Posts

Showing posts from January, 2021

Mkataba wa Messi wavuja, Barca wageuka mbogo

Image
Barcelona imesema kuwa itachukua “hatua za kisheria” dhidi ya gazeti la Uhispania la El Mundo baada ya kuchapisha maelezo kuhusu mkataba wa mshambuliaji, Lionel Messi wa pauni milioni 492. Barcelona vs Bayern Munich: End Of An Era As Barca Humiliation Makes  Revolution The Only Option | Football News Barcelona ilikanusha kuhusika kwa namna yoyote ile katika uchapishaji wa taarifa hizo. Kwa mujibu wa El Mundo, mkataba wa Messi wa miaka minne ulikuwa wa thamani ya takriban euro 555,237,619 hadi Juni 30, 2021. Hii inamaanisha kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 33, atakuwa anapokea pauni milioni 123 kwa msimu. Barcelona imesema katika taarifa iliyotoa kuwa “inasikitishwa na uchapishaji wa maelezo hayo”. Na kuongeza kuwa: “FC Barcelona haihusiki kwa namna yoyote ile katika uchapishaji wa taarifa hiyo na itachukua hatua stahiki za kisheria dhidi ya gazeti la El Mundo, kwa uharibifu wowote ule ambao huenda umetokea kwasababu ya taarifa hiyo. “FC Barcelona imeonesha kumuunga mk

DR Abbas: Ukitaka jifungie Serikali haitafungia watu ndani kisa corona

Image
Dar es Salaam. Serikali imetoa msimamo wake kuhusu Covid - 19 kwamba, haitachukua uamuzi wa kuwafungia Watanzania ndani, huku ikitoa maelekezo ya kuendelea kuchukua tahadhari. Hayo yamesemwa leo Jamapili Januari 31, 2021 na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbas wakati akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma, kuelezea mambo mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano. Amesema mwongozo wa Serikali kuhusu kile kinachoendelea duniani kuhusu Covid - 19 ni kuendelea kuchukua tahadhari kama ilivyotamkwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli wakati wa ziara yake Kanda ya Ziwa wiki iliyopita. “Kifupi cha ugonjwa wa virusi vya corona ni Covid - 19 ndiyo Kiswahili sanifu, Rais amesisitiza duniani ugonjwa unaendelea na kwa sababu ya maingiliano baina yetu na nchi zingine ni lazima tuendelee kuchukua tahadhari. “Watanzania waendelee kuchukua tahadhari zote lakini tusiwe na woga wala tusichomekewe mawazo na mikakati ya watu wengine,” amesisitiza Dk Abbas. Amesema ijap

Breaking News: Treni yapata ajali vingunguti Dar

Image
Imetokea Vingunguti Dar Es Salaam ikihusisha lori lililokuwa limebeba sukari na treni ya abiria. Taarifa zaidi zitafuata hapa hapa endelea kufuatilia   from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/36uKqpe via IFTTT

Baba Levo: Ningekuwa Mwanamke ningemzalia Diamond watoto watatu

Image
  Kupitia mtandao wa Instagram, Baba Levo ameandika: "KWA WEMA ALIONITENDEA DIAMOND PLATNUMZ KAMA ningekuwa Demu ningemzalia Watoto WATATU. NAMSHANGAA SANA ZUCHU...!Ndio maana NIMEKASHUSHA NA SUKARI ZAKE Youtube. Kwakweli #SHUSHA IMENIPA HESHIMA KILA KONA YA MTAA... THANKS BIG" from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3oIgvAk via IFTTT

JUMA LOKOLE na ARISTOTE wamlipua TANASHA, Watoboa SIRI ya ZARI na MAMA DANGOTE, Ujio wake Bongo

Image
JUMA LOKOLE na ARISTOTE wamlipua TANASHA, Watoboa SIRI ya ZARI na MAMA DANGOTE, Ujio wake Bongo VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3r9VAHT via IFTTT

Kumbe BongoFleva inalipa!! Diamond Platnumz anaingiza Milioni 200 kwa mwezi kwa matangazo tu

Image
  Msanii wa Bongofleva, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz amesema kila mwezi huingiza Sh200 milioni kutokana na kuingia mikataba na kampuni mbalimbali kuwa balozi wa bidhaa zao. Akizungumza katika kipindi cha TheSwitch kinachorushwa na redio ya Wasafi leo Alhamisi Januari 28, 2021, Diamond amesema fedha hizo ni mbali na zile anazoingiza kupitia muziki. Amebainisha kuwa anaingia mikataba na kampuni na amekuwa akifanya hivyo kwa kila kampuni inayohitaji huduma yake. “Endosment zangu mimi mshahara wangu kwa mwezi si chini ya milioni 200, na tunasaini mikataba kila siku. Ninaingiza kwa wiki Sh55 milioni kwa siku Sh7 milioni kwa saa moja Sh300,000 na kwa sekunde Sh6,000.” Amesema mwaka 2021 fedha anazozipata katika eneo hilo huenda zikaongezeka kwa kuwa anatarajia kuwa balozi wa vitu vingi zaidi kwa kuwa ameamua kufanya muziki kuwa kazi na biashara. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/36wdT1X via IFTTT

Zuchu aweka rekodi mpya Africa kwa wasanii wa kike wa muziki

Image
  Leo record mpya imeandikwa na Zuchu katika bara la Africa. Amekuwa msanii wa kwanza wa kike kufikisha views million 1 kwenye YouTube ndani ya masaa 22. Hongera queen wa bongofleva. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3cwKad4 via IFTTT

Myanamar: Jeshi latangaza hali ya dharura na kuchukua madaraka Baada ya Kumkamata Kiongozi wa Nchi Hiyo

