Posts

Showing posts from December, 2020

Haji Manara Atoa MPYA "Hivi Nikiondoka SIMBA Namuachia Nani Ukubwa wa Jina Langu Unaniponza?

Image
Mkuu wa Idaya ya Habari na Mawasilino Simba SC, @hajismanara amewajibu baadhi ya wadau wa soka nchini ambao wamekua wakimtabiria mabaya kuhusu kazi zake ndani ya klabu hiyo. #Manara ametuma majibu hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram, kufuatia madai yaliyotolewa na baadhi ya wadau hao wakisema amesimamishwa kazi, huku akitakiwa kutozungumza lolote kuhusu Simba SC. #Manara ameeleza kuwa, bado yupo Simba SC, na ataendelea kufanya kazi zake kama kawaida, huku akiwatuliza mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kongwe katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. “Please Please Please (Tafadhali) Wanasimba mimi Haji wenu bado nipo nanyi na nitaendelea kuwa msemaji wenu hadi pale riziki yangu itakapokwisha, (Hatatokea mmoja wetu kubaki milele iwe kwa kifo au vinginevyo). “Waambieni wenye kuandika tetesi za kuondoka kwangu, mimi mtu dhaifu lakini ni mjuzi mno katika mambo ya mawasiliano ya umma na nina uzoefu mkubwa katika eneo hili na nishakuwa sugu na changamoto za kazi.” “Hala

Stori Fupi ya Mchezaji Christian Ronaldo "Nilimwambia Baba Yangu Nataka Kuwa Kama Michael Jackson"

Image
Anasimulia Kwamba ALIPOKUWA mdogo mwenye Umri wa Miaka 7 alikuwa anaongea na Baba Yake mzazi na kumwambia Baba nataka siku Moja nije kuwa na nyumba kubwa ya thamani kama Mtaalamu Michael Jackson.Baba akamwangalia Mwanaye na akamwambia kwamba Mwanangu ndoto Ni ndoto tu hilo swali haliwezekani Mwanangu maana ndoto Ni ndoto tu Mambo makubwa ni ya Watu wenye pesa tu Mwanangu. Lakini CR7 anasimulia ya kwamba leo hii Nina miliki majumba na Nina maisha mazuri lakini Cha kushangaza Ni kwamba Baba yangu hayupo tenaa alikwishaaga Duniaa. Cr7 anatamani baba yakee angekuwepo Ili aone mafanikio yakee hii leo lakini baba yakee hayupo na wala hajashuhudia mafanikio hayo. Never give up🤞 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3n3rR0A via IFTTT

Yasemekana Ali Kiba Aachana na Mkewe Tena Kisa Play Station 5

Image
  Inasemekana Ndoa Imeingia Nzi Kisa PS5 na Marafiki watoto. Mwana DSM hit Maker @officialalikiba na Mkewe wametengana tena. Chanzo PS5. Habari zinasema Alikiba ana marafiki watoto sana na anapenda kucheza PS5 hamsaidii mkewe kazi na Pia kingine Nyumba anayoishi ina watu sana bado wanaendelea kuenda. Pia inasemekana Amina Keshasepa kwenda zake Mombasa @divamediaafrica inatafuta balance ya story Hii ya Mwanamuziki Nguli wa Muziki wa Bongofleva na ambae Ni Kipenzi cha watu. Hivi karibuni Alikiba ameachia ngoma mpya toka africa kusini na inasemakana 2021 ataacha muziki na kununua Private jet iwe inampeleka sehemu za tour yake na mapumziko Yake from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2JANNTm via IFTTT

Muuaji hatari katika historia ya Marekani, Samuel Little afariki Dunia

Image
Samuel Little, mtu aliyetajwa na shirika la kijasusi la FBI kama muuaji mkubwa wa kuvizia katika historia ya Marekani amefariki akiwa na umri wa miaka 80. Samuel Little, most prolific serial killer in U.S. history, dies Little alifariki katika hospitali mjini California siku ya Jumatano, idara ya magereza imesema. Alikuwa akihudumia kifungo cha mauaji ya wanawake watatu Lakini kabla ya kifo chake , alikuwa amekiri kuwauawa wanawake 93 kati ya mwaka 1970 na 2005. Little aliwalenga watu waliokuwa hawawezi kujitetea, wengi wao wakiwa makahaba ama watumiaji wa mihadarati , walisema maafisa. Little alikuwa akiuwa bila kuwacha ishara zozote za mauaji, kama vile kuwadunga kisu ama kuwapiga risasi na kwamba mtu huyo alikuwa ameuawa. Badala yake vifo vyake vingi alivyo uwa vilidaiwa kula dawa kupitia kiasi ama vya ajali na havikuchunguzwa. Baadhi ya miili haijapatikana , kitengo hicho kilisema. Mwaka uliopita FBI lilisema kwamba wachambuzi wake walisema kwamba madai yote alioki

