TCRA yatoa sababu bando kwisha haraka
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuongezeka kwa mitandao ya simu na kasi ya simu janja nchini ni miongoni mwa mambo yanayochangia ‘bando’ kwisha haraka. Mkurugenzi wa Masuala ya Sekta wa TCRA, Dk. Emmanuel Manasseh, aliyasema hayo jana mkoani Dar es Salaam, wakati wa mkutano wake na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF). Alitaja mambo mengine yanayosababisha kumaliza 'bando' kwa haraka kuwa ni kuongezeka kwa kasi ya mtandao kwenye simu janja mfano kutoka 3G hadi 4G. Mambo mengine, kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo ni ubora wa video na picha unavyoongezeka unasababisha matumizi nayo kuongezeka. "Tuna “application” mbalimbali kwenye whatssap zinafanyiwa ‘update’ mara kwa mara nazo zinatumia data. Watumiaji wengi wa simu kuna vitu vinaendelea kwenye simu yake lakini mtumiaji hajui. Uwapo wa ‘application’ nyingi, zingine hazitumii hivyo zinamaliza ‘bando’,” alisema. Alisema mamlaka hiyo imekuwa ikifanya majaribio mbalimbali ili kuhakikisha watoa huduma ...