MASHAIRI MATAMU YA MAPENZI

Mpenzi mwandani mahabubu 
Naanza kwa kukuomba samahani 
Kuandika kwa lugha hii legevu 
Nilijaribu lakini sikuweza 
Kuyasarifu maneno matamu 
Kwa lugha muafaka ya kimapenzi 
Mara nyingine ninaahidi 
Kutakalamu kwa lugha inayofaa 
Bidii nitafanya 
Kuyaelewa machungu na matamu yanguKwa lugha tukufu isiyo yangu 
Badala ya hiki kishairi duni, 

Nitakwandikia poem 
Nitajitahidi mpenzi 
Maneno kuyaelewa 
Si kwa jicho la kwangu kijijni 
Bali kwa mboni na urazini wa kule kulikotukuka 
Nitayatongoza machozi yangu 
Kububujika kwa vokali na konsonanti za kimombo 
Makali ya moyo wangu kulipuka kwa Kireno, 
Kitaliani au Kituruki 
Badala ya huu msamiati nilokujazia hapa, 

Nitakuwa na vocabulary Mpenzi nitakusifu 
Kwa majina ya mimea, wanyama na ndege 
Wasiopatikana kwetuNitakutungia koja 
Nilirembe kwa vito na maua ya nchi za baridi 
Au mimea ya jangwaniNisamehe kwa sasa mpenzi 
Naikumbuka tu lugha yangu 
Ilonitoa tumboni mwa mama 
Ninajua mpenzi 
Ni vigumu kwangu kujieleza 
Vigumu kwako kuelewa 
Nyimbo za nyumbani kwetu kijijini 
Ambako tulitembea pamoja tukivikwea vilima 
Mikono yetu ikiwa kama sumaku na chuma
Ni vigumu mpenzi 
Wewe kuzikumbuka zile harufu 
Za mimea iliyotushangilia 
Katika sherehe yetu ya mahaba na huba 
Samahani mpenzi 
Nimeianza barua hii kwa jina lako la kwanza 
Wewe kwako ndilo jinalo la kati 
Lililotumika kule nyumbani 
Kabla ya kuujua mji, 
Ugeni na ustaarabu wake. 

Nitakuita kwa jina ajualo nyanyako kutamka 
Nitajitahidi mpenzi 
Kukujua kwa jina lako la mjini, dini na usasa wake 
Niwie radhi mpenzi 
Nitasema nawe kwa sauti 
Wanaokuona na kukusikia laazizi 
Wajue asili na usuli wako 
Kwa muda wasikunasibishe 

Na ungwana wa lugha uliyoizoea 
Kwa mishangao waashame 

Badala ya salaale
Wamake na kubweka ’gosh’!
Ningelipenda kuahidi kwenda nawe kupata mlo
Lakini natanguliza samahani
Ni haja yangu kukupeleka kula pizza
Lakini nimetafuta jinale katika lugha yangu
Nikakosa kabisa kabisa
Kwa hivyo mpenzi

Samahani zangu zikitangulia
Nakuahidi ugali wa wimbi
Samaki wa kuchemsha
Na mkunde wa kibakuli cha kando

Mpenzi hitari kula mtori
Jasiri pia kuonja makande,
Rojo la mrenda,
Mukimo na muthogoi.
Tutakula pia sageti,

anagu na wenzao.
Tutanyunyiza mafuta
Matamu ya samli,
Kisha tummemene tombo,
Alochomwa kwa makaa.
Jioni tutakaa
Chini ya uso wa mbalamwezi
Tukichoma ndizi,
Viazi na mihogo
Anga zitachanua
Kwa thureya ya nyota
Zikiimba wimbo bora
Wa mapenzi motomoto
Hewani kutafukizwa,
Uturi wa manukato

Ya samadi kavu inayoungua.
Samahani mahabubu,
Ingawa utatamani,
Kifukuza mbu muafaka,
Hii mwandani, haina viletamaradhi.
Sikio letu kichuna,
Tutamwazima bibi,
Babu akiwa mwenzake
Fikira zetu tuwape pia
Kutusafirisha mbali
Watupatie paukwa pakawa
Za miaka hii na iliyokuwa
Samahani mpenzi
Yameniishia maneno
Nimeyatesa macho yako,
Masikio na fikira zako
Misri kukurudisha
Japo kwa muda kidogo
Nikuandikiapo mara nyingine,
Nitakupeleka Zayuni
Kwenye miji mikuu ya utandawazi.
.....................................................
KALAMU ILIYOPOTEA
Ile iliyopotea, sasa nimeshaipata,
Kule likopotelea, nami nimeitafuta,
Kalamu ‘litokomea, kwa miezi hii sita,
Kalamu yangu, nishaishika.

Sasa naweleza nyote, mlionisubiria,
Kichofanya sinipate, kalamu ‘linikimbia,
Nikasaka kotekote, bado sikuifikia,
Kalamu yangu, nishaishika.

Leo nimeshaishika, nimeipata kalamu,
Kichobaki kuandika, yote ninayofahamu,
Kwandika pasi kuchoka, yote yote mumu humu,
Kalamu yangu, nishaishika.

Hamu mi sikuishiwa, daima nilitamani,
Tungo sikukaukiwa, zilibakia kichwani,
Imekuwa majaliwa, kalamu i kibindoni,
Kalamu yangu, nishaishika.

.................................
Majira hubadilika,
Miaka inasogea,
Nyasi nazo hunyauka,
Mimea kujiozea,
Lakini nina hakika,
Wewe hutonipotea.

Wewe unayo thamani,
Ya upendo ulo kweli,
U pekee duniani,
Ambaye wastahili,
Kukupa yalo moyoni,
Kwa pendo letu wawili.

Mi nawe twapendezana,
Kwa pendo lililoshiba,
Hakika tunatoshana,
Kwa dhati pia kwa huba,
Pendo tunalopeana,
Linayo tele mahaba.

Wanipa mie furaha,
U zawadi maishani,
Kuwa nawe kuna raha,
Ni raha iso kifani,
Nafurahi kwa madaha,
Waridi langu moyoni. 

...........................
kitaka kunipenda nipende taratibu,
Ukizidisha utaniuwa mwenzio!
Ukitaka kunipa raha basi iwe taratibu,
Ukizidisha utaniuwa mwenzio!

Ukitaka kuniumiza niumize tu kidogo,
Ukizidisha utaniuwa mwenzio!
Ukitaka kunitesa sikuzuwii ila taratibu,
Ukizidisha utaniuwa mwenzio!

Moyo wangu, moyo wangu uendee taratibu,
Ukizidisha waniletea masahibu!
Usiku silali ukiniuliza we ndo sababu,
Taratibu basi utaniuwa mwenzio!

Moyo wangu, moyo wangu unauadhibu,
Basi fanya japo taratibu!
Niondolee madhila yaliyozidia hesabu,
Utaniuwa mwana wa mwenzio!

Taratibu, twende taratibu basi taratibu,
Nitese tu kidogo ukipata sababu!
Ukizidisha moyo wangu wauharibu,
Ukizidisha utaniuwa mwenzio!







from Utundu kitandani https://ift.tt/2XHmxIO
via IFTTT

Comments

Popular posts from this blog

SIMULIZI: PENZI LA DADA SEHEMU 02