Ridhiwani Kikwete Ampa Shavu Harmonize, Ataja Wimbo wa Jeshi Ndio Wimbo Wake Pendwa

Image
Tumebakiza siku chache tuumalize mwaka 2020 na tuingie 2021, kama ilivyo kwa Rais mstaafu wa Marekani, Barack Obama ambaye hutoa orodha ya ngoma kali zaidi kwake kila mwaka kuelekea mwisho wa mwaka, sasa Mbunge wa jimbo la Chalinze, Mh. Ridhiwani Kikwete yeye anaitaja #Jeshi ya @harmonize_tz kama wimbo wake pendwa mwaka 2020. Wimbo Jeshi (Video) ambao unafanya vizuri YouTube, tangu video hiyo ipandishwe Agosti 11 mwaka huu, umemkosha vilivyo Mh. Ridhiwani 2020. Kupitia Instagram, Mh. @ridhiwani_kikwete amepost video ya wimbo wa "Jeshi" na kuandika, "Kuna nyimbo zinakuwa na hisia fulani hata unapokuwa unaoga unasikia inaimba kichwani. That Number toka kwa Konde Boy inakuwa katika list ya Nyimbo hizo". Mheshimiwa #Ridhiwani anaungana na maelfu ya mashabiki mtaani kuipokea Jeshi kama wimbo bora from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2WWZ4Az via IFTTT

Wimbo mpya wa HARMONIZE "Wapo" watafsiriwa kama majibu kwa DIAMOND, Mashairi yake ni utata mtupu

Image
Wimbo mpya wa HARMONIZE "Wapo" watafsiriwa kama majibu kwa DIAMOND, Mashairi yake ni utata mtupu VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/34Y4iAk via IFTTT

Wachezaji Watano Simba SC Kutolewa kwa Mkopo

Image
  Uongozi wa klabu ya Simba SC kupitia kwa Afisa Mtendaji Mkuu wake Barbara Gonzalez amethibitisha kuwatoa baadhi ya wachezaji kwa mkopo ili kukuza uwezo wao, baada ya kukosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Mabingwa hao watetezi wa VPL.   Wachezaji ambao huenda wakatolewa kwa mkopo ni kiungo Ibrahim Ajibu, mshambuliaji Miraji Athumani, mlinzi Kennedy Wilson Juma, Ibrahim Ame na mshambuliaji Charles Ilanfya ambao wawili hao huu ni msimu wao wa kwanza klabuni hapo. Washambuliaji Miraji Athumani, Charles Ilanya na mlinzi Ibrahim Ame wanahusishwa kwenda kukipiga kwenye klabu ya Ihefu ya jijini Mbeya, ikiwa ndiyo klabu pekee inayoripotiwa kuuandikia uongozi wa Simba kuomba uwezekano wa kuwatumia wachezaji hao kwa mkopo. Klabu ya Ihefu ambayo ni ya pili kutoka mwisho kwenye msimamo wa VPL imedhamiria kubaki ligi kuu msimu huu, kwani tayari wamewasajili kipa Deogratius Munisi, washambuliaji Juma Mahadhi kutoka Yanga na kiungo Joseph Mahundi na Andrew Simchimba kutoka Azam FC. K

Mripuko katika uwanja wa ndege wa Yemen wauwa watu 26

Image
Karibu watu ishirini na sita wameuwawa baada ya miripuko katika uwanja wa ndege wa Aden huko Yemen muda mchache baada ya maafisa wa serikali mpya ya Yemen kuwasili nchini humo.  Duru za serikali na kimatibabu zimeliambia shirika la habari la Ufaransa AFP kuwa ingawa hakuna afisa yoyote wa serikali aliyeathirika zaidi ya watu hamsini wamejeruhiwa.  Kipindi moshi ulipokuwa unafuka kutoka uwanja huo wa ndege huku watu wakikimbia kuwanusuru waliojeruhiwa, kulisikika mripuko wa pili.  Ukanda wa video wa shirika la habari la AFP umeonyesha kile kilichoonekana kuwa kombora lililoulenga uwanja huo wa ndege.  Baadhi ya maafisa wamewalaumu waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran kwa shambulizi hilo. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3ofo4Pa via IFTTT

Mange Kimambi Amshukia Jux Tena Baada ya Vanessa Mdee Kuvalishwa Pete na Rotimii, Amwita Mlamba Lipsi