Image
 Jeshi la Myanmar limetangaza hali ya dharura likidai udanganyifu wa kura katika uchaguzi, baada ya kuwakamata viongozi kadhaa akiwemo Aung San Suu Kyi. Jeshi la Myanmar limetangaza hali ya dharura kwa muda wa mwaka mmoja na kumuweka jenerali wa zamani kama rais, kimetangaza Jumatatu kituo cha televisheni cha Myawaddy kinachomilikiwa na jeshi. Jenerali wa zamani Myint Swe, ambaye awali alikuwa makamu wa rais, ametangazwa kama kaimu rais. Hata hivyo, katika hali hiyo ya dharura kamanda mkuu wa jeshi Min Aung Hlaing amechukuwa udhibiti kamili wa nchi hiyo. Tangazo hilo la jeshi limetolewa kufuatia kukamatwa kwa kiongozi wa Myanamar Aung San Suu Kyi baada ya siku kadhaa za mivutano nchini humo iliyozua hofu ya kutokea mapinduzi. Rais Win Myint na viongozi kadhaa wa ngazi za juu wa chawa tawala pia wamekamatwa mapema Jumatatu, amesema Myo Nyun msemaji wa chama hicho cha National League for Democracy . Akizungumza kwa njia ya simu na shirika la habari la dpa, Nyun amesema wak

Mfahamu Muuaji wa Wauaji Aliyeua Wauaji zaidi ya 70 Nchini Brazili

Image
Imekua ikiaminika kwamba chaguo (Choices) tunayochagua ndio yanatueleza tulivyo. Kuna msemo kwenye Biolojia unasema " Every major decision made human brain undergo a physical change over time" Lakini vipi kuhusu maamuzi ya mtu kuchagua maisha ya kua muuaji? Watu waliochagua kuishi kama wauaji wapo na huyu ni muuaji wa kutoka Brazili ambaye amekua akifanya uuaji kwa muda mrefu sasa. NAFASI ZA AJIRA ZILIZOTANGAZWA LEO BONYEZA  HAPA Pedro Redrigues Filho ni mmoja kati ya wauaji bora wa muda mrefu lakini yeye uuwaji wake ulikua tofauti na Wauwaji wengine (Killers). Yeye alikua anaua wauaji na wahalifu tu. Anaelezewa kama mmoja wa wagonjwa wa akili (Psychopath) na mchambuzi aliyekua anashughulikia kesi yake. Amezaliwa katiko mji wa Minas Geraismwaka 1954. Filho alikua na maisha yaliyogubikwa na mateso pamoja na vifo. Filho maisha yake ya unyanywasaji yalianza toka akiwa tumboni kwa mama yake ambapo baba yake alikua akimtesa sana mama yake japokuwa alikua na ujauzito, mate

50 Cent anataka kuingia ulingoni kuzichapa na Floyd Mayweather

Image
  50 Cent anataka kuingia ulingoni kuzichapa na Floyd Mayweather. Kwenye mahojiano yake kupitia V-103 "The Morning Culture", 50 Cent aliulizwa ni nani anataka kupigana naye kwenye pambano la masumbwi na hakusita kumtaja hasimu wake huyo wa muda mrefu. "Nitapigana na Floyd. Lakini hofu yangu ipo kwenye uzito, sijui kama naweza kufanana naye." alisema rapa huyo na mfanyabiashara. 50 Cent aliwahi kuwa memba wa karibu na Mayweather na hata kuingia naye ulingoni siku ya pambano na Oscar De La Hoya. Wawili hao walikuja kupishana kutokana na kutokubaliana kibiashara. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/39wW0lu via IFTTT

T.I Ajibu Tuhuma za Kuwadhalilisha Wanawake Kingono 'Mimi na Mke Wangu Hatujawahi Husika na Biashara ya Ngono Wala Kubaka"

Image
 T.I. na mkewe wamevunja ukimya, wameibuka na kukanusha tuhuma za unyanyasaji wa kingono zilizotolewa na wanawake zaidi ya 25 wiki hii. Rapa huyo ametumia njia ya video kuzungumzia suala hilo, amesema tuhuma hizo ni uongo na hazina ukweli wowote. "Kwa nguvu zote na hekima tunakanusha tuhuma hizi za kipuuzi zilizotolewa na watu wasiofahamika." ilisomeka caption kwenye video hiyo yenye dakika 8. T.I. aliendelea kusema kwamba ilikuwa ngumu kuweza kukaa kimya kufuatia tuhuma hizi ambazo pia zinamchafua na mkewe Tiny Harris. Anaamini amechafuliwa (defamed) kwa sababu wanaomtuhumu hawajafungua shauri lolote mahakamani. - "Hatujawahi kumlazimisha mtu yeyote, hatujawahi kumuhusisha mtu yeyote kwenye masuala ya kingono, hatujawahi kumteka mtu yeyote pasina ridhaa yake. Hatujawahi kusafirisha chochote, yani kinachohusu biashara ya ngono." alisema T.I. na kukanusha pia tuhuma za kubaka, "Sijawahi kumbaka mtu yeyote, kamwe sijawahi kumbaka yeyote." from UDAK

Taji Liundi "Mama Yetu Alitunywesha Sumu Mimi na Wadogo Zangu, Nipona Wadogo Zangu Wakafariki"

Image
Kwa mara ya kwanza mtangazaji nguli nchini Taji Liundi amefunguka kuhusu maisha yake binafsi na mchango wake katika tasnia ya muziki. Taji Liundi aka Master T ambaye amefanya kazi na vituo mbalimbali vya redio ikiwemo Redio one na Times fm toka miaka ya 1980 amefunguka mengi wakati akihojiwa na kipindi cha Salama Na cha Salama Jabir. Taji Liundi amesimulia kisa cha kusisimua na kusikitisha ambapo mama yake mzazi aliamua kuwanywesha sumu yeye na wadogo zake watatu tukio lililopelekea wadogo zake watatu kufariki dunia huku yeye (taji) akiponea chupu chupu. Tukio Hilo lilitokana na mgogoro wa ndoa baina ya mama yao na baba yao kutokana na kukosekana kwa uaminifu hasa upande wa mzee wake, baada ya mama Taji maarufu sana nchini Agnes Doris Liundi kugundua hilo aliazimia kujiua yeye na wanaye na ndiyo kisa cha kuwanywesha sumu wanaye. Mama Taji alihukumiwa kunyongwa mpaka kufa na Mahakama kabla ya kupewa msamaha wa Rais na Hayati Baba wa Taifa J K Nyerere. Baba yake Taji Liundi alik

