tayari wawili hao wameshavalishana pete za uchumba na kinachofuata ni ndoa ambayo bado haijajulikana ni lini. Kajala Masanja ni mkristo huku mpenzi wake Rajabu aka Harmonize akiwa ni muislam. Leo muda mchache baada ya kuvalishana pete, Harmonize alionekana akitumia ishara ya msalaba hali ambayo imezaa maswali mengi kwamba atakuwa amebadili dini kumfuata Kajala. Una mazamo gani kutokana na hiyo video hapo chini? from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/9QjO0ZW via IFTTT

Maneno Kuntu ya Mwijaku Baada ya Harmonize Kumvisha Pete Kajala Masanja

Image
FACT-Mwenyezi MUNGU anayotabia ya kuwatumia wale watu ambao wamekataliwa. MUNGU anayo tabia ya kuwabariki wale watu ambao wamedharauliwa, kuumizwa na kufedheheshwa. MUNGU anayotabia ya kuwainua, kuwapa hadhi na kuwaheshimisha wale walioumizwa vibaya. Hufanya hivyo makusudi kabisa, ili tu, pale utakapofanikiwa, asiinuke mtu awaye yote na kusema kwamba, bila yeye wewe usingekuwepo hapo ulipo. Mwenyezi MUNGU atakubariki ule wakati ambapo hakuna hata mmoja anaesimama na wewe kukusaidia. Ili tu, pale utakapofanikiwa mtu awaye yote asiinuke na kusema mimi nilikusaidia mpaka kufanikiwa. Endapo mtu ataanzisha vita na wewe, endapo mtu atakuumiza, kukufedhehesha na kushushia heshima, hebu furahi maana hiyo ni dalili tosha kwamba, MUNGU ameamua kukubariki. Sijui ni yepi unayoyapitia, ila elewa kwamba, kwa yote yanayokuumiza muda huu hebu kuwa na furaha, wala usioneshe huzuni. Usiwape ushindi wa mezani. Kilima uzuri mbali, karibu kina majuto. You are a candidate for God's next bl

Mwigulu Nchemba "Hatuwezi Kuacha Kukopa Kuogopa Deni Kuwa Kubwa"

Image
  Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema haiwezekani kuacha kukopa kwa kuogopa deni kuwa kubwa, mikopo ya Serikali ni kwa ajili ya Maendeleo ya Miradi mikubwa ya Nchi na siyo ya kulipia Mishahara au Matumizi ya kawaida Amesema Deni la Serikali kwa sasa uwiano wake na Pato la Taifa ni 31% wakati ukomo ni 55%, Deni la Nje kwa Uwiano wa Pato la Taifa ni 18% wakati ukomo wake ni 40%, Deni la Nje kwa mauziano ya nje ni 142% ukomo ni 180% Waziri ameongeza "Tunafurahia 4G na 5G lakini Mkongo wetu wa Taifa ni deni, miradi ya aina hiyo ni mingi. Mradi ukishakopewa hauwezi kusimama, fedha zinapoingia ndivyo deni linavyokua. Mfano kuna madeni nimesaini yalipwe ambayo yalikopwa kabla sijazaliwa" from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/UV56W38 via IFTTT

Mchezaji Cristiano Ronaldo Afikiria Kuondoka Manchester United..Kisa na Mkasa Huu Hapa

Image
  Cristiano Ronaldo anafikiria kuondoka Manchester United ikiwa timu hiyo haitafanya usajili mzuri katika dirisha la sasa Ronaldo ambaye alirejea klabuni hapo mwaka 2021 baada ya kuondoka miaka 13 iliyopita kwenda Real Madrid yupo tayari kubaki ikiwa usajili kwa ajili ya msimu ujao utakuwa mzuri Aidha, Bayern Munich ambao wanahusishwa kutaka kumsajili wamesema hawana mpango na Ronaldo ambaye msimu uliopita alifunga mabao 24 katika mechi 38 from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/DxNZCmP via IFTTT

ESMA PLATNUMZ akata simu baada ya kusikia jina la ZUCHU, Je kuna UGOMVI? afanyiwa hili la kushtusha

Image
  ESMA PLATNUMZ akata simu baada ya kusikia jina la ZUCHU, Je kuna UGOMVI? afanyiwa hili la kushtusha VIDEO: from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/2FJ1wHj via IFTTT

Mchezaji Mwafrika Anayelipwa Zaidi Kuliko Wote

Image
Sadio Mane anakuwa mchezaji wa Kiafrika anayelipwa zaidi baada ya kujiunga na Bayern Munich. 1.Sadio Mane πŸ‡ΈπŸ‡³ (£250,000 sawa na Tsh 714.9m kwa Wiki) 2.Mohamed Salah πŸ‡ͺπŸ‡¬ (£220,000 sawa Tsh 629.1m kwa wiki) 3. Riyad Mahrez πŸ‡©πŸ‡Ώ (£200K sawa na Tsh.571m kwa wiki). from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/WkT0ILH via IFTTT