Image
From @mangekimambi_ OMG, my pare sister is engaged!!!! Congrats babe @vanessamdee so happy for you and @rotimi. Ladies you see, pale unapoachana na walamba midomo wanaume wa maana wanakuja. Mwanaume analamba lips asubuhi mpaka jioni, kuna mume kweli hapo? Just be patient, msikimbilie kulea wanaume, wa maana watakuja na utaolewa asipokuja basi hukuandikiwa ndoa.Sio kila ndoa mwanamke anastirika, ndoa zingine wewe mwanamke unakuwa unamstiri mwanaume. Huku ndo kustirika sasa. Yani Vanessa kastirika kisawasawa, vile inavyotakiwa yani....Hapana chezea wapare wewe. I’m so happy for you Vee. Yani you leveled up kama utani, duh!! from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2LbtUm1 via IFTTT

Mama Diamond Akata Mzizi wa FITINA, Amweka Zari Namba Moja Anaefaa Kuolewa na Mondi

Image
  Mama Dangote Bi Sandra azidi kumkubali Zari kuwa anafaa kuolewa na Mwanae Diamond... Mama Dangote kavunja ukimya na kuandika Ujumbe kuwa " HAKUNA MWINGINE" Yaani zari ndio Top Manyota from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3n2k5nN via IFTTT

JPM Alivyotimiza Ndoto ya Baba wa Taifa

Image
  Oktoba 12, 2019, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, alitangaza rasmi kuhamia jijini Dodoma, wakati alipokuwa akijiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga kura yeye na mke wake Mama Janeth, katika kijiji cha Chamwino mkoani Dodoma. Kushoto ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli, na kulia ni Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere. Rais Dkt. Magufuli, alitoa amri ya serikali kuhamia Dodoma mwezi Julai 2016, wakati alipopewa wadhifa wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), zoezi ambalo lilichukua safari ya zaidi ya miaka 40 iliyopita. Kitendo cha Rais Dkt. Magufuli, kuamua kuihamishia serikali makao makuu ya nchi jijini Dodoma, ilikuwa ni kama ndoto ambayo ilikuwa ikingojewa kutimia kwa muda mrefu, kwani Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ndiyo ilikuwa ndoto yake kubwa ya kuihamishia serikali kwenye Makao Makuu ya nchi. Dodoma ilitangazwa kuwa Mji Mkuu wa Tanzania mwaka 1973, lakini mnamo Aprili 26, 2018, kat

Dkt. Ndugulile Azipa Siku 30 Taasisi Za Umma Zinazodaiwa Na TTCL Kulipa Madeni

Image
  Na Prisca Ulomi, WMTH Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile amezipa siku 30 taasisi za umma zinazodaiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kulipa madeni kwa Shirika hilo ili liweze kujiendesha, kutekeleza majukumu yake ya kutoa huduma ya mawasiliano ya sauti na data kwa taasisi za Serikali, sekta binafsi na wananchi ili kukuza uchumi na kuchangia pato la taifa Dkt. Ndugulile ameyasema hayo wakati wa ziara yake alipotembelea TTCL kwa lengo la kufahamiana na kuzungumza na wajumbe wa Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wa TTCL, Dar es Salaam ambapo aliambatana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo A. Mathew na Mejimenti ya Wizara hiyo Ameongeza kuwa zaidi ya taasisi 20 za Serikali zinadaiwa na TTCL zaidi ya kiasi cha shilingi bilioni 30 ambapo zipo taasisi zinatumia huduma za mawasiliano za TTCL na zinakusanya mapato ya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa mwezi ila hawako tayari kulipa huduma za TTCL Vile vile, ametoa onyo kali kwa

Maskini Diamond Platnumz Afunguka HAYA Kuhusu Wasanii Wanaomwimba Vibaya

Image
  Nyota wa muziki nchini na bara la Afrika kwa ujumla, msanii Nasib Abdul @diamondplatnumz amesema hawezi kukasirika anaposikia wasanii wengine wanamuimba katika nyimbo zao kwa mabaya au mazuri. Akizungumza na Wasafi TV, #Diamond amesema hilo linatokana na nguvu kubwa ya ushawishi aliopewa na Mungu hivyo hawezi kuchukia. “Ni baraka namshukuru Mwenyenzi Mungu, hutakiwi kuchukia, Mungu amenipa nguvu kubwa ya ushawishi, kwa hiyo sitakiwi kununa. Wao ni binadamu wanatafuta riziki kupitia mimi, sasa nikinunua nakuwa namkasirikia kwanini kanipa huu ukubwa,” amesema. Ameendelea kusema kuwa kuna wasanii wengi wapo mtaani wangetamani kupata nafasi hiyo lakini wameikosa, hata ile ya kuzungumziwa. Kwa sasa nyota huyo, ambaye pia ni boss wa lebo ya @wcb_wasafi anafanya vizuri na wimbo wake "Waah" ambao amemshirikisha Koffi Olomide kutokea DR Congo. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2MnOpgb via IFTTT