Baba Levo: Natamani nife wa kwanza kabla ya Diamond, akitaka lolote ntamfanyia. Wadau wamfananisha Baba Levo na Gigy Money

Image
Msanii Baba Levo ameweka wazi kuwa anatamani Mungu amchukue hata leo ili watoto wake walelewe na Diamond. Baba Levo amesema hayo akieleza hisia zake baada ya Diamond kumlipia ada za watoto wake wawili wanao soma TUSIME SEC. Baba Levo anasema anatamani Mungu amchukue hata leo kabla hajamchukua Diamond kwani Diamond ni muhimu hapa duniani kuliko yeye .... napia amesema yuko tayari kumfanyia chochote Diamond akimwambia...maana ni mtu muhimu sana kwake. Hata hivyo wadau wengi wamekuwa wakimuona Baba Levo kama ni mtu aliye na matatizo ya akili hivi karibuni kiasi ambacho utofauti wake na Msanii Gigy Money ni mdogo sana na wengine wamekwenda mbali zaidi kumthadharisha Diamond kuwa makini na watu ya aina ya Gigy na Baba Levo ambao wanaweza kumponza zaidi kwani wamekuwa wakiropoka sana bila kujali wako watu na wana muingiza kwenye gharama sana. Hata hivyo wadau wamemuomba Diamond kumpatia Baba Levo Daktari wa Magonjwa ya akili. Wasalaam By Ruttashobolwa from UDAKU SPECIAL BLOG h

What went wrong with Dullvan (Nini kimempata msanii wa vichekesho Dullvan)?

Image
  Dogo ana kipaji kizur Sana , lakn sasa anakoelekea , sio poa baadhi ya reaction za mwili zinajengwa na mazoea , baada ya mda sitashangaa anakuwa na mambo ya kike kike...ajitahdi kubalance mambo naona sa hv amekuwa extremely kuact kama mwanamke , may be anamake huge 💰 , but soon gharama yake itaonekana .... from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/36rzLf5 via IFTTT

Gigy Money Ajiweka Kwa Juma Jux

Image
Ni Picha ya Pamoja Msanii Juma Jux na GigyMoney Wakiwa Katika Pozi Matata Sana. Inasemekana lakini Kwa sasa wapika umbwambwa na Kupakua from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3pzrBIR via IFTTT

Wachezaji wa Simba SC watakaoikosa TP Mazembe

Image
  Kuelekea mchezo wa Simba Super Cup leo Januari 31, 2021 kati ya TP Mazembe dhidi ya Simba SC kwenye uwanja wa Mkapa, hawa ndio wachezaji wa Simba SC ambao hawatakuwa sehemu ya mchezo huo.   Kwa mujibu wa meneja wa timu ya Simba SC Abbas Ally, wachezaji wa timu hiyo ambao walikuwa na timu ya taifa kwenye michuano ya CHAN kama Aishi Manula hawatacheza licha ya kujiunga na kambi ya Simba SC. Wengine ni Shomari Kapombe, Said Ndemla, Ibrahim Ame na John Bocco, ambao nao watakosa mchezo wa leo dhidi ya TP Mazembe.    Mchezo huo pia utatangazwa mubashara kupitia East Africa Radio na watangazaji Mtaalam wa Soka Ibra Kasuga na Abissay Stephen kuanzia saa 9:30 mchana ambapo studio watakuwepo David Kampista na Tigana Lukinja. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/36vDuIy via IFTTT

Unaambiwa Serikali imeokoa Shilingi Milioni 389, Dr Gwajima Afunguka

Image
  Wizara ya Afya imeokoa takribani shilingi milioni 389 katika ujenzi wa jengo la Idara ya huduma za wagonjwa wa dharura linalojengwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora- Kitete ambalo limewekwa jiwe la msingi na Rais Dkt. John Magufuli. Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia Dkt. John Pombe Magufuli, Dkt. Gwajima amesema ujenzi wa jengo hilo litakalo wahudumia wakazi wa Tabora, mikoa ya jirani na hata nje ya nchi kutokana na barabara kuu zinazopita mkoani hapo kwakuwa jengo hilo litakua na uwezo  kuwahudumia wagonjwa 50 hadi 60 tofauti na awali ambapo walikua wakihudumia wagonjwa 3 hadi 5. "Tumepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Mhe. Rais mimi pamoja na wizara yangu tutayafanyia kazi ikiwemo kuongeza madaktari bingwa, kuwafuatilia wale walioondoka pamoja na jengo la huduma la mama na mtoto kwa ajili ya kujifungua na ICU", amesema Dkt. Gwajima. Mi

Naumia Sana, Nimemzimikia Boss Wangu Kazini ..Sijui Nifanyaje

Image
Nimepata ajira mpya wiki ya kwanza mambo yalikuwa safi kuizoea na kuipenda kazi yangu wiki ya pili nikajikuta nimampenda sana huyu kaka yeye ni moja wapo ya superiors wangu ninareport kwake baadhi ya kazi zangu. Nahisi kagundua nimezama kwake so huwa ananiongelesha kwa upole sana hata nikikosea katika kazi hawi mkali kabisa na haikuwa hivyo wiki ya kwanza nilipofika,saingine hawezi kuniangalia machoni kwa mda mrefu,tukionana huwa tunasalimiana kwa furaha na matabasamu ya kutosha ila ni mtu ambaye yupo busy sana ni wale hardworkers kwenye institution. Kweli naumia nahisi sijawahi kupenda hivi ofcoz maisha yangu yote ilikuwa a man ananifata kwanza then ananiconvince mpaka naingia line ila this is different mimi ndiyo nimefall yeye ni mme wa mtu na mimi ni mke wa mtu (of coz mimi bado mrembo najijua ninamvuto)Mme wng tuna miaka 8 ndoani sasa anaupendo sana na ni baba bora sana ila ndo nimekumbwa jamani nimesali na kukemea hii hali ipotee ila ndo inazidi sijawahi kuwaza hela yake nata

