Meneja wa Harmonize Afunguka Kumng'oa Harmonize WCB



Meneja wa msanii Harmonize Dr Sebastian Ndege maarufu kama Jembe ni Jembe, amesema alikuwa anatuhumiwa na watu suala la kumchukua Harmonize kwenye menejimenti aliyokuwa ili aweze kufanya naye biashara.


Akizungumza kwenye Show ya SalamaNa inayoruka kila siku ya Alhamisi saa 3:00 usiku kupitia East Africa TV, Sebastian Ndege amesema kuna hisia tatu ambazo watu walikuwa na mashaka naye wakati anamchukua Harmonize.

"Kuna hisia tatu ambazo watu walikuwa wana mashaka mimi kuwa meneja wa Harmonize, moja ni kumfelisha dogo, mbili ni kumpoteza tatu ni kumtoa WCB, lakini ukweli ni kwamba mimi nilisubiri muda wake uishe ili niweze kufanya naye kazi" amesema Meneja wa Harmonize Dr Sebastian Ndege 


from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/3jRqfqF
via IFTTT

Comments

Popular posts from this blog

Zifahamu staili 6 za Kufanya Mapenz

JINSI YA KUMVUTIA MVULANA/MSICHANA HADI KUWA MPENZI WAKO

Nikiwa na Msichana Namkinai, Hivi Nina Pepo au ni Tamaa tu?