Nini Amchokoza Mke Mwenzake Kwa Nay Wa Mitego

Image
  Msanii Official Nini amesema kwa sasa hayupo tena kwenye mahusiano na boss wake Nay wa Mitego, ila huwa ana-post picha akiwa naye kwa sababu hutaka kumrusha roho mwanamke mpya wa Nay wa Mitego.   Official Nini ambaye yupo chini ya lebo ya 'Free Nation' inayomilikiwa na Nay Wa Mitego amesema mapenzi yao yameisha muda mrefu sana na kwa sasa kinachoendela ni kumsimamia kwenye upande wa kazi. "Ile picha ilikuwa ni ya muda mrefu nilijisikia tu kumchokoza wifi, mimi sina mke mwenzangu maana naogopa nisije nikaribu ndoa za watu, yule wa sasa hivi ni wifi yangu kwa boss wangu siku nikikutana naye nitamwambia ampende sana boss wangu hicho ndicho kikubwa" amesema Nini  from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2Me5VTS via IFTTT

Kajala Masanja Akata Tamaa Kuzaa TENA, Kisa Kizima Hichi Hapa

Image
  MASKINI! Mkali wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja ameweka wazi kuwa kutokana na umri alionao wa miaka 38, ameshakata tamaa ya kuzaa mtoto mwingine tena hivyo atabaki na mwanaye Paula tu. Kajala aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, kipindi cha nyuma alikuwa akisaka mtoto mno, lakini ilishindikana hivyo umri unasogea na pia mtoto wake ameshakua ni msichana mkubwa hivyo inabidi aangalie maisha mengine na siyo kuzaa tena. “Nilitamani sana kupata hata watoto wawili, lakini ilishindikana kwa wakati, hivyo nimeona bora sasa kuangalia kitu kingine mbele maana nimekata tamaa kabisa ya kuongeza mtoto mwingine, ninajikita kwenye kumuwezeshe Paula asonge mbele kielimu,” alisema Kajala kwa masikitiko. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/34SGC0f via IFTTT

Tazama Askari Alivyomuokoa Mtoto Kwenye SHIMO la Choo "Alimfuata Mama Yake Chooni"

Image
Tazama Askari Alivyomuokoa Mtoto Kwenye SHIMO la Choo "Alimfuata Mama Yake Chooni" Tazama VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3hxfrNn via IFTTT

Mange Kimambi amchana Shilole kuhusu mpenzi wake mpya, adai Rommy analelewa, Shishi ajibu mapigo

Image
Mange Kimambi amchana Shilole kuhusu mpenzi wake mpya, adai Rommy analelewa, Shishi ajibu mapigo VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3aUs3gv via IFTTT

CORONA: Hadithi ya Mapambano isiyoisha Utamu

Image
  Machi 16, 2020, Tanzania ilithibitisha kisa cha kwanza cha mgonjwa wa Corona, taarifa ambayo ilitolewa na Waziri wa Afya wa wakati huo Ummy Mwalimu, ambaye alisema kuwa mgonjwa ni mwanamke raia wa Tanzania aliyewasili nchini Machi 15 kupitia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanajaro.  Taarifa ya Waziri Ummy, ilieleza kuwa mgonjwa huyo aliwasili na ndege ya shirika la Rwanda akitokea nchini Ubelgiji, ikiwa ni moja ya Taifa ambalo lilikuwa limeathirika na virusi hivyo kwa kiasi kikubwa. Mara baada ya mgonjwa wa kwanza kuthibitika nchini, Machi 17, 2020, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alitangaza kufunga shule kwa muda wa siku 30, pamoja na kuzuia mikusanyiko mbalimbali ikiwemo matamasha na michezo, mikutano mbalimbali ikiwemo ya shughuli za kisiasa, jambo ambalo lilikuwa ni kama tahadhari za kujikinga na kusambaa kwa maambukizi ya virusi hivyo. Mbali na serikali kuchukua hatua hizo, Serikali pia ilijipanga kwa uhakika kwa kuweka mazingira ya kukabiliana na ugonjwa huo ikiwemo

Mrembo SANCHI baada ya kubadili DINI aonesha uwezo wake wa kusoma QURAN, Inapendeza

Image
Mrembo SANCHI baada ya kubadili DINI aonesha uwezo wake wa kusoma QURAN, Inapendeza VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3mXPuId via IFTTT

Ngoma ya ALIKIBA na DJ-SBU yapiga VIEWS 1M ndani ya saa 24, Mashabiki waonyesha kupagawa

Image
Ngoma ya ALIKIBA na DJ-SBU yapiga VIEWS 1M ndani ya saa 24, Mashabiki waonyesha kupagawa VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2JvWxtO via IFTTT