Nimemkuta Mume Wangu Akifanya Ngono na House Girl wa Jirani Yetu

Image
Juzi nilikuwa naenda kazini nikamuacha mume wangu nyumbani anaangalia TV, gari langu likazima ghafla kiasi cha kilomita moja toka nyumbani. Nikaona nitembee mpaka nyumbani kumwomba mume wangu aje anisaidie kutengezagari, kwa mshangao wangu nilipofika nyumbani nikamkuta mume wangu yuko chumbani na msichana wa kazi wa nyumba ya jirani. Mume wangu ana miaka 43, mimi nina miaka 39 na msichana huyo ana miaka 19 hivi.Tumekuwa katika ndoa kwa miaka 10. Nilipomuuliza mume wangu alikubali kuwa uhusiano wao umekuwa ukiendelea kwa miezi sita sasa, nifanye nini mimi? NISHAURINI NIFANYAJE NDUGU ZANGU... SHARE HII TAFADHALI from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2EPYazH via IFTTT

Siri Yafichuka H Baba Adai Irene Uwoya ana Damu Yake "Tuendelee Kuitunza Siri Yetu"

Image
  ANAANDIKA H.BABA >>>Polee sana @ireneuwoya8 kwa Msiba wa Babu yetu kipenzi Allah akupe nguvu Allah akulinde Allah akusimamie nitunzie damu yangu #Tuendelee kuitunza Siri yetu Nakupenda pia !! Damu nzito kuliko maji??? 😭 DAMU GANI TENA HILO?? from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3j4aGvI via IFTTT

The Story Book Msitu Wa Shetani wenye Vituko Vya Kutisha Vya Nguvu za Giza

Image
The Story Book Msitu Wa Shetani wenye Vituko Vya Kutisha Vya Nguvu za Giza VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/32xl8nA via IFTTT

Maajabu ya Wanawake Yaliyowashinda Hata Wana Falsafa Kuelewa

Image
*Naomba msipanick walimu,🙌🏼* *Ukinipinga pinga kwa hoja.* Wanawake ni binadamu wa ajabu sana katika uso huu wa Dunia yaani hawa watu ni next level, kuwaelewa ni ishu iliyowashinda hata wana falsafa, Newton na uwezo wake wote linapokuja suala la wanawake lazima atoke kapa na (ndio maana haieleweki hata kama akioa). Manabii na busara zao zote walishindwa kuwaelewa wakaishia kushauri ya kwamba tuishi nao kwa akili. Sasa najiuliza ni jambo gani unaweza fanya bila kutumia akili?, hapa ndipo napata ushahidi kwamba kumbe wanawake walishindikana tangu zama za mwanzo kabisa!. Wanasaikolojia wanasema kuwa kama utamuoa/kuishi na mwanamke mwenye miaka 25 basi itakuchukua miaka 25 mingine kumuelewa huyo mwanamke angaalau kwa 90% maana hawa kila siku hubadilika na kuwa wapya kimatendo na kifikra. Mwanamke unaweza mnunulia BMW X6 akatoka nayo kwenda kutembea, akiwa njiani akaombwa lift na kijana akampa akipitia sheli hela ya mafuta ikawa haitoshi, yule kijana akaamua kumuongeza ata elfu 20 ba

Diamond amchezesha mama yake singeli jukwaani, amuita na Uncle Shante (+Video)

Image
  Ikiwa ni mwishoni mwa Show walipanda jukwaani familia ya Diamond Platnumz ikiongozwa na mama yake mzazi Mama Dangote, Mzee Shante pamoja na dada yake Esma. Wakiwa Jukwaani Diamond alimchezesha mama yake Singeli akiwemo Mzee Shante na Esma kupitia wimbo wa Dulla Makabilla. Video nzima ipo kwenye akaunti yetu ya YouTube ya ya Bongofive. VIDEO:   from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3cE1fCb via IFTTT

Diamond awataja Tanasha, Hamisa jukwaani, arusha dongo hili (+Video)

Image
  Akiwa jukwaani Diamond Platnumz aliamua kutumia wimbo wa Singeli aliokuwa akiimba na Dulla Makabilla kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa kusema kuwa Eti wanasema yeye amerudiana na Tanasha lakini pia hawajaishia hapo wakasema tena yeye ( Diamond Platnumz) hajafanana na mtoto wa Hamisa Mobetto ( Mtoto wake) Dyllan VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3t90xm2 via IFTTT

Uso kwa Uso CHID BEENZ na PROFESSOR JAY wafunguka mazito baada ya kufika kwenye SHOW ya tumewasha

Image
Uso kwa Uso CHID BEENZ na PROFESSOR JAY wafunguka mazito baada ya kufika kwenye SHOW ya tumewasha VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/36rwQTC via IFTTT