Onyo Watakaochoma Matairi Mwaka Mpya

Image
  Jeshi la Polisi nchini limepiga marufuku uchomaji wa matairi ambayo yamekuwa yakiharibu miundombinu mingi kama vile barabara ambazo zimejengwa kwa gharama kubwa pamoja na kuleta kero kwa raia wema.   Taarifa ya Kamishna wa Polisi, Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu CP Benedict Wakulyamba iliyetolewa kwa niaba ya Inspekta Jenerali wa Polisi imepiga marufuku uchomaji wa matairi  sambamba na Disko toto kote nchini na imelekezwa kuwa watoto washerehekee chini ya uangalizi wa wazazi au walezi. Jeshi la polisi limewataka wananchi watakao kuwa wamekusanyika katika fukwe za bahari na maziwa  kwa ajili ya kusherehekea sikukuu kurejea majumbani mwao mara ifikapo saa kumi na mbili jioni. Aidha Jeshi la Polisi limesema limejipanga vizuri kuhakikisha  hali ya ulinzi na usalama inaimarishwa  kwa kiwango kikubwa kwa kuelekeza  makamanda  wa Mikoa  kuimarisha ulinzi kwenye nyumba za ibada na maeneo mengine ambayo wananchi watakusanyika huku likitoa wito kwa kila mtanzania kutii sheri

Fahamu Kwa Undani Aliyoyaacha Mama Rwakatare

Image
  Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto Assemblies of God,  Askofu Dkt. Gertrude Rwakatare, alifariki dunia Alfajiri ya Aprili 20, 2020, katika hospitali ya Rabininsia iliyopo jijini Dar es Salaam baada ya kuugua maradhi ya moyo. Taarifa ya kifo cha Mama Rwakatare ilitolewa mapema na mwanaye wa kiume Mutta Rwakatare, alipozungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio, taarifa ambayo baadaye pia ilitolewa na Spika wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai. Mama Rwakatare alizaliwa Desemba 31, 1950, huko Ifakara mkoani Morogoro, na alisoma Shule ya Msingi Ifakara, akajiunga na Sekondari ya Korogwe hadi kidato cha sita na baadaye alijiunga na Chuo cha North London Polytechnic nchini Uingereza na baadaye pia alijiunga na Chuo cha Eastern and Southern Africa Management Institute alikopata shahada ya kwanza ya mawasiliano ya umma. Aidha marehemu Mama Rwakatare pia alijiunga na chuo kikuu cha kikristo cha Moody, na safari yake ya kielimu h

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi Disemba 31

Image
  Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi Disemba 31 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3pD96Tz via IFTTT

Ujerumani yarekodi vifo 1,129 vya COVID-19 ndani ya saa 24

Image
Ujerumani imerekodi vifo 1,129 kutokana na virusi vya corona ndani ya saa 24 zilizopita.Idadi hiyo ya juu zaidi kuwahi kurekodiwa Ujerumani ni kwa mujibu wa takwimu kutoka katika taasisi ya kupambana na magonjwa ya kuambukiza ya Ujerumani Robert Koch mapema leo. Aidha kwa mujibu wa data za Robert Koch, jumla ya maambukizi mapya 22,459 pia yamerekodiwaKatika wiki za hivi karibuni, Ujerumani imeimarisha vikwazo vya kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona, ikiwa ni pamoja na kufunga maduka na shule, kuhimiza watu kuvaa barakoa, kutosogeleana na kuepusha mikusanyiko ya watu. Uingereza pia imerekodi idadi ya juu zaidi ya maambukizi ya virusi hivyo. Serikali ya nchi hiyo imetangaza kuwa jumla ya maambukizi 53,135 mapya yamerekodiwa ndani ya saa 24 zilizopita.Hayo yakijiri, Uingereza imetangaza kuidhinisha matumizi ya chanjo ya pili ya COVID-19, iliyotengenezwa na kampuni ya nchi hiyo AstraZeneca kwa ushirikiano na chuo kikuu cha Oxford. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2KMkQEw

Miti ni yetu na ni Dawa Toka Enzi na Enzi..Onana na Doctor Jimwenda Aweze Kukusaidia Matatizo yako

Image
DOCTOR JIMWENDA MITI NI YETU NA NI DAWA TANGU ENZI NA ENZI UKIAMINI NA NIA KWA MALAZI YANAYO KUSUMBUA ONANA NA MIMI NIWEZE KUKUSHAULI JINSI YA KUTATUA TATIZO LAKO NAPATIKANA DAR ES SALAAM KAMA UPO MIKOANI DAWA ZITAKUFIKIA KWA NJIA YA USAFIRI AINA ZA DAWA HEGA MIX POWER-hii ni dawa inayotibu nguvu za kiume kwa vijana na wakina baba wenye upungufu wa kutofika kileleni, kuwahi kuchelewa,na kukuza maumbile DOZI SIKU 6 MWITYA MITI 18 MIX-hii ni dawa inayotibu uzazi, chango kwa kina mama walio na matatizo ya kuto pata watoto DOZI SIKU 14 natatizo kuisha kabisa MITI 7 MIX -inatibu ngiri, tezi dume bila operation kwa mda mfupi dozi siku 9 LYELA -ni dawa inayotibu kisukari cha kupanda nakushuka dozi siku 19-20 Tumbo kujaa gesi na kuunguria uvimbe ktk tumbo kupata choo ngumu dozi siku 7 KWA MAWASILIANO PIGA SIMU NAMBA CALL TO 0736 171 773 WHAT SAAP 255 783 969 338 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2WJ4vCU via IFTTT

Mwanaume Fanya Hivi ili Mkeo Akuone Mtenda Miujiza Kila Siku..Hakika Hatasikia la Mtu...

Image
Hili ni fundisho kwa vijana wengi ambao wanataabika, suala la fedha limekuwa mwiba mkubwa na chanzo kikubwa cha mahusiano na ndoa kuyumba. Nimelazimika nije na ushauri huu ambao utawasaidia vijana wa kileo ambao wanataabika na ndoa hususani suala la fedha. Kinachowaumiza vijana wengi katika fedha na wenza wao ni tabia ya wanaume kuwa wazi kwa kutoa taarifa za pato lake kamili. Jambo la uwazi ni jema lakini muwe na kiasi kwani usipokuwa na akiba ya 'taarifa za kipato chako' utakosa fusra ya kufanya miujiza pale mambo yanapokwama. Fanya hivi. Mfano kipato chako ni shilingi milioni moja kwa mwezi, mweleze kwamba unapokea shilingi laki 7 na hizo tatu hakikisha unaweka katika sehemu salama ambayo hata ikitokea umekufa familia yako itafaidika, mfano benki kila unapochukua mshahara hakikisha unaacha laki tatu kama akiba asiyoijua. Sasa katika hii laki saba panga matumizi pamoja na akiba ya pamoja. Wanawake wanapenda 'mshtuko/suprise'..so siku ya siku ukiona kanuna unamt

Ni Kweli Wivu wa Mapenzi ndio Chanzo cha Mauaji?

Image
Kufuatia kukithiri kwa matukio ya mauaji na ukatili wa aina mabalimbali  ambayo yanahusishwa na wivu wa mapenzi nchini athari za kisaikolojia zimetajwa kuwa ni moja ya sababu inayopelekea watu kufanya matukio ya ukatili. Akizungumza katikia kipindi cha Supa Breakfast,  Mwanasaikolijia, Alexedes Kamugisha amesema kuwa mapenzi peke yake sio sababu ya moja kwa moja inayopelekea mtu kufanya matukio ya kikatili bali namna  mtu ameathirika kiundani hupelekea kufanya matukio hayo. “Kisababishi cha watu kufanya matukio ya ukatili ni kutokana na namna wanavyoathirika kisaikolojia kutokana na tofauti zinazotengenezwa na haiba ya mtu ambapo moja wapo ni kuwa na hali ya kughadhabika, kukosa hali ya kuelewa hisia za wengine” amesema Kamugisha Aidha kwa upande wa namna ya kusaidia kuiepusha jamii na matatizo hayo, Kamugisha ametaka malezi katika ngazi ya familia kwa watoto yapewe kipaumbele ili kuepusha matatizo ya kisaikolojia. “Malezi yapewe kipaumbele kuhakikisha tofauti za mama na bab

Huyu Mwanamke Ndio wa Kuoa ila Sijui Kama Anapatikana Tanzania.......

Image
1. Mpenzi wako akija kwako na akakakuta unakula ugali na kachumbari na akaamua kula nawe..huyo muoe.... 2.ukienda nae hotelini akaamua kuagiza ugali dagaa na maji tu...muoe anajua uchumi. 3.Mdada ambaye akimuona mkaka mwingine anaendesha Land cruiser na wewe una vitz yako Number A lakini akaamua kuja kwako...usimuache... 4.Mwanamke akikutembelea kwako akakuta nguo zako chafu akafua zote mpaka za wadogo zako, huyo mke usimuache! 5. Mwanamke unampa sh elfu tano akafanye shopping sokoni anakurudishia chenchi..huyo usimuache...anajua kubana bajeti na muaminifu. 6. Ukimpata mwanamke ambaye anakupigia simu na kukuuliza kama anaweza kukutumia credit au hela ya lunch, au anakupa pocket money saa nyingine, huyo tangaza ndoa fastaaa! 7.Mwanamke ambae anakupa password ya benki,laptop, simu na emails zake, huyo ni zaidi ya malaika.oa haraka..watamgombania wenzako! 8.Ukipata mwanamke ambaye mkipanda daldala analipa nauli au mkitoka out analipia bill ya chakula na vinywaji...huyo usi

KISA Cha Kusikitisha 'Baba Yangu Alisababisha Nilale na Mjomba Wangu, Kamwe Sitamsamehe'