Arusha DC yataja sababu za kutofikia malengo ya ukusanyaji mapato

Image
   Halmashauri ya Arusha imetaja sababu zilizochangia kushindwa kufikia malengo ya ukusanyaji wa mapato katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2020/21,ikiwa ni pamoja na kokosekana kwa ulipaji kodi wa hiari kwa wafanyabishara na kuyumba kwa bishara ya utalii. Hayo yamesemwa Januari 29, na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Saad Mtambale, akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani. Amesema halmashauri hiyo ilijiwekea makisio ya makusanyo ya Sh billioni 59.188 ila hadi Desemba 31 mwaka jana ilikuwa imekusanya zaidi ya Sh bilioni 21.837. Ametaja sababu hizo ni kukosekana kwa ulipaji kodi wa hiari kwa baadhi ya wafanyabiashara na kuwa bila kusukumana wengi wao hawatoi kodi ambapo wamejipanga kama watendaji kutembelea maeneo mbalimbali na kuhakikisha kila anayepaswa kulipa kodi analipa na kwa kiwango kinachotakiwa. Amesema changamoto nyingine ni kushuka kwa biashara ya utalii ambapo amesema kuwa uchumi wa Arusha unategemea  sana utalii na kutokana na janga la corona lililokumba

Hofu ya bomu kwenye msikiti Uswidi

Image
Kisanduku kinachofanana na bomu kimepatikana kwenye mlango wa msikiti mmoja uliopo katika mji mkuu wa Stockholm nchini Uswidi. Imam wa Msikiti wa Stockholm, Mahmoud Khalfi, alitoa  maelezo kwenye kituo cha SR cha redio ya serikali nchini Uswidi na kusema kwamba walikuta kisanduku kinachofanana na bomu kilichowekwa kwenye mlango wa kuingilia msikitini na kuzua hali ya wasiwasi. Khalfi alisema, “Tulipofika kwenye sala ya asubuhi, tuliona kisanduku kiinachofanana na bomu mlangoni. Nyaya zote 3 kutoka kwenye kisanduku hicho ziligandishwa mlangoni. Tuliwajulisha polisi haraka ambao baadaye walitenganisha kisanduku na nyaya zake na  kuchukua ili kufanyia uchunguzi.” Akibainisha kwamba misikiti yake imekuwa ikishambuliwa mara kadhaa, Khalfi alisema kuwa wao wamekuwa walengwa wa mashambulizi ya kibaguzi zaidi ya mara mbili kwa mwaka. Msemaji wa Polisi wa Stockholm Per Fahlström, aliarifu kugunduliwa kwa mtu aliyeweka vifaa hivyo kupitia kamera za usalama na kwamba uchunguzi unaendelezwa.

Album ya Ray Vanny 'Sound From Africa' ni nzito! Hawa ni wasanii aliowashirikisha

Image
  Album ya Ray Vanny 'Sound From Africa' ni nzito! Hawa ni wasanii aliowashirikisha VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3r5Cgvl via IFTTT

Kaze Akisuka Upya Kikosi Chake

Image
KOCHA Mkuu wa Yanga Mrundi, Cedric Kaze ameanza program ya kukinoa kikosi chake kwa kuwatengeneza kisaikolojia nyota wake Said Ntibazonkiza ‘Saido’ na Tuisila Kisinda baada ya kutoka katika mapumziko kwa lengo la kuendelea na kasi waliyoanza nayo mwanzoni mwa msimu.Yanga ilianza vema msimu huu kwa kucheza michezo 18 bila ya kupoteza ikishinda 13 na sare tano pekee. Yanga inayoongoza kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 44, juzi iliingia kambini huko kijiji cha Avic Town, Kigamboni jijini Dar es Salaam tayari kwa kuendelea na michezo ya ligi wakiwa wameliimarisha benchi lao la ufundi. Akizungumza naChampioni Jumamosi,mara baada ya kuanza mazoezi alifanya kikao na wachezaji wake na kikubwa kusahau likizo fupi ya siku kumi aliyowapa mara baada ya kutoka kwenye Kombe la Mapinduzi na badala yake wafahamu wamerejea katika majukumu yao ya kazi.Kaze alisema mara baada ya kikao hicho taratibu aliona mabadiliko makubwa ya wachezaji wake kwa kurejea katika hali yao ya kawaida katika mazoez

RAY VANNY adondoka vibaya jukwaani na kushindwa kuendelea na SHOW, BABA LEVO ashindwa ashuka naye

Image
RAY VANNY adondoka vibaya jukwaani na kushindwa kuendelea na SHOW, BABA LEVO ashindwa ashuka naye VIDEO: from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3ouXZLn via IFTTT

Shoo Ya Diamond, Aingia Kifalme Uwanjani, Aandika Historia -Video

Image
TAMASHA la Wasafi Tumewasha na TiGo limefanyika usiku wa kuamkia leo Januari 31, 2021 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar na wasanii zaidi ya 20 wamepafomu wakiongozwa na, Diamond Platinumz. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/36sTlYi via IFTTT

Wabunge wa Trump wanaingia Bungeni na bastola

Image
  Spika wa Bunge la Marekani Nancy Pelosi ameomba Serikali kuwaongezea ulinzi zaidi Wabunge huku akisema Adui yupo miongoni mwa Wabunge wenyewe.   “Kuna Wabunge wa Chama cha Republican cha Rais wa zamani Donald Trump wanaingia Bungeni wakiwa na Bastola, na kutishia usalama, tuongezewe ulinzi”-Nancy Kumekuwa na kauli kadhaa za FBI kuonya kuwa huenda kukatokea tukio la kigaidi siku za karibuni Nchini Marekani, tangu Wafuasi wa Trump wavamie Bunge na kufanya vurugu zilizopelekea vifo vya Watu kumekuwa na hofu ya kutokea kwa vurugu nyingine pia. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2MkSHVV via IFTTT

Huyu Mwanamke Aliyeitwa Ngamia Kutokana na Ugonjwa Wake wa Miguu

Image
  Ella Harper alizaliwa Januari 5, 1870 akiwa na tatizo la mifupa ambalo lilisababisha magoti yake kujipinda kwa nyuma, hali iliyomlazimisha kutembea kama mnyama Ugonjwa wa Mifupa aliokuwa nao ulikuwa unafahamika kama Congenital genu recurvatum, na hali hiyo ilipelekea Ella kuitwa ‘The Camel Girl’ au Msichana Ngamia Mwaka 1886 alijiunga na kikundi cha maonesho mbali na ulemavu wake, na alikuwa akijipatia $200 kwa mwezi kama mshahara, hali iliyoleta nuru katika maisha yake. Alifariki dunia Desemba 19 mwaka 1921 from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3oxokbK via IFTTT