Image
Nimeona leo nitoe siri yangu hapa ya muda mrefu ambayo imekuwa ikiniumiza sana pale tu ninapokumbuka, nakosa raha na amani inapotea. Kwa ufupi kabisa, nilizaliwa mkoani Mara wilaya ya Musoma mjini maeneo ya Nyakato, mama yangu alibeba mimba yangu akiwa darasa sita hivyo hakumaliza shule. Ilibidi akae nyumbani mpaka pale alipojifungua, kwa wakati kulikuwa hakuna sheria kali kwa wanaowapatia wanafunzi mimba wakiwa shule. Na aliyempatia hiyo mimba naye alikuwa mwanafunzi mwenzake lkn alikuwa la saba yeye alimaliza shule. Baba yake mama ambaye ni babu yangu alikuwa na uwezo mkubwa hivyo hakushindwa kutulea mimi na mama. Nikiwa na miaka 6 ndipo nilipokuja kumjua baba yangu wakati huo nae alikuwa amekuwa mtu mzima, alikuja akanisalimia akaondoka, kwao pia walikuwa vizuri kimaisha. Nikiwa na miaka 9 naanza darasa la kwanza wakati huo tulikuwa tunaingia shule tukiwa na umri mkubwa tofauti na sasa. Mama aliolewa na mume mwingine na alikuwa ni askari jeshi, alifanikiwa kuzaa nae watoto wa

Wasiliana na Dr Cheif Mihambo, Mtaalam wa Tiba Asili na Visomo

Image
DR CHEIF MIHAMBO NI MTAARAM WA TIBA ASILI ANATATUA TATIZO LAKO POPOTE ULIPO DUNIAN KWA KUTUMIA MITI SHAMBA NA KISOMO HABAGUI DINI KUTANA AU WASILIANA NA CHEIF MIHAMBO ANAPATIKANA MOROGORO NA DAR ES SALAAM NA KANDA YA ZIWA MATATIZO ANAYOTATUA 1,zindiko la nyumba 2, nyota 3, unataka kumipiki mali magari makampuni 4, migogoro ya ndoa 5, kupata mke/mme takiri 6, Kupata kazi nzuri 7 , kupandisha cheo kazini 8, pete za bahati 9, kurudisha mali zilizopotea au kuibiwa 10, wateja kwenye biashara 11,kutajirika ndani ya wiki 2 12, kumrudisha, kumfunga, kumpata mke/ mme,mchumba 13, kukomesha wachawi/ wezi /majambazi NA MATATIZO MENGINE MFANO MAGONJWA YOYOTE YANAYO KUSUMBUA HAYASHINDIKANI KWANGU KWA MAWASILIANO PIGA SIMU NAMBA CALL 0714 289 910 WHAT SAAP+255 658 171 773 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/34H3wr5 via IFTTT

MO Dewji atoa ya moyoni “sitamvumilia anenivunjia heshima”

Image
Mfanyabiashara na Mwekezaji wa Klabu ya Simba, Bilionea Mohammed Dewji ‘Mo’ amesema mwaka 2021 hatowavumilia wale wote wanaotoa lugha za matusi na kumvunjia heshima. MO ametoa onyo hilo jana kupitia ujumbe wake mrefu wa kufunga mwaka 2020 aliouchapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram. “Azimio langu kwa mwaka ujao humu mtandaoni ni kutovumilia wale wenye lugha za matusi na kunivunjia heshima mimi binafsi, nitalazimika, japo kwa shingo upande na moyo mzito sana, kuwa-block, ku-report na ikibidi, kuchukua hatua za kisheria. Naamini kutumia lugha ya matusi na kudhalilisha dhidi ya mtu katika hadhara si ustaarabu wetu Watanzania, si maadili ya dini zetu na si uungwana pia” MO dewji “Sote tuna maisha nje ya mtandaoni. Wengi wetu ni wazazi, tunao pia wazazi, wategemezi na watu wengine muhimu kwetu ambao tunawaheshimu, wanatuheshimu na wana matarajio juu yetu, haipendezi kuwakwaza na kuwaumiza hao wanaotuthamini na kutuheshimu kwa figisu za maisha yetu ya mtandaoni” MO Dewji  “Nachu

Ajibu, Sheva Waugomea Uongozi Simba

Image
JUMLA ya wachezaji watano wa Simba wamegoma kutolewa kwa mkopo kwenda kucheza katika klabu nyingine zilizoomba barua za kuwahitaji nyota hao katika usajili huu wa dirisha dogo.   Wachezaji wanaotajwa kutolewa kwa mkopo ni Kennedy Juma, Miraji Athumani ‘Sheva’, Charles Ilanfya, Ibrahim Ame na Ibrahim Ajibu ambao wamekosa nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.   Simba imepanga kuwatoa wachezaji hao kwa mkopo baada ya Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mbelgiji Sven Vandenbroeck, kupendekeza nyota hao kutolewa ili wakalinde vipaji vyao baada ya kukosa nafasi. Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatano, wachezaji hao wamegoma kutolewa kwa mkopo kwa kuhofia kutelekezwa na timu hiyo.Mtoa taarifa huyo aliwataja baadhi ya wachezaji waliogoma kutolewa kwa mkopo ni Kennedy, Ajibu, Sheva huku Ame akionekana kuwatega viongozi wengine wakipendekeza abakie hapo. Aliongeza kuwa wachezaji waliobakishwa wakiwa katika hatua za mwisho za kutaka kutolewa kwa mkopo ni kiungo F

Ishu Siyo Kilevi, Sababu ya Mkude Kuondolewa Simba SC Iko Hivi

Image
KIUNGO wa Simba Jonas Mkude juzi alitangazwa kuondolewa kwenye kikosi cha timu hiyo kutokana na utovu wa nidhamu.   Mkude amekuwa akikumbana na rungu la utovu wa nidhamu mara kwa mara kwenye kikosi cha Simba na sasa uongozi wa timu hiyo umeamua kumsimamisha.   Simba hawajaweka wazi sababu za kumuondoa kiungo huyo, ingawa chanzo cha ndani kinasema kuwa amefanya mfululizo wa makosa, huku ikidaiwa kuwa anafanya makusudi.   Chanzo hicho kimesema kuwa awali ilikuwa inaelezwa kuwa chanzo cha utovu huo wa nidhamu ni utumiaji wa kileo, lakini siyo kweli bali mara zote amekuwa mzima kabisa wakati anafanya matukio hayo.   “Kwanza amekuwa akichelewa mazoezini makusudi, lakini wakati mwingine amekuwa ananuna tu bila sababu zozote.“Kwa wiki mbili nafikiri amechelewa mara tatu na hana majibu sahihi kila anapoulizwa, sasa hata kama mtu unataka kuondoka au una ishu yako basi ipeleke kwa uongozi,” kiliseme chanzo chetu.   Inaelezwa kuwa kiungo huyo hatakuwepo kwenye mchezo dhidi

Ramaphosa Aja na Masharti Mapya Kudhibiti Corona

Image
RAISwa Afrika ya Kusini, Cyril Ramaphosa, amesema hali ya maambukizi nchini humo ni mbaya sana, hivyo serikali ya nchi hiyo imerejesha masharti mbalimbali yanayolenga kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona katika ambayo imeathirika zaidi barani Afrika.   Hatua hiyo inakuja ikiwa ni siku moja tangu nchi hiyo itangazwe kuwa nchi ya kwanza Afrika kufikisha visa 1,004,413 huku 26,735 wakipoteza maisha tangu kutangazwa kwa mlipuko wa virusi hivyo Machi, 2020.   Masharti yaliyotolewa ni pamoja na wananchi kutotoka nje kuanzia saa 3:00 usiku hadi saa 12:00 asubuhi bila kibali.  Mauzo ya pombe pia yamezuiwa, ambapo migahawa na maduka yatafungwa saa 2:00 usiku.   Pia watu wote wametakiwa kuvaa barakoa kila wanapokuwa katika maeneo ya umma na watakaokiuka agizo hilo watatozwa faini au kufungwa jela.   Hivi karibuni mamlaka nchini humo zilitangaza kuwepo kwa virusi vipya vya corona vinavyosambaa kwa haraka, hali iliyopelekea hospitali kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa.  

Askari shujaa Koplo Denis Minja aokoa mtoto mwingine chooni

Image
Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Koplo Denis Minja, ambaye mwezi Mei alimwokoa mtoto mchanga akiwa hai ndani ya shimo la choo wilayani Ngara mkoani Kagera, amemwokoa tena mtoto mwingine wa kiume mwenye umri wa miaka 2, kutoka katika shimo la choo, eneo la Kayanga wilayani Karagwe. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kagera, Hamis Dawa, amesema kuwa walipata taarifa za mtoto kutumbukia katika choo cha shimo wakati akimfuata mama yake aliyekuwa bafuni akioga na kwenda kumuokoa na kufanikiwa kumtoa akiwa hai na kwa sasa anaendelea vizuri. Amesema Askari huyo Koplo Minja, ambaye alishirikiana na Askari wenzake na kuingia katika shimo hilo kumwokoa mtoto huyo, kituo chake cha kazi ni wilaya ya Ngara lakini yuko wilayani Karagwe kumuuguza mke wake. Dawa amesema kuwa tukio hilo limetokea Desemba 28 mwaka huu, saa 10:00 jioni, na kutaja Askari wengine wa zimamoto walioshiriki kuokoa maisha ya mtoto huyo kuwa ni Norbert Saka, Eliad B