Masau Bwire "Niombeeni nimekamatika haswa! Nimeambiwa nimekula chakula chenye sumu"

Image
OFISA Habari wa Ruvu Shooting inayoshiriki Ligi Kuu Bara amewaomba Watanzania wamuombee kwa kuwa kwa sasa hali yake haijatengamaa kwa kile ambacho ameambiwa na madaktari kuwa amekuwa chakula chenye sumu. Kupitia ukurasa wake wa Istagram Masau Bwire ameandika: Kwa siku kadhaa zilizopita, nimekuwa sipokei simu, au nikipokea nasema tu siko vizuri, siwezi kuzungumza! Wapo walionielewa, lakini wapo walioona kama ni jeuri na kiburi tu, nafanya makusudi, kwa sababu sitaki kuzungumza nao. Niwaombe radhi, wanisamehe kwa yote, lakini pia niwaaambie, na kuwahakikishia kwamba, sina kawaida hiyo ya kutopokea simu ya mtu yeyote atakayenipigia, siwezi kudharau simu ya mtu yeyote, daima namuomba Mungu, aniepushe na tabia hiyo ya kishetani ya kudharau na kutowapa ushirikiano pale wanapohitaji lolote kutoka kwangu. Kwa kweli nilikuwa katika hali ngumu, kama unavyoiona hiyo picha, ndio uhalisia wa namna nilivyokuwa, nilikamatika haswa! Baada ya vipimo vya Hospitali, wataalamu wa afya (Daktari), wa

Breaking: Ishu ya Polisi Kusitisha Tamasha la Wasafi Dar

Image
Kamanda wa polisi Mkoa wa Temeke, Amon Kakwale amekanusha taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba limesitisha tamasha la “Tumewasha na Tigo” linaloandaliwa na Wasafi Media kwa sababu za kiusalama. Taarifa hizo ambazo Kakwale ameziita za uzushi zimesambaa mitandaoni leo Januari 30 zikionyesha barua yenye taarifa zote muhimu za jeshi la polisi kama vile nembo, muhuri, jina na sahihi. Kamanda Kakwale amesema tamasha hilo lipo, litaendelea kuwepo na Jeshi la Polisi litatoa ulinzi kama kawaida. “Hiyo barua si ya kweli, tamasha lipo na litapewa ulinzi na Jeshi la Polisi kama ilivyo kwa matamasha mengine,” amesema kamanda. Aidha, kamanda huyo amewakemea watu wenye tabia ya kugushi barua kama ilivyofanyika kwa hiyo na kuwataka waache mara moja. “Si jambo zuri kugushi barua namna hii. Hiki kilochofanyika ni matumizi mabaya ya ofisi,” amesema. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3oxX7Wu via IFTTT

Breaking News: JPM Aagiza Daktari Aliyeacha Kazi Asakwe "Wanakuwa Wabinafsi Sana"

Image
  RAIS  John Magufuli amemwagiza Waziri wa Afya, Dkt Dorothy Gwajima, kuhakikisha anawafuatilia madaktari walioacha kazi katika hospitali ya rufaa mkoa wa Tabora kwa sababu ya maslahi na kuhamia hospitali binafsi na ikiwezekana wafungiwe pamoja na hospitali walizokimbilia. Ametoa amri hiyo kufuatia kuondoka kwa daktari mmoja katika hospitali hiyo ya mkoa na kwenda katika hospitali binafasi.   Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 30, 2021, wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la magonjwa ya dharura katika hospitali hiyo na kwamba haiwezekani serikali ipoteze pesa kwa ajili ya kusomesha madakatari na wao badala ya kuwatumikia wananchi wanaanza kuwa wabinafsi kwa kutaka maslahi makubwa. “Mfuatilie huyo daktari aliyekimbia hapa, uifuatilie na hiyo hospitali ikiwezekana tunamfungia huyo daktari na tunaifungia na hiyo hospitali aliyoenda kutibia ili watu waanze kujifunza kwamba wizara ya afya siyo ya kuchezea tu, unamsomesha mtu kwa fedha za Watanzania halafu anasema ma

Barbara: Kesi ya Yanga na Morrison Bado Ipo, Bado Wanahangaika Kama Wameachwa na Mpenzi

Image
OFISA Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba, Barbara Gonzalez amethibitisha kuwepo kwa kesi kati ya Klabu ya Yanga na mchezaji wao, Bernard Morrison na kusema kuwa kwa sasa sakata hilo lipo mikononi mwa wanasheria wao ambao wanalishughulikia. Tangu asajiliwe na Simba katika usajili ulioonekana kuwa na utata Morrison amekuwa akikumbana na vipingamizi vingi kutoka kwa waajiri wake wa zamani Yanga, huku kesi iliyopo CAS ikitajwa kuwa sababu kubwa ya kushindwa kuonekana kwa mchezaji huyo uwanjani kwenye michezo ya kimashindano tangu Desemba mwaka jana. Hivi karibuni uongozi wa Yanga chini ya Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Fredrick Mwakalebela ulikiri kupeleka kesi hiyo kwenye mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa michezo CAS, ambapo Yanga wamesema shauri hilo linatarajiwa kusikilizwa hivi karibuni. Akizungumzia kuhusu sakata la mchezaji huyo Barbara alisema: “Kesi ya Morrison na Yanga kweli bado ipo na wanasheria wetu wanashughulikia.“ Naona Yanga bado wanahangaika, ni kama u

Babu Tale – Marehemu Mke Wangu Aliniambia Nimechoka Kuishi, Mimi Naondoka ila Usioe

Image
MBUNGE wa Morogoro Kusini Mashariki, Mhe. Hamisi Taletale ‘Babu Tale’, ambaye alifiwa na mkewe, Shamsa Kombo ‘Shammy’, Juni 26, 2020, amefunguka mazito kuhusiana na marehemu mke wake huyo kwenye mahojiano na mtangazaji Salama Jabir kwenye kipindi chake cha SalamaNa. “Marehemu mke wangu tulifahamiana Magomeni Kota kwa sababu na yeye alikuwa anaishi pale, nilimtongoza mwaka mzima hajanikubali. Enzi hizo nilikuwa mtu flani rafu halafu yeye ana mambo ya Kizungu” ameeleza Babu Tale. “Mke wangu aliniambia nisioe, nakumbuka hiyo siku nimeshinda naye Muhimbili, akaniambia nimechoka kuishi hii hali, akanishika mkono kuniambia mimi naondoka, lea watoto lakini usioe, usioe, usioe.” BabuTale aliendelea, “Kinachoniliza ni kupoteza mtu ambaye angeweza kuniongoza kwa vitu vingine, nimepata uongozi lakini yule aliyetakiwa kula good time hayupo”. Marehemu Shammy enzi za uhai wake alifahamika zaidi kutokana na asasi yake aliyoimiliki ya ‘Nasimama Nao‘ iliyokuwa ikiwasaidia kina mama na

Tumia Dawa ya Mitishamba ya Super Mihayo Inayotibu Tatizo la nguvu za Kiume

Image
SUPER MIHAYO MPYA WHATSAP NO +255 746 758 853 Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile, - kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa - maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo - kukosa hamu ya tendo la ndoa - kushindwa kurudia tendo la ndoa - uume kusimama kwa kulegea - uume kulegea katikati ya tendo - kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu - kuishiwa nguvu kutokana na punyeto. Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MIHAYO. kiboko ya matatizo haya. _______________________________ Pia kuna SUPER MIHAYO. Kiboko ya uume mdogo inaboresha maumbile ya uume kwa kurefusha na kunenepesha kwa saizi uipendayo haijalishi umri hata kwa walioathirika na upigaji punyeto. _______________________________ Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume na uume mdogo. _______________________________ (1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea. (2) ngi

DC Sabaya aibukia mochwari apiga marufuku maiti kuzuiwa kisa madeni

Image
  Serkali Wilayani Hai imepiga marufuku masharti yanayowekwa na Hospitali ya kuzuia miili ya watu waliofariki hadi Ndugu zao watakapomaliza madeni yanayotokana na matibabu wakati wa uhai wake. Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ameelekeza kutowekwa sharti lolote wakati wa kuchukua mwili na kuongeza kwamba utaratibu huo unaongeza huzuni na majonzi kwa wafiwa. Amesema inashangaza kuona huu utaratibu unakita mizizi huku ukiwa hauendani na Mila na Desturi za kibinadamu. Sabaya pia ameonya Watumishi wa Afya kuacha kuwekeza katika kufitiniana na majungu kwani kunaua na kuondoa Watu wenye uwezo katika Taasisi na kubakiza Watu ambao wamewekeza katika maneno tu. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3t8DoAf via IFTTT

NIGERIA; Wasichana waliotekwa na Boko haramu mwaka 2014 wafanikiwa kutoroka (+ Video)

Image
  Taarifa kutoka Nigeria zinasema kwamba wasichana zaidi waliokuwa wametekwa nyara kutoka shule ya wasichana Chibok mwaka 2014 wametoroka kutoka kwa wanamgambo wa Boko Haram. Baba wa mmoja wa wanafunzi wa zamani wa Chibok ameiambia BBC kuwa alizungumza na binti yake ambaye amenusurika. Amesema walizungumza nae kwa njia ya simu baada ya kufanikiwa kutoroka na alikuwa analia. Yeye na wasichana wengine waliotekwa nyara katika shule ya wasichana ya Chibok na maeneo mengine wameripotiwa kutoroka kutokana na operesheni za kijeshi dhidi za jeshi la Nigeria dhidi ya Boko Haram. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/39x936t via IFTTT

Akamatwa kwa kumuweka mama yake kwenye jokofu nyumbani kwa miaka 10

Image
  Polisi nchini Japan wamemkamata mwanamke mmoja baada ya mwili wa mama yake kukutwa kwenye jokofu nyumbani kwake.   Yumi Yoshino, 48, amesema kuwa alimkuta mama yake akiwa amefariki kisha aliuficha mwili wake miaka 10 iliyopita kwa sababu ” hakutaka kuhama” katika nyumba waliokuwa wakiishi mjini Tokyo, vyombo vya habari vimeripoti, vikinukuu maafisa polisi ambao hawakutajwa majina yao. Hakukuonekana majeraha yoyote kwenye mwili ulioganda barafu, polisi wameeleza. Mamlaka hawakuweza kuthibitisha muda na sababu ya kifo cha mwanamke huyo. Mwili uliripotiwa kugundulika na mfanya usafi baada ya Bi. Yoshino kulazimishwa kuondoka katika nyumba hiyo kwa sababu ya kukosa kodi. Mwili ulikuwa umekunjwa kiasi cha kutosha kuingia kwenye jokofu lenye barafu, polisi walisema. Bi Yoshino alikamatwa katika hoteli mjini Chiba karibu na jiji la Tokyo, siku ya Ijumaa. from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2M8toX9 via IFTTT

Majambazi Warejesha Mali za Wizi

Image
Kizaa zaa kilizuka katika mtaa wa Mathare jijini Nairobi baada ya wanaume wiwili, kuanza kula  nyasi. Wenyeji walifika eneo hilo kwa wingi kuweza kujionea tukio hilo lisilo la kawaida.  Kulingana na wenyeji wa kitongoji hicho ni kua jamaa hao ambao mara kwa mara wamekua  wakijihusisha na visa vya ujambazi wamewaangaisha kwa muda, na wamependezwa sana  kuwaona wakila nyasi. Mmoja wa mwenyeji katika eneo hilo alisema kuwa, mara kwa mara  amekua akipoteza vifaa vidogo vidogo chumbani mwake kwa njia tatanishi asijue nani alikua  anajihusisha na swala hilo. Ameweza kuripoti visa hivyo katika kituo cha polisi mtaani humo  lakini hakuna yeyote yule ameweza kunaswa na tuhuma hizo za wizi wa mali. Analalama polisi  mtaani humo ni kama wanashirikiana na majambazi hao ndiposa ripoti ya wizi inapopigwa haichukuliwa na uzito au hadhi yoyote ile.  Muathiriwa Juma pia naye alilalama kua mara kwa mara wezi huvunja lango kuu kwake nyakati  za usiku na kuingia kwake nyakati za usiku na kuiba mali. Al

Natamani Mpenzi Wangu Achepuke Aweze Kujua Ladha ya Wengine..Mimi sio Mwanaume Sahihi Kwake

Image
Niko kwenye mahusiano na binti mmoja kati ya wengi nilionao. Kiukweli natamani huyu binti achepuke kwa mwanaume mwingine, huyu binti niko nae kwenye mahusiano zaidi ya mwaka mmoja sasa. Natamani achepuke labda huko atapata mwanaume atakaemfaa katika maisha yake. Huyu binti ni mwema sana kwangu kiasi kwamba wema wake unageuka kua kero kwangu, mimi ndie mwanaume wake wa kwanza, nina uhakika hajawahi kutoka na mwanamume mwingine kabla yangu na baada yangu. Nikiri kua nilitumia muda mwingi na gharama nyingi kumshawishi huyu binti kua mimi ndie mwanaume sahihi aliekua amemtunzia mwili wake hadi akakubali kuniruhusu kuchana nyavu. Download App ya Udaku Special  HAPA  Kusoma Hizi Habari Kupitia Simu yako Kirahisi Natamani achepuke maana huko aanaweza kupata mwanaume mwingine mwema kwake,kwa kweli hutu binti hastahili kua na mimi, ni mwema kiasi kwamba hadi namuonea huruma, anaomba radhi kwa makosa ambayo hakufanya au nimefanya mimi. Nashindwa huyu binti namuachaje ili aende

Kuvaa Shanga Miguu au Vikuku Kwa Mwanamke Kuna Maana Yoyote Mbaya?

Image
Kumekuwa na tetesi nyingi kuhusu urembo huu wa kuvaa cheni za miguuni. Wengi wamekuwa wakisema kuwa cheni hizo zinamaanisha kwamba mvaaji anaonyesha kwamba yeye anaweza mapenzi ya kinyume na maumbile, au analika pande zote tetesi hizi zimeleta mchanganyiko kidogo kwenye urembo huu. Watu wengine wamediriki hata kukataza kabisa wapenzi wao wasivae urembo huo, mimi binafsi siwezi kuongozana na mtu amevaa kitu kama hicho. Haya sasa kazi kwako mdau, wewe unaonaje ni sawa urembo huo kutumika, na je mwenza wako akivaa urembo huo, utaafiki? from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2ZH8gLa via IFTTT

Diamond aibuka na sakata mtoto wake kupewa mwanaume mwingine

Image
Dar es Salaam. Wakati sakata la yupi baba mzazi wa msanii wa muziki, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz likiwa bado vichwani mwa watu, msanii huyo ameibuka na kufunguka kuwa hata yeye ana mtoto ambaye mzazi mwenzie amegoma kumpatia na huenda ameshapewa baba mwingine. Diamond alisema hayo kupitia mahojiano aliyoyafanya na kipindi cha The Switch cha Wasafi FM, Januari 28 baada ya kuulizwa anadhani ana watoto wangapi. Akijibu, Diamond alisema anachojua ana watoto sita, tofauti na watu wengi wanavyofahamu kwamba ana watoto wanne ambao ni Tiffah na Nillan aliozaa na Zarina Hassan “Zari”, Dylan aliyezaa na mwanamitindo Hamisa Mobetto na Naseeb Junior aliyezaa na mwimbaji kutoka Kenya, Tanasha Donna. “Watu wengi wanafahamu mtoto wangu wa kwanza ni Tiffah, lakini ninao wengine wawili ambao walizaliwa kabla yake. Kuna mmoja yuko Mwanza, mama yake amegoma kunipa, pia juzi kati nimeletewa mtoto mwingine wa kike hapa hapa Dar es Salaam, lakini sijawahi kumuona. “Mama wa huyo mtoto yuko

Breaking News: Waziri Mkuu DRC Ajiuzulu

Image
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Sylvestre Ilunga Ilunkamba,  amejiuzulu rasmi wadhifa huo na kuwasilisha barua yake kwa Rais Félix Tshisekedi.   Ilunga, ambaye ni mshirika mkuu wa mtangulizi wa Rais Tshisekedi, Joseph Kabila, ameongoza baraza la mawaziri la Serikali ya Muungano kwa miezi 15.     Hata hivyo, wabunge walipitisha kura ya kutokuwa na imani na serikali yake Jumatano wiki hii na akapewa saa 24 awe amejiuzulu. Kujiuzulu kwake kunatoa fursa kwa  Tshisekedi  kuwateua washirika wake kama mawaziri.     Hadi sasa, utendaji wa Tshisekedi umekuwa ukidhibitiwa na muungano alionao na Kabila ambao uliafikiwa wakati alipoingia madarakani miaka miwili iliyopita.   Ushindi wake katika uchaguzi mwezi Desemba 2018 ulisifiwa kama wa kihistoria, ambapo kulikuwa na makabidhiano ya kwanza ya utawala kwa njia ya amani ambayo hayakuwahi kushuhudiwa katika historia ya miongo sita nchini humo. Tshisekedi bado hajamchagua waziri mkuu mpya ambaye